Friday, September 05, 2008

Sinema Edge of Darkness imepata pigo!

Robert DeNiro akiwa kwenye seti hapa Boston juzi

Wadau, ile sinema, Edge of Darkness ambayo nimo kama background (extra) policewoman imepata pigo. Moja wa waigizaji wakuu, Robert DeNiro, amejitoa ghafla kwenye sinema. Alikuwa ameshashuti scene kama mbili hapa Boston. Scenes zilikuwa kwenye golf course.

Yaani tunashangaa imekuaje tena. Watu walikuwa wamepania kweli kuwa kwenye scenes na DeNiro. Sasa itabidi wazishuti tena. Mimi sikuwepo kwenye hizo scenes zake za wiki hii.

Wanasema kuwa wanatafuta mwigizaji mwingine kuchukua nafasi yake. Kwa sasa inabidi wabadilishe ratiba ya kupiga sinema, na watashuti scenes ambazo character ya DeNiro (Darius Jedburgh) haimo. Mjue leo watu wamehaha kutafuta jeti kwenda Hollywood kutafuta star mwingine.

Jamani, Mel Gibson alimwudhi au Boston haijamfaa? Nilivyokuwa kwenye set nilimwona Mel kama mtu poa, mcheshi na alikuwa anajichanganya na sisi extras bila wasiwasi. Mpaka wakati wa kula alikuwa anakuja kula na sisi. Lakini hao stelingini wengine hutawaona wanakula na crew na extras au actors wengine. Wanapelekewa chakula kwenye trela yao ya kifahari au wanapelekwa kula hotelini. Na wengine hata wakati wa kushuti wanakaa mbali na wengine. Wakati mwingine mnaambiwa msiwatizame! (haki ya mungu!) Hebu fikiria Mel Gibson alivyokuwa poa, anagongana na sisi na wala hajali.

Kwa sasa wasemaji wa DeNiro wanasema kuwa kajitoa kwa ajili ya 'creative differences' yaani hakubaliani na jinsi sinema invyoenda, au staili ya mwongoza sinema. Wengine wanasema kuwa ni 'code' kuwa anaenda rihabu (yaani sehemu wanapoenda walevi wa madawa ya kulevya navitu vingine kupumzika).

Hollywood bwana! Nitaendelea kuwapasha.

Kwa habari zaidi soma:

http://www.variety.com/article/VR1117991604.html?categoryid=13&cs=1


No comments: