Monday, July 30, 2007

Siti Binti Saad

Siti Binti Saad 1880-1950

Kama kungekuwa na uwezekano wa kurudi nyuma katika miaka na kukutana na mtu maarufu ambaye aliwahi kuishi duniani, ningependa sana nikutane na Bibi Siti Binti Saad.

Bila shaka kwa sasa kuna watu wengi Tanzania ambao hawajawahi kumsikia, lakini Bibi Siti Binti Saad ni mwanzilishi wa Taarab, Tanzania. Siti alizaliwa katika familia maskini huko Zanzibar, lakini aliweza kuchukua muziki iliyokuwa unaimbwa kwa kiarabu na kuanza kutunga nyimbo zake na kuimba kwa Kiswahili. Pia zamani taarab ulikuwa kwa ajili ya matajiri tu, lakini aliufanya uwe kwa ajili ya wote.

Bibi Siti pia alisafiri hadi India kurekodi santuri kadhaa. Mwanafunzi maarufu wa Bibi Siti, bado yu hai, naye ni mpendwa Bibi yetu, Bi Kidude.

Nina website kuhusu maisha ya Siti Binti Saad. Na ni:

http://groups.msn.com/SitiBintiSaad/tributetositibintisaad.msnw


Karibuni.

No comments: