Thursday, July 05, 2007

Safarini Tanzania

Kwa sasa niko Dubai. Natumia keyboard enye maandishi ya kiarabu. Bahati nzuri najua keys ziko wapi. Airport ya Dubai ni safi sana. Hata bathrooms nu safu kuliko za JFK New York. Duty Free nzuri pia.
Ila joto. Air condition haifanyi kazi vizuri.

See you in Dar soon.

10 comments:

Anonymous said...

Chemi unaenda kuolewa au?
hahahahahahaha.

Anonymous said...

Safari njema Chemi. Karibu kwetu Mbagala dada!!!

Anonymous said...

safari njema. Usisahau kununua "bling bling"

Anonymous said...

chemi mambos.
mimi ni mmoja wa mpenzi wa hii blog. Yaani nakuzimia sana mambo yako...dont get me wrong...labda niseme nakuadmire sana. Ningependa utupe historia fupi ya maisha yako...una familia? watoto/mtoto, n.k. Please...
Marie.

Anonymous said...

Haya Chemi,
Karibu Dar.Wengi tunahamu ya kukuona ila hatujui utapatikana wapi na pengine utakuwepo kwa muda gani hapa Dar.

Anonymous said...

Hey,blogger wowote wa kibongo, shukrani kwa kazi unayofanya. Unajua kitu kimoja kuna huyu mbongo anaitwa hakingowi nae kafungua kijiblogu chake na sasa naona amekuwa pain in the ass yaani picha zoooote anacopy kwako then anapaste kwake yaani upuuzi mtu halafu anaanza kujidai eti ooh sijui wadau wengi wameomba picha hii na upuuzi mwingine kibao kumbe ukiangalia picha katoa hapa au kwa michuzi au kwenye site nyingine. kwa kweli huyu jamaa ni mpuuzi sana na HAWEZI kabisa mambo ya kublog sasa nilikuwa naomba mumbanie picha zenu anazoomba/anazoiba kila kukicha. Kwa kifupi jamaa angekuwa na picha zake ingekuwa safi lakini anajidai sana kwa picha za wizi. Hiki kijamaa haki ya nani kwanza kiko bongo flava oriented sana, na kazi kujipendekeza kwa watu maarufu ambao hata kuonana nao hajawahi, yaani he like riding other people deaks yaani. Mbanieni na picha zenu bana, mwambie anunue kamera yake na aanze kuwapiga watu picha yeye mwenyewe au kama vipi apitishe bakuli kama Mjengwa alivyofanya na kama watu wataamua kumchangia itakuwa good for him. Wewe haki nashauri ufunge upuuzi wako huo. Na wewe kaka michuzi naomba ufanye hivyo !!!!!!!

Fadhy Mtanga said...

wow!
karibu sana Tanzania.
najua umekwisha zowea maisha ya huko, lakini nyumbani ni nyumbani.
usikonde kwa vumbi utakalolikuta Temeke hadi Mbagala, vumbi la makongo juu.
tatizo la foleni bado lipo pale pale. ila maisha yanazidi kuwa magumu na kuna bajeti ya kufunga mikanda. karibu ukiwa tayari na mkanda unafunga vema,(pesa za kutosha)
lakini bado Tanzania ni nchi nzuri sana hata nashindwa kuielezea.ukiondoa tofauti ndogo ndogo za kiitikadi bado tunavumiliana sana kisiasa kiasi kwamba ni jambo la kawida kwa Hamad na Karume kuketi meza moja na kufurahia jambo.
nisikuchoshe hizo zilikuwa ni longolongo tu!
karibu sana nyumbani. mkoani Iringa ndo wanavuna mahindi, bila shaka utapata nafasi ya kujimuvuzishia nafaka bora.

Anonymous said...

Anonymous wa july 7 5:55 mi nadhani uwe unachnguza sana kabla hujaanza kuandika upupu wako hivi unaakili wewe?Ama unatafuta nini maana sikuelewi wewe shida yako ni nini asa kumgombanisha huyu food for thought na wanablog wenziwe au ni vipi?Nakumbuka d chemi nae wakati wa msiba wa chifupa Amina alichukua picz kutoka blog mbalimbali ikiwemo ya huyu food for.....?Hii si kazi yako kumfuatilia mtu namna hii asie omba msaada kwako na isitoshe huyu kaka wa watu hata hakujui.Mimi Namtakia HAKI kazi njema endeleza mapambano maana hakuna mtu apendae mafanikio ya mtu pia da chemi kazana kutupa habari...Haterz kip on HATING maana hamna faida mnayoipata....

Jules S. Damji said...

Safari njema kabisa..I am jealous!!
Na mimi piya, nimeamua, nita rudi nyumbani mwezi wa kumi bada ya muda mrefu sana.

Anonymous said...

Whats up guys,
Ninahitaji kujua kama bado kuna ruhusa ya kuingiza gari nchini for free after owning it for more than a year in other country.
Thank you
Joel