Friday, January 15, 2010

Mbgaguzi Rush Limbaugh Amchamba Rais Obama juu ya Haiti


Yaani sielewi kwa nini huyo mbaguzi, evil hate monger, Rush Limbaugh bado anatamba hewani na kipindi chake cha redio. Jana kawaambia watu wasipeleke misaada Haiti, kwa vile tayari Marekani imekuwa ikisaidi nchi hiyo miaka mingi. Je,ingekuwa nchi ya wazungu kama Bosnia angesema hivyo? Anasema kuwa Rais Obama anapeleka misaada huko kwa vile ni nchi ya weusi na anataka kupendwa na weusi! Ndo maana majuzi huyo shetani Limbaugh alipopatawa na matatizo ya afya watu walimombea afe! Jitu jina roho mbaya kweli kweli! Anafaa kuwa Grand Wizard wa KKK!

Nchi ya Haiti imeangamizwa na tetemeko la ardhi. Watu hawana maji, wala chakula. Hawana sehemu ya kulala. Maelefu na maelfu ya watu wamekufa na hawajazikwa. Serikali ya Haiti imekufa kwa sasa, yaani hali ni mbaya mno kule. Kwenye TV tunaona picha za watu wameumia hakuna tiba. Mtu yuko hai, huko kuna karibu yake kuna maiti. Jamani!

Halafu kuna wabaguzi kama huyo Rush Limbaugh wanaowaambia watu eti wasisaidie nchi hiyo. Lakini si siri kashasema mengi mabaya juu ya watu weusi wa Marekani na dunia nzima. Si weusi tu, hata maspanish na wengine. Anaona kama wazungu ndo binadamu na wengine siyo!

Kwa habari zaidi soma:

http://www.nydailynews.com/news/politics/2010/01/15/2010-01-15_rush_limbaugh_haiti_earthquake_comments_are_really_stupid_says_white_house_press.html

8 comments:

Mzee wa Changamoto said...

Umenena vema Da Chemi. Kuna wengi wanaodhani kilichotokea Haiti ni makosa yao. Si kweli. Mother-nature amefanya maasi makubwa. Haiti imekuwa kwenye DHORUBA mbalimbali za kisiasa na kijamii. Leo hii 50% ya population wako under 18. Port-Au-Prince imaharibika na hata majengo yaliyosimama yameathirika kiasi kwamba yanahitaji kuvunjwa kwani hayafai kuishi. Lakini bado Rush anaendeleza ubaguzi. Si yeye pekee mwenye kauli za kibaguzi. Mtazame huyu "mtumishi wa Mungu" Pat Robertson alivyouchefua ulimwengu kwa kauli zake hapa http://www.huffingtonpost.com/2010/01/13/pat-robertson-haiti-curse_n_422099.html
Rush ni kati ya watu wanaotumia vubaya freedom of speech humu nchini. Kauli zake za kibaguzi ni kero na kwa hakika YEYOTE ANAYETAKA KUSITISHWA KWA MSAADA WA HAITI KWA KUWA TU NI WEUSI AMA NI MASKINI NA ALAANIWE.
Jioni njema dada

Anonymous said...

Da Kemi huyo bwege tu wala hatubabaishi sasa kila mtu anamdharau hajijui tu ni wachache (wajinga wenzie)ndio wanao msapoti, kwanza hiyo misaada hajatoa Obama peke ya kuna hao2 waupe wenzie wametoa na wanaendelea kutoa na Clinton je mbaona hamsemi... jinga hili sasa tumelidharaaaaaaaaaaaaaauuu

Mdau USA

Anonymous said...

NA WEWE MBAGUZI ,YEYE HAKUTAJA BOSNIA.

Anonymous said...

kwani lazima muwepo huko chemi? si mrudi kwenu? waacheni nchi yao tuone box watabeba wenyewe?

warabu bada ya sept 11 walikuwa walibaguliwa wakidhalilishwa na kufanyiwa kila vituko eti ni magaidi. sasa wengi wao wanakwenda holiday asia n frica. wamewaachia wenywewe bara lao.

nanyi rudini kwenu tone. dunia ya sasa mtu mweupe ili aendele kuwa juu anamhiaji mwafrika sasa huyo anaebagua inaonekana hajenda shule kabisa.

Anonymous said...

DA CHEMI thanks for giving us news as always. I can assure you that many people are appreciative of your efforts.

The world is grieving for what happened in HAITI. Imagine you woke up in the morning and found out that the whole of your family is wiped out! If that is not enough, you also realised many of the people and friends you know, they’ve been crushed to death. This is just imagination and it’s always easy to imagine but in reality none of us has ever experienced such a traumatized moment but people of HAITI have!

To add an insult to the wound, a so called ‘man of the god’, evangelist Pat Robertson came up with a controversial statement that “HAITI has been cursed by devil pact”. It’s so painful to take this idiocy especially at the time when you see those poor injured toddlers are being excavated from debris of demolished houses and some are still buried underneath! He sincerely lacks common sense and sense of humour! Man of the god! What god?!

I don’t know his evangelical beliefs but even if what he says is what he believes, I think he should have kept that ‘opinion’ for him and himself. He was called “stupid” by White House spokesman Robert Gibbs and I add, he uses his balls to think instead of his head.

Da CHEMI, you also need to name and shame this guy just like you did to evil hate monger, Rush Limbaugh . They’re all in the same brackets.


________________________________
Jua Kali

Anonymous said...

Alivyougua majuzi na mimi nilifanya ni sababu ya mimi kumpiga mavoodoo apate heart attack!

Anonymous said...

Angekufa huyo shetani,yani angejua tunavyomdharau asingethubutu kufungua domo lake na kuongea upuuzi kama huo.
he has no heart at all,he rather die

Anonymous said...

Kama amethubutu kushawishi watu wasipeleke misaada kwa waathirika wa HAITI huyo kweli ni shetani na kweli hana moyo kama alivyosema mdau mmoja hapo chini,sijui hiyo heart attack kaipataje?! na huyo msimuombee afe mwacheni tu Mungu kamrinyulia vissa yake apate kulipwa hapa hapa duniani ahera kwende hesabu tu!

Watu wa mataifa mbali mbali wanalia wakiangalia dhahama iliyowapata na inayoendelea kuwapata watu wa Haiti halafu yeye anathubutu kushawishi watu wasipeleke misaada?!
Mimi nipo Dubai na juzi nilikuwa natembea madukani nikaingia duka la electronics, sehemu ya maTV kulikuwa na Tvs zinaonyesha HAITI kutoka channel ya CNN, Watu waliokuwapo hapo dukani wengi wao waliishia kuangalia kwa masikitiko hiyo habari kuliko kuendelea na shopping zao, katika kuangalia angalia nikamuona kijana mmoja wa kiume wa kihindi akiafuatilia habari hiyo huku machozi yakimbubujika kama vile ni kwao, kuna mtu karibu yake akamuuliza kama aliwahi kufika HAITI; akasema hajawahi na wala hakuwa akiifahamu sana nchi hiyo, lakini ameshindwa kujizuia sababu maafa waliyopata huwezi mtu kumtakia hata adui yako yamfike!
(umeona watu wenye mioyo hao?!)
Sembuse huyo Shetani hao Haitians si jirani zao marekani moja ? kweli mtu unakuwa na roho mbaya kwa mwanadamu mwenzio kama vile utaishi milele hapa!
Mungu na asituonyeshe tena janga kama hili, AMINA.