Wednesday, July 02, 2008

Bongoland II - Zanzibar

Kwa wale wote mlioko Bongo!!

Tunafurahi kuwatangazia kuwa sinema ya Bongoland II itaonyeshwa katika Tamasha la filamu la Zanzibar (Zanzibar International Film Festival) Sinema ya Bongoland II itaonyeshwa rasmi Jumamosi, July 12 saa moja na dakika 15 jioni.

Kwa mujibu wa mkurugenzi wa tamasha, Bwana Martin Mhando, alisema "ratiba hii imezingatia umuhimu wa kuwapatia watanzania wengi fursa ya kuiona sinema hii, ndo maana ikapangiwa jumamosi". Itaonyeshwa kwanza katika sinema zote zitakazoonyeshwa usiku huo.Kama mnavyokumbuka, Bongoland II ilishutiwa katika jiji la Dar mwaka jana mwezi wa saba.

Wasanii wote katika sinema hii ni wakazi wa Bongo. Hii ni sifa kubwa maana sinema hii itachuana na sinema nyingine nyingi kutoka mataifa mbali mbali ulimwenguni.

Mwezi ujao Bongoland II itaonyeshwa Chicago katika Gene Siskel Film Center katika Black Harvest Film Festival. Soma zaidi hapa. TUTAONANA ZENJ!! - link it to in their own words.

No comments: