Sunday, January 25, 2015

Mwanaume Ajifanya Mwanamke Ili Apate Kazi Dar

 Kutoka Facebook

 
LAHAULA UMEISIKIA HII??? Katika hali isiyo ya kawaida kijana mmoja mwenye jina la Naftaeli Mbowe ameibua mapya jijini Daresalam. Kijana huyu ambaye ni graduate wa sociology katika moja ya vyuo hapa nchini alimaliza chuo mwaka 2011 na kufaulu vizuri sana. Kutokana na maisha ya kuiga akiwa chuoni alijitumbukiza kwenye siasa na kujidai ni mwanaharakati wa chadema hivyo kutokana na uwezo wake darasani aliweza kujenga hoja zilizomfanya akajulikana na uongozi wa juu wa CDM.

Alipomaliza chuo kijana huyu alichukuliwa na viongozi hawa wa ufipani kwa ahadi kuwa aendelee kukisaidia chama ambapo alipangwa kwenye department ya matusi mtandaoni kwa ujira wa kulipiwa chumba jijini daresalam na kulipwa shilingi laki moja kama posho ya mwezi. Chakula na vinywaji walikuwa wanapata kwenye getho walilopangiwa mtaa wa kimara Bucha. Kijana huyu amekuwa akifanya kazi hiyo kwa muda mrefu na yupo humu humu kundini kwa jina bandia. Kutokana na chama kufilisika siku za hivi karibuni kwa kuendekeza kesi za kupinga kila jambo la serikali na safari za viongozi zisizokuwa na tija vijana hawa walitelekezwa.

Kijana huyu toka mwaka 2013 amekuwa akisota mtaani bila mafanikio yoyote ndipo alipoamua kujibadilisha jinsia kwa kuvaa nguo za kike na kusuka rasta ili aombe kazi za uhasegirl na azma yake hii ilitimia. Aliajiriwa na mama mmoja asiyekuwa na mume maeneo ya ubungo msewe na hakuweza kumshtukia kwa muda wa miezi miwili kwani aliishi kwa umakini mkubwa sana. Juzi ijumaa limemtokea la kumtokea baada ya mtoto wa kiume wa mwenye nyumba kwenda kumpiga chabo akioga ili afaidi kuona maumbile ya beki tatu huyo.

Alishangazwa na alichokiona ikabidi amkasirikie mama yake sana kwa kumleta mwanamme ndani ya nyumba yao huku akisingizia ni mwanamke. Gadhabu zilimpanda zaidi kwa kuwa njemba hilo lilikuwa likilala na dada yake ndipo njama za kumuumbua bila mama yake kujua ziliposukwa.Alipotumwa sokoni mtoto wa mama wa kazi ambaye ni wa kiume aliamua kufuatilia nyuma ili kumuumbua, huku akiwa na wenzanke walimsimamisha na kumshushia kipigo cha maana ndipo alipoelezea kisa kizima.

Vijana wa chadema mliopo kwenye magetho mbali mbali okokeni sasa njooni ccm. mtaumbuka mjini hapa.

1 comment:

Unknown said...

Chemi acha uongo, hiyo picha iko kwenye mitandao kwa muda mrefu tu. Hiki kiblogu chako siku hizi kimekuwa kama magazeti ya Shigongo