Monday, October 05, 2009

IBUA Film Star Awards - Tanzania


WACHEZA FILAMU CHIPUKIZI KUSAKWA TANZANIA

Mchakato wa kutafuta na kuibuwa vipaji vya waigizaji chipukizi linaanza rasmi na litahusisha mikoa ya Arusha, Mwanza, Mbeya, Dodoma, Zanzibar na Dar es Salaam.
Uibuaji na ukuzaji wa vipaji vya wasanii chipukizi wa filamu ambao hawajawahi kushiriki katika filamu au tamthilia yoyote itawahusisha watanzania wenye vigezo vya kuwa na umri wa miaka 16 na kuendelea, awe na akili timamu, awe ni raia wa Tanzania na ajue kusoma na kuandika.
Mchakato utahusisha kufanya usaili katika mikoa husika hadi watakapopatikana kumi bora ambapo washiriki watachuana kumtafuta msanii chipukizi wa filamu Tanzania.
Mwaka huu kampuni mbali mbali zimejitokeza kudhamini mashindano haya lakini yatatajwa hapo baadaye
Mshindi wa IBUA Film Star Tanzania atajinyakulia zawadi ambayo itatangazwa baadae na pia atapata mkataba wa kushiriki filamu mbali mbali za wasanii wa ndani na nje ya nchi.
Mshindi atapatikana kwa kupigiwa kura na wananchi kupitia kipindi maalumu kitakachoonyeshwa hapo baadae.
Fomu za kushiriki shindano la IBUA Film Stars Tanzania zinapatikana mikoa husika kama ifuatavyo Arusha (Club Silk), Mwanza (Salma Cone), Mbeya (CPMTL Stationery mkabala na ofisi ya mkuu wa mkoa), Dodoma (Zunny Ice Cream Parlour), Zanzibar (Ofisi za Zenj FM), Dar es Salaam (TCC Chang’ombe, Shear Illusions mlimani City, Royal Salon Sinza, Zizzou Fashions). Fomu zitaanza kupatikana tarehe 10 Oktoba 2009.
Mwisho wa kuchukua fomu ni tarehe 30 Oktoba 2009 kabla ya kuanza usaili mjini Arusha tarehe 31 Oktoba na 01 Novemba.
Zoezi la usaili litafanyika kabla ya wananchi kupata nafasi ya kutoa maoni na kufanikisha kuwapata washindi.

Jacqueline Wolper
Afisa Uhusiano-YEC PRODUCTION

No comments: