Tuesday, June 26, 2007

Mjue Msanii Thecla Mjatta

Thecla Mjatta in Arusi ya Mariamu
Thecla Mjatta at a screening of the film, Tumaini
Thecla Mjatta (in baibui) with other cast of the film, Mlima Kolero
(photo from Jiachie blog)


Mama Thecla Mjatta ni mwigizaji mkongwe wa Tanzania. Huenda mnakumbuka zile michezo za kuigiza kwenye redio. Tulikuwa tunazingojea kwa hamu kila wiki, hasa kwa vile wakati huo hakuna TV miaka ya 70 na 80. Pia aliigiza katika michezo ya kuigiza kadhaa.

TV ilivyoanza alianza kuigiza kwenye michezo ya television. Mama Thecla pia ameigiza katika sinema kadhaa na kucheza kama watu ambao hamwezi kusahau.

Katika sinema ya Arusi ya Mariamu, anaigiza kama shangazi yake Mariamu, na hamtasahau anvyopagawa.

Katika sinema ya Maangamizi the Ancient One aliigiza kama mama wa mhusika mkuu, Samehe. Samehe, alishuhudia kifo cha cha kuunguzwa na moto na baba yake mzazi amabaye alikuwa ni mchungaji mwenye imani kali ya dini. Sinema ya Maangamizi iliteuliwa kama sinema ya kwanza kutoka Tanzania, katika mshindano ya Oscars mwaka 2001 (Foreign Language category).

Pia ameigiza katika sinema za Simu ya Kifo, Tumaini, Mzee Mkude, na mlima Kolero. Hivi karibuni ataigiza katika sinema ya Bongoland II, akicheza kama mama yake mhusika mkuu, Juma.

Kwa habari zaidi za sinema ya Bongoland II nenda : http://www.kibirafilms.com/bongoland/home.html

No comments: