Wednesday, December 15, 2010

Nimerudi Boston

Mashine ya Fluoroscopy juzi kabla haijatengenezwa na fundi.

Mimi na baba jana nyumbani mara kabla ya mimi kuondoka kurudi Boston.


Wadau, nimerejea Boston kutoka Dar leo.

Baba alifanyiwa X-ray aliyohitaji baada ya mashine ile ya Fluoroscopy kupona. Alikuwa discharged juzi, lakini tulimrudisha Muhimbili jana kwa ajili ya hiyo X-ray. Yuko nyumbani Tenki Bovu sasa anaendelea vizuri. Hiyo X-ray tulilipa 80,000/- wiki tatu zilizopita lakini ndo alipata jana. Nilikuwa nimeanza mpango wa kumpeleka private kwa ajili ya hiyo x-ray lakini nilipigiwa simu kuwa mashine imepona na angeweza kufanyiwa. Ingawa ilifanya kazi jana huenda mashine hiyo imekwishaharibika tena. Niliambiwa ilishawahi kufa kwa miezi mitatu! Sasa wale wagonjwa wasio na uwezo wa kwenda private walifanya nini?
Wanaofanya kazi pale wako frustrated kwa vile wanshindwa kufanya kazi yao vizuri kutokana na mashine mbovu. Ilivyoharibika, wafanayakazi waliondoka kwa vile hawakuwa na kazi ya kufanya. Ilikuwa kila nikienda kucheki kama mashine imepona, hakuna mtu! Wana frustration ya hali ya juu.

Kwa kweli lazima niseme huduma Muhimbili ilikuwa nzuri kwa ujumla. Siyo Best lakini nzuri, tofauti na miaka ya nyuma. Baba alikuwa Semi private Ward huko Mwaisela.

Ila jamani tulikuwa tunafika pale Muhimbili kila siku saa 12 asubuhi, halafu unasikia vilio, mtu kaja kamkuta mgonjwa wake ameaga dunia usiku.
Picha tele za Muhimbili zinakuja. Safari hii sijaweza kwenda popote maana kila siku ilikuwa safari ya hospitali.

No comments: