Sunday, May 25, 2014

Mama Bishanga Amlilia Kuambiana

OHIO: USA, MAMA BISHANGA AMLILIA KUAMBIANA

Nimepokea kwa huzuni taarifa ya kifo cha msanii mwenzagu wa fani ya filamu marehemu Adamu Philip Kuambiana, ni pigo kubwa kwa tasnina yetu na kwa taifa pia kwa kuondokewa na mtaalamu mahiri kama yeye, namuombea usingizi wa milele wa amani.

Adamu alikuwa mtoto wa mwalimu Philip Kuambiana mwalimu wangu wa major yangu chuoni Theater Arts, alikuwa director na producer mkali sana. Na kama itakumbukwa nilihojiwa mwaka 2001 baada ya kupokea  Award ya The Best Actress wa mwaka wa 2001, nilieleza mengi pamoja na production tuliocheza  mbele ya wabunge na  Rais wa kwanza Mwl Julius Nyerere, Marehemu Mwalimu Philip kuambiana ndie aliidirect, na alisimamia Nyanja zote, mandhari, costumes, sound, na hata lebasi za ulibwende (wale tuliokuwa darasa moja mnaikumbuka hiyo?), na alikuwa very serious kazi inapoanza, alikuwa akitutania kila tunapoanza mazoezi kuwa kila mtu aende chooni kabisa kwani kazi ikianza ni moto moja kwa moja, kazi moja tu, na hakika matokeo ya production zake yalikuwa mazuri sana. Na ndio hapo nilimjua Adamu akiwa mdogo sana mwaka 1982-83.

Mwaka 2011 niliporudi tz kufunga ndoa ndipo nilipoonana tena na Adamu akiwa mkubwa kabisa, na tulipanga kuicheza tena jukwaani ile production ya mtihani wetu wa mwisho, alisema pamoja  kuwa alikuwa mdogo sana lakini anakumbuka ile production ya mfalme Odepasi (The King Odepus) kutoka kwenye kitabu cha Shake Spear, ambayo kwa kifupi mfalme Odepas alifungwa miguu na mikono kwenye mti na kupewa wafugaji wakamtupe mtoni akafe maji, Odepus alikuja kuwa mfalme baada ya miaka mingi, alimuua baba yake bila kujua kuwa ni baba yake na alimuoa mama yake na kuzaa nae watoto wawili bila kujua! ni production nzuri sana na ninasikitika kuwa Adamu amefarika na ndoto ya kuicheza hii production tena jukwaani sijui ndio vipi! Pamoja na yote namuombea Amani ya kudumu,

Mwisho nawapa pole kwa familia yake, na kwa taifa Zima.

 Bwana alitoa, Bwana ametwaa; Pumzika kwa Amani Adamu Philip Kuambiana.

Christina Innocent Marolen
Mama Bishanga
OHIO  

The Late Adam Kuambana

No comments: