Friday, November 09, 2007

Binti MKenya ajiunga na jeshi la Bush sasa marehemu

Marehemu Christine Ndururi


Hapa USA wahamiaji wengi wanajiunga na jeshi la Marekani kusudi wapate Green Card, uraia na hela za kulipia masomo. Kuna hata waBongo waliojiunga, waKenya, waGanda na wahamiaji kutoka karibu kila nchi ya dunia katika jeshi la Marekani. Kutokana na upungufu wa waMarekani wanaotaka kujiunga kwa hiari siku hizi ukionyesha moyo wa kujiunga wanakuchukua. Hata wahalifu waliotakiwa kuwa jela wanachukuliwa asante vita vya Iraq.

Jana tulisikia kwenye taarifa ya habari, habari ya kusikitisha. Msichana wa KiKenya mwenye miaka 21 kutoka Lowell, Massachusetts, Christine Ndururi, amefariki dunia akiwa safarini kwenda Iraq. Jeshi linasema kuwa alifariki Kuwait kwa, "Non-related Combat Illness". Yaani ugonjwa usiohusika na mambo ya kupigana.

Sasa ni kitendawili. Wazazi wake walimwona akiwa kambini kwake Texas wiki mbili zilizopita, alikuwa mzima. Jumatatu wiki hii saa tatu za asubuhi (9:00AMEST) waliongea naye kwa simu alikuwa mzima na hakusema anaumwa. Jumanne jioni saa tatu (9:00PM EST) walipigiwa simu na jeshi kuwa amefariki kwa ugonjwa!

Huyo binti alihamia Marekani na familia yake akiwa na miaka 16. Baba yake mzazi alikuwa ni polisi Kenya na alihamia hapa na familia yake. Sasa anaendesha malori. Kaka zake wote pia walijuinga na jeshi la Marekani.

Akiwa anasoma High School alijiunga na Army Reserves. Baada ya kumaliza masomo yake aliendelea kukaa jeshini kwa vile alitaka hela za kusomea unesi. Alikuwa amepangiwa kupelekwa Korea, lakini badala yake jumatatu alishutukia anapelekwa Iraq, ndipo alipiga simu kwa wazazi wake. Familia yake wanasema alikosa raha aliposikia hizo habari.

Na watu sasa wanauliza jeshi la Marekani kinaficha nini kuhusiana na kifo cha huyo binti?

Mungu amlaze mahali pema mbinguni. AMEN.

Kwa habari zaidi someni:

http://www.eagletribune.com/punews/local_story_312093852

http://www.thebostonchannel.com/news/14544601/detail.html

1 comment:

Anonymous said...

REST IN PEACE. The Army needs to explain what happened.