Saturday, April 28, 2007

Watalii waharibu Mbuga za Wanyama

(UTANI)

Jamani, jamani, jamani. Inasemekana mtalii kutoka USA alienda kwenye mbuga ya wanyama na backpack mgongoni. Alikuwa kwenye land rover na watalii wengine. Sasa walivyoona simba, waliingiwa na kiwewe na backpack ikaburuzwa kwenye chuma fulani kwenye land rover yao. Kwa bahati mbaya chupa ya shampoo ilianguka mbugani. Shauri ya woga ya kuliwa na hao simba, waliamua kuacha chupa pale pale ilipoanguka.

Watalii waliondoka na gari yao. Sasa simba na utundu wake kaona hiyo chupa, kaanza kulamba lamba maana ilikuwa na ladha ya nazi. Mwisho kaipasua na kulamba shampoo yote. Baada ya wiki moja watalii walirudi na kuona huyo simba wa kiafrika kawa simba wa kizungu (pichani)!

3 comments:

Anonymous said...

Utani mzuri huu, nadhani ni tangazo la biashara au sio?
Lete stori kuhusu lile shindano la 'dancing with the stars' (abc channel???)!

Anonymous said...

Nimeona kwa Michuzi umetoa e-mail yako, mi naomba utoe na. ya mobile yako au landline nikupigie nikipata nafasi: ni maongezi ya kawaida/kirafiki tu!

Mikundu Matako Makalio Manundu said...

Looh, huyo simba alipoimaliza hiyo shampoo naona akapitia bush-saloonm maana naona kapambwa!!