Tuesday, October 30, 2012

Hurricane Sandy Ilivyotupiga Cambridge, MA!

Wadau, jana Kimbunga Sandy kilipita kwetu. Upepo mkali sijawahi kuona. Hiyo kelele utadhani treni inapita.  Mtaa wa jirani, Howard St., Cambridge, MA walikipata!  Tuliruhusiwa kuondoka kazini mapema jana kwa vile  MBTA walikuwa wanasimamisha huduma ya basi na treni. Nilivyofika Howard St. nilikuwa mitawi ya mti imeanguka na kuponda magari kadhaa. Dirisha zao zilivunjwa.  Leo asubuhi nikapita tena na kukuta usiku mtu wote umeanguka! Yaani imevunjika kwenye kisiki. Bahati mbaya gari iliyokuwa upande wa pili wa barabara umepondwa kabisa! Duh! Lakini uzuri hakuna aliyeumia. Sasa sijui kama bima itamlipa jirani yangu hela ya kutosha kununua gari nyingine.

Tazama picha nilizopiga, Howard St., Cambridge, Massachusetts.


10/29/12 Howard St. Mitawi ya miti imeanguka na kuvunja vio vya magari




10/30/12  Upepo mkali ulivunja ule mti!

Maskini gari ya watu

Mti ulikatika kwenye kwenye kisiki!

1 comment:

Anonymous said...

Poleni. Mambo haya yangekuwa yanatokea mara kwa mara katika nchi zetu masikini sijui ingekuwaje.