Tuesday, April 07, 2009

Skandali ya Ngono kwenye Shule ya Oprah


Wasichana wanne wamefukuzwa kwenye shule ya fahari ya wasichana ya Oprah Winfrey huko Afrika Kusini. Wasichana watatu wamesimamishwa kwa muda. Kisa? Walikuwa wanafanya ushoga na kulazimisha wanafunzi wenzao kufanya vitendo vya kishoga!

Wasichana waliofukuzwa wamelia baada ya kunyanganywa simu za mikononi, nguo, viatu na vitu vingine walivyopewa shuleni.

Hiyo shule inaitwa Oprah Winfrey Leadership Academy. Wanafunzi wanasoma katika madarasa ya fahari kuliko hata vyuo vikuu vingi duniani, wanalala kwenye malazi yanayozidi five star hotel, na wanakula chakula kizuri kuliko unachoweza kununua kwenye restaurant. Hela aliyotumia Oprah kujenga hiyo shule ingetosha kujenga shule 10 nzuri sana Afrika Kusini.

Oprah mwenyewe anachagua wasichana wanaosoma pale na wengi wanatoka kwenye maisha ya dhiki.

Nawapa pole hao wasichana. Wameharibu wenyewe! Wenyewe wanaomba wasamehewa kwani bado wanakuwa na walitaka kufanya 'experimentation' (majaribio)!

Kwa habari zaidi someni:




6 comments:

Anonymous said...

Kwakweli huu usagaji na ushoga unaathiri sana teenagers. Wazazi tuna kazi kubwa mno.

Anonymous said...

Ufahari wote huo na watoto bado wanashikwa na ashki! Oprah amepoteza pesa kwenye hiyo shule. Anaelimisha wasichana wachache wakati anageweza kusomesha wengi zaidi kwa hela hiyo hiyo! Rich and stupid!

Anonymous said...

Huyo mzungu ndo kiongozi wao.

Anonymous said...

we unaesema oprah ni rich na stupid, Mungu akusaidie kwa kweli u dont know wat u saying.afrika wangapi wenye asili halisi ya kwetu afrika wamefanya hivyo? kwanza its a shame kwa afrika mtu toka marekani asomeshe watoto kwetu afrika wakat wapo matajiri sana lkn wanafadhili mambo yasiyo hata na maendeleo acheni mama tajiri afanye ambavyo moyo wake unamsukuma, waafrika wengi wamekalia awe tajiri ili aionekane na watu kama ufahari tu na kusaidia ndg zake tu. huyu aliejitolea Mungu amzidishie sana aendelee kufadili sehemu mbali mbali.

Anonymous said...

wanafrika kusini hawana shukurani. bora angejenga Bongo.

Anonymous said...

Duh tru kabisa Anonymous April 08, 9:42, tena ingekuwa vizuri ajenge Bukoba.