Friday, February 18, 2011

Wanafunzi wa Mwenge University Wafukuzwa Chuo!


Wiki chache zilizopita wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mwenge huko Moshi walishiriki katika mgomo. Sasa wamepewa barua wajieleleza la sivyo watafukuzwa kwa kuvunja sheria za Chuo.

Ukibofya kwenye picha utaweza kusoma barua.

3 comments:

Anonymous said...

poleni wanafunzi,
www.pamojasms.com

Anonymous said...

Tumieni www.pamojasms.com kupashana habari dunia nzima

Anonymous said...

Kabla ya hawa wanafunzi kupata msaada kutoka kwa wanasheria, ni vyema wakajijua kama wanaumoja ulioimara na kusimama kutetea kile kilichotokea! Kwa uzoefu wangu katika mambo haya ya migomo chuoni, ni kwamba vyuo vina student by-law ambazo ni sheria ndogondogo zinazowahusu wanafunzi. Kawaida migomo huwa haiibuki hivihivi tu, hutokea pale makubaliano kati ya wanafunzi na uongozi husika wanaposhindwa kufikia makubaliano!

Lakini hawa wanafunzi watuambie wazi kama mgomo huu ulipewa baraka na Serikali ya wanafunzi, kama ulipewa baraka na wanafunzi, basi hata wanafunzi wenyewe wanaweza kuwarudisha wenzao kwa umoja wao! Je, kwanini wanafunzi wameamua kurudi madarasani kama madai yao hayajatimizwa? au waligoma tu ilimradi? Let them (students) be openly on that ili wapate msaada kutoka kwa wadau wa sheria!