Tuesday, July 31, 2007

Bongoland II - Manzese


Picha hizi zinatoka Kwenye site ya Sam Fischer, ambaye ni Cameraman kwenye sinema ya Bongoland II. http://web.mac.com/samfischer/iWeb/Site/Africa%20Photos%202.html
Hapo juu Star wa Bongoland II Peter Omari, na actor mwingine wanajiandaa kuacti scene kwenye gari.
Scene inapangwa. Hapa Sam Fischer anapanga jinsi atakavyopiga picha ya scene ya kupigana.

Stunt Coordinator, Jason Hilton, akicheza Kung Fu na watoto wa Manzese.


Hapa wanapadisha camera kwenye crane.



Akina Sam walitengeneza Crane kwa ajili yakupandisha camera na kupiga scene kutoka juu. Ila bahati mbaya crane ilivunjika na haikuweza kutumika.




Uchochoro wa Manzese. Amini msiamini, zamani hii ilikuwa barabara ambayo magari yalikuwa yanapita. Baba mdogo alikuwa ana drive hapo na kupaki gari yake kwenye gereji yake. Sasa asante ujenzi holela hakuna barabara tena.



Muongozaji na Mwandishi wa sinema ya Bongoland II, Josiah Kibira, akifika kwenye nyumba ya Manzese.




Hapa Timu ya Bongoland II wana survey kama nyumba itafaa kwenye filamu. Nyumba hiyo ni ya marehemu baba yangu mdogo, Prof. Crispin Hauli. Na inatumika kwenye sinema ya Bongoland II kama nyumba ya 'Uncle'.

No comments: