Wednesday, April 07, 2010

Kutozwa Mapesa Kwenye Ndege Inazidi... Sasa Hata Kutumia Choo!

Haya, leo tumesikia kuwa tutatozwa hela kwa ajili ya 'carry on' bag kwenye Spirit Airlines. Mjue na airlines zingine zitaiga! Haya sasa Ryan Air wanasema utatozwa hela kutumia choo kwenye ndege! Jamani, sasa kama mtu kambanwa, ndo akae nayo mpaka ndege itue! Hii sasa ni uchu wa pesa!

Kaa habari zaidi:

http://www.cnn.com/2010/TRAVEL/04/07/ryanair.lavatory.fee/index.html?hpt=T2

http://www.latimes.com/business/la-fi-spirit7-2010apr07,0,5945292.story?track=rss

3 comments:

Anonymous said...

Jamani! Si bora waongeze hizo fee katika bei yak tikei? Waseme kila mtu ataenda angalau mara moja. Mtu akiwa na tumbo la hkuhara je, itakuaje kama hana hela!

MICHUZI BLOG said...

Hahahaaa poleni. Huku bado hawajaanza. wakianza sijui itakuwaje..

Anonymous said...

Ndo hapa mtu anahangaika kutafuta chenji kutia mle. Mwisho foleni inaanza.

Na je, hao wahudumu kweneye ndege wako tayari kusafisha mikojo na mavi ya watu wakipata eksidenti kwa ajili ya kushindwa kubana haja mpaka ndege itue?