Monday, February 06, 2012

Mimba na Siri ya Precious

Imeletwa na Mdau YM:

Mimba na Siri ya Precious

MIMBA
Mimba ilitungwa baada ya baba kutoa hongo kwa kimada

Ili kuthibitisha kama ni mimba kweli kimada akatoa rushwa kwa daktari ili apimwe harakaharaka kwa kuwa kulikuwa na msongamano wa wagonjwa

Kila alipoenda kliniki wakati wote wa Ujauzito alitoa 'chai' ili ahudumiwe vizuri na wauguzi na madaktari

Hata wakati wa kujifungua akatoa 'chai' kwa manesi apate huduma safi

BAADA YA KUJIFUNGUA
Baada ya kujifungua aliendelea kutoa hongo awe wa kwanza kuhudumiwa, mwanae awe wa kwanza kuchomwa sindano za Chanjo n.k.

Mwanae akaitwa 'Precious'

ELIMU KWA PRECIOUS
Kuandikishwa chekechekea akatoa hongo ili Precious apate nafasi katika shule nzuri kwa kuwa nafasi zilikuwa chache, Precious anaangalia

Kuandikishwa shule ya msingi mchezo uleule, Precious anaangalia

Tena sekondari akatoa 'Chai' kwa mwalimu wa Hisabati ili Precious apate alama nzuri

Chuo kikuu Precious hali ikawa ngumu, akagawa uroda kwa mkufunzi ili apate alama nzuri

KAZI
Precious akagawa uroda ili apate kazi, akapata

Precious akatishiwa mara kwa mara kufukuzwa kazi kutokana na utendaji mbovu kinga ikawa ni kugawa uroda

Akatumia nafasi yake kwa manufaa yake binafsi

Kwa tamaa ya vitu vya thamani kuliko mshahara wake akaendelea kupokea rushwa

NDOA
Kwa kuwa wazazi wake (baba yake) hakuwa mwaminifu katika ndoa yake (Precious ni mtoto wa kimada), naye Precious hakuona sababu ya kuwa mwaminifu ktk ndoa

Watoto wake wote walifuata mlolongo kama wa kuzaliwa kwake

KIFO

Hata alipougua ghafla , hongo ikatumika apate huduma bora lakini Mungu alimpenda zaidi

Walipoenda kuchonga jeneza, wakakuta kuna order nyingi ikabidi watoe 'Cha Juu' ili kuchukua jeneza lilokuwepo tayari

Wakati wa mazishi Kwaya iliyotakiwa kuimba wakati wa Maombolezo ilikuwa na safari , ikapewa 'cha juu' ili kuahirisha safari

MWISHO

Kwaya ikaimba na Kumsifia Precious alivyokuwa 'mtumishi mwema wa Mungu', tena wakamwomba Mungu ampokee kwa mikono miwili , amuepushe na Moto wa milele.

Risala ikasomwa, na kusifia utumishi wake uliotukuka, tena kaacha pengo lisilozibika.


TAKE HOME MESSAGE
Wazazi 'huwapakaza' watoto wao matope ya dhambi toka pale mimba inapotungwa hata baada ya kuzaliwa

Watoto wote huakisi tabia walizojifunza toka kwetu, kama wazazi (Observational Learning)

Kama hatuwezi kuwa wawazi hasa pale kaburini hata kwa mtu aliyekufa na sifa mbaya akasifiwa basi tunahalalisha matendo mabaya aliyoyafanya marehemu.

Ili Kupambana na Rushwa twahitaji kuanzia wakati wa Ujauzito, mtoto azaliwe bila rushwa, akue bila rushwa n.k

KWA LEO NI HAYO TU!!!

No comments: