Saturday, January 10, 2015

Mr Sugu Apata Ajalia ya Gari Iringa

 Kutoka Facebook:


Picha zikionesha Mbunge wa Mbeya mjini Mr Sugu na rafiki yake wakiwa kando ya gari lao baada ya kupinduka katika mteremko wa Kitongo leo.

MBUNGE wa jimbo la Mbeya mjini Joseph Mbilinyi a.k.a Mr Sugu (Chadema) amenusurika kifo baada ya gari lake kupinduka katika mlima wa Kitonga wilaya ya Kilolo kwenye barabara kuu ya Iringa - Dar es Salaam.

Ajali hiyo imetokea mchana wa leo wakati gari la mbunge huyo likiwa na watu wengine wanne likitokea Mbeya kuelekea jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo vyanzo vya habari hizi viliueleza mtandao huu wa www.matukiodaima.co.tz kuwa mbunge huyo amepatwa na michubuko kiasi na hakuna aliyepoteza maisha katika ajali hiyo .
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Iringa Ramadhan Mungi akimethibitisha kutokea kwa ajali hiyo japo amesema taarifa kamili zitapatikana mara baada ya askari waliokwenda eneo la tukio kurejea.




No comments: