Saturday, April 14, 2007

Bongoland 2


(Photos courtesy of Muhidini Michuzi)

Naona Kibira Films International inasonga mbele na maandalizi ya kupiga picha ya Bongoland 2, Tanzania mwezi Julai. Wasanii nchini Tanzania wanatoka kwa wingi kujaribu kupata nafasi ya kuigiza katika hiyo sinema. Katika picha za juu, ni baadhi ya wasanii waliotokea kwenye Casting Call.
Sinema itakuwa sehemu ya pili kuhusu maisha ya Juma Pondamali, ambaye katika sinema ya Bongoland, alishindwa na maisha ya Marekani. Hatimaye aliamua kurudi zake Tanzania, tena baada ya waBongo wenzake kumchangia nauli ya tiketi. Je, alivyorudi maisha yake yalikuaje?
Kibira Films, inaongozwa na Bwana Josiah Kibira, wa Minneapolis, Minnesota. Kampuni hiyo ilitengenza sinema ya Tusamehe. Mimi naigiza katika sinema hiyo kama Mama Kurusumu.

No comments: