Monday, April 01, 2013

Utani wa April Fools! Tambi unaota Kwenye Miti

TAMBI UNAOTA KWENYE MITI HUKO USWISI!

Mwaka 1957 BBC walitangaza kuwa Uswisi inavunwa Tambi kwa wingi.  Walisema kuwa wamefanikiwa kumwua mdudu anayeua miti ya tambi (spaghetti weevil) na pia msimu wa baridi (winter) haukuwa mbaya sana, hivyo tambi unaota kwa wingi.  Watu waliaamini na wengine walidiriki, kuuliza wanawezaje kupata mtu wa tambi, ili walime wenyewe!



Kusoma habari kamili BOFYA HAPA:

3 comments:

Anonymous said...

Miminina mti unaota pesa tena dola!

emuthree said...

Aisee, wakati naanza kusoma nilishahisi jambo, ....nilikuwa sijasoma kichwa cha habari. Ni nani aligundua huu utani wa kudanganyana,...

Anonymous said...

Yaani nimecheka! Kumbe wazungu wengine hawakuelimika! Eti tambi inayotokana na unga ngano unaota kwenye mti!