Showing posts with label Snow. Show all posts
Showing posts with label Snow. Show all posts

Tuesday, March 12, 2013

Poleni Kwa Baridi Huko London!


Kaka Freddy Macha huko London, Uingereza ameleta taarifa hii.
BARIDI KALI LEO LONDON

by Kitoto

Wamesema mara ya mwisho baridi kali namna hii kutokea visiwa vya Uingereza ilikuwa miaka 30 iliyopita.

Leo kila mtu nliyekutana naye jijini: mzee, mtoto, mwanaume, mwanamke, alilalama na kulaani baridi.



Hata "maglovu" nliyovaa mkononi hayasaidii. Ngumi haikunjiki sawasawa. Miti kule nyuma imepukutika matawi- zimebaki tu kuni kavu. Ndevu zangu zimenyaushwa. Upepo wa kutoboa kisindano sindano ulikuwa ukisaidia baridi kuwa kali zaidi.

Aliyewazidi wote kwa malalamishi alikua ajuza mmoja mzawa wa visiwa vya Karibian. Alihamia hapa miaka 55 iliyopita.

"Nlikuja kusoma na kutafuta ajira. Sipendi na siizoei baridi hata kidogo."

Nkamuuliza kama haipendi baridi kwanini harudi tu kwao kwenye ujoto joto?

Basi linapitisha abiria waliojikunyata ndani.

Ajuza akajibu keshapazoea; lakini asichokiweza baridi.

Rudi basi kwenu.

Ajuza akacheka.

"Baridi kama hii ya leo sijapata kuona." Nilikisia umri wake ushapita miaka 70 na kitu.

Tulikua katika foleni posta. Foleni ndefu kidogo.Foleni za Ulaya, hizo; kila mtu kimya; nje baridi kali.

"Nkishaondoka hapa nakwenda kulala," akatangaza.

Kweli nje palikua kiama.

Kawaida hii sehemu ya kuchezea watoto katika mtaa ninaoishi -huwa imejazana vijana wakicheza kila aina ya utoto, lakini leo palikuwa patupu kama jangwa la Sahara.

Kawaida barafu inapodondoka baridi hupungua, watoto wanacheza; lakini ya leo ilikua na matone machache tu ya barafu. Imeongozana na upepo mkali - wanasema toka Siberia.

Monday, February 11, 2013

Kimbunga Nemo Ilivyotukomesha!!

Wadau, Kimbunga Nemo imemwaga theluji (snow) kibao hapa Boston! Yaani karibu futi tatu!  Sasa kazi kuindoa maana haiyeyuki haraka, na kwa vile ilidondoka haraka kwa kipindi kifupi, ma-plow walishindwa kuondoa theluji kwenye barabara nyingi hapa mjini.

Wazungu hawajazoea kuambiwa wasiendeshe magari yao. Basi siku ya Ijumaa wakawa wanamwita Gavana wetu, Deval Patrick ambaye ni mweusi, Dikteta, MKomunisti nk..  Lakini sasa wanamshukuru na kukubali kuwa alifanya jambo la maana, maana barabara kuu ziliweza kusafishwa haraka.  Hata Connecticut na Rhode Island walifuata nyayo za Gava wetu na kuzuia watu wasiendeshe magari yao! Huko Long Island New York, watu walikoma maana mamia ya magari ya kwama na watu ndani.


Mtaani kwangu Cambridge, MA jumamosi mchana! Plow haikupita hadi jioni. Ilikuwa kazi kweli kufika nyumbani maana hiyo snow iliuwa zaidi ya futi mbili!!!  Nilitoka kazini nimechoka.  Ingawa Gavana alizuia watu kuendesha magari nilibahatika kupata lifi hadi karibu na napokaa.  Kufika mtaani ndo jinsi nilivyokaribshwa! DUUUUHHHH!

Wadau, mgongo unaniuma! Jana ilinichukua masaa kufukua mkweche wangu!!!!

Hii ndo Executive Order ya Gavaana wa Jimbo la Massachusetts kuamurisha watu wasiendeshe magari baada ya saa 10 jioni siku ya Ijumaa Februari 8, 2013.  Ilikuwa ukikamatwa unaweza kufungwa jela mwaka moja na kupigwa faini ya $500!   Gavana kaitwa Fashisti, na kutanawa matui ya nguoni.  Watu walirushusiwa kuendehsa magari saa 10 jino siku ya jumamosi. Hata hivyo, utaenda wapi bila ku-risk gari kukwama kwenye snow!

Tuesday, February 01, 2011

Mwokozi Wetu Tunaopambana na Snow?


(pichani Mnyama aina ya Groundhog)


Kesho macho ya wanaoishi maeneo ya baridi Marekani yako kwa huyo mnyama
aina ya groundhog. Hasa groundhog ambaye anaitwa Punxatawney Phil na anakaa Pennsylvania.
Watu wanaamini kuwa Phil asipoona kivuli chake basi tutaendelea kupigwa na snow na barafu. Kama akiiona basi ina maana haya mateso yataisha. Kwa vile mwaka huu tumekuwa na winter mbaya sana watu hawatalala leo usiku wakingojea kusikia Phil atasemaje!
Phil, Please don't see your shadow!
Kwa habari zaidi za Groundhog Day na Phil someni:

Snow Imezidi Boston! Tumechoka!



Yaani leo ni siku ya kwanza ya Februari. Tunapigwa na snow tena. Kesho tutapigwa tena. Ikiisha tutakuwa na karibu futi mbili na nusu ya snow! Hiyo ni juu ya ile snow ambayo ilianguka majuzi! Hatuna pakuiweka. Ni hatari kutembea na kuendesha magari shauri ya milima ya snow. Watu wameonywa kuwa ikianza kuyeyuka kutakuwa na mafuriko!

Thursday, January 27, 2011

Hii Winter ni Mbaya Mno!


Wadau, sijui huko ulipo lakini hapa Boston tunapigwa na theluji (snow) si kawaida. Sasa hatuna pa kuiweka. Wanasema kuwa snow ya mwaka huu itaingia katika vitabu vya historia. Sasa watu wanatania na kusema kuwa hali ikiendelea kama ilivyo sasa itakuwa kama wale wanaodesha magari yao pichani! Kama snow ingekuwa inayeyuka kabla ya nyingine kuanguka hali isingekuwa mbaya. Lakini sasa kuna milima ya snow kila mahala!
Kwa habari zaidi soma:

Thursday, January 13, 2011

Tunapambana na Theluji na Barafu!






Ni msimu wa winter (Baridi) hapa Marekani. Tunatamani joto la Dar. Hizi picha nilipiga hapa Cambidge, Massachusetts leo asubuhi.