Thursday, July 02, 2009

Danny Glover Awasilli ZIFF

Danny Glover akiongea na Martin Mhando

Kutoka LUKWANGULE BLOG:

Danny Glovver Atua Uwanja wa Zenj

Muigizaji maarufu wa Hollywood na ambaye pia ni balozi wa Shirika la Umoja wa mataifa la Kuhudumia watoto(UNICEF) danny glover amewasili mjini Zanzibar leo majira ya alasiri na kusema ziara yake nchini itasaidia kujenga mahusiano zaidi kati ya Wamarekani weusi na ndugu zao wa Afrika.

Muigizaji huyo alisema hayo akiwa uwanja wa ndege wa zanzibar wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Amesema pamoja na kuwa balozi wa uNICEF na kupeleka salamu za UNICEF maeneo anayotembelea pia ana shirika lisilo la kiserikali ambalo hushughulikia mahusiano na nchi za Kiafrika hasa kudumisha utamaduni ulipo wa miaka mingi kati ya wamarekani weusi na ndugu zao waliopo bara la Afrika.

Amesema katika kuimarisha uhusiano huo anajikita zaidi katika mawasiliano na kunyambua tamadunia mbzo anaona ndio ufunguao wa mahusiano kati ya Afrika na bara la Amerika.
Glovver ambaye atakuwa nchini kwa siku tano anatarajiwa pia kushiriki katika masuala mbalimbali ya tamasha kuwa na mahojiano na vyombo vya habari na kufanya shughuli za UNICEF ikiwa ni pamoja na kumuona Rais wa Zanzibar, Abeid Aman karume.
Pia akiwa hapa atashiriki katika kongamano la watoto na amani linaloandaliwa na GNRC na na kuzungumza na watengeneza sinema .

Pichani kama nilivyomnyaka akiwa na Mkurugenzi wa tamasha la filamu za zanzibar Dk martin wakikumbushana enzi hizo za nairobi, kenya mara tu baada ya kumaliza mazungumzo na waandishi wa habari ndani ya VIP ya zanzibar.

No comments: