Showing posts with label Tendo la Ndoa. Show all posts
Showing posts with label Tendo la Ndoa. Show all posts

Saturday, November 07, 2015

Kizee wa Miaka 72 Aolewa na Kijana wa Miaka 22


Wadau, kijana wa miaka 22 kutoka Dominican Republic, amemwoa bi kizee tajiri wa kiMarekani mwenye miaka 72.  Ni mapenzi au.... labda kizee anapenda ngono anayopata kutoka kwa huyo kijana, na huyo kijana anataka hela ya huyo bi kizee na pia atapata makaratasi ya kukaa Marekani.  Haya tuwatakie maisha mema ya ndoa.

Sunday, June 30, 2013

Kwa nini Wanaume Wanalala Baada ya Tendo la Ndoa?

Haya akina mama/dada. Nadhani wote tumekutana na hii tatizo la wanaume kulala wakimaliza shughuli yao katika tendo la ndoa!  Hebu soma hii habari.

************************************************************

Na Mdau Mtambuzi wa Jamii Forum




Jambo hili huwaacha wanawake wakiwa wamechanganyikiwa na kujiuliza maswali chungu mzima kama kuna mahali wamekosea au hawajawavutia wapenzi wao, pale wenzi wao wanapogeukia upande wa pili na kushikwa na usingizi punde tu baada ya kumaliza tendo la kujamiiana.

Lakini utafiti uliofanywa hivi na wanasayansi unawapa wanaume ahuweni katika kuepuka lawama hizo, kwamba, kumbe siyo hiyari yao, bali ni maumbile.

Wanasayansi hao wamebaini kwamba, kwa sababu za kimaumbile ubongo wa wanaume unawalazimisha kulala muda mfupi baada ya kushiriki tendo la kujamiiana. Katika utafiti wao wanasayansi hao walibaini kwamba, kwa jinsi ubongo wa mwanaume ulivyotengenezwa, pale wanapomaliza tendo la kujamiiana na kufika kileleni kuna eneo linalozimika na kuwafanya kupata usingizi.

Wakati hilo likitokea kwa wanawake hali ni tofauti, kwani wao hubaki wakikodolea macho dari wakiwa wamechanganyikiwa na kujiuliza maswali lukuki, wakijihisi kutowaridhisha wapenzi wao.



Utafiti huo ulifanyika kwa kuhusisha kipimo cha kumulika, maarufu kama scan, ambapo kilitumika kuwamulika wanaume katika ubongo wao pale wanapofanya tendo la kujamiiana na baada ya kumaliza kujamiiana na kufika kileleni na kubaini kwamba, eneo linalojulikana kama cerebral cortex, eneo linalohusika na ‘fikra’ huzimika baada ya mwanaume kufika kileleni.

"Utafiti huu unatupa matokeo ya kile kinachotokea ndani ya ubongo pale mwanaume anapofika kileleni.” Gazeti la Mirror lilimnukuu mwanasayansi mmoja wa serikali ya Ufaransa aitwae Serge Stoleru.

“Lakini kwa wanawake inaonekana ni tofauti kabisa……” Aliongeza kusema mwanasayansi huyo.

Mwanasayansi huyo aliendelea kusema kwamba, wanawake hushangazwa sana na jambo hilo na ndio sababu hubaki wakiwashangaa wapenzi wao wanapolala baada ya kumaliza tendo il hali wao wakitaka zaidi….

Kwa hiyo hakuna sababu ya wanawake kuwalaumu tena wanaume baada ya kumaliza tendo na kulala kwa sababu hivi sasa wameshajua sababu, watuwache tupumuwe…… 


 

Tuesday, July 10, 2012

Mbunge Frank ndiye wa Kwanza Kufunga Ndoa ya Kishoga!

Mbunge wa Massachusetts, Barney Frank amekuwa mbunge wa kwanza kufunga ndoa ya kishoga Marekani. Frank, mbunge wetu mpendwa wa miaka mingi hakuficha ushoga wake.  Aliwahi kuwa na skandali ya kutembea na malaya wa kiume na pia kutembea ma kijana wa kiume ambaye alikuwa intern Bungeni.
Mbunge wa Massachusetts Barney Frank (kulia) na mke wake Jim Ready

 
Congressman Barney Frank (D-MA) (72) married  longtime partner, Jim Ready (43) this past weekend . The couple got hitched Saturday at the Newton Marriott in a ceremony officiated by Governor Deval Patrick , and attended by Representatives Nancy Pelosi , Dennis Kucinich , and Steny Hoyer , and Senator John Kerry .

Kwa habari zaidi BOFYA HAPA:

Kwa picha zaidi ya arusi yao BOFYA HAPA:

Monday, October 03, 2011

Sinema 'Historia ya Khanga" Cheki Mimi na Kaka Michuzi!

MaStaa wa Bongowood 1991 Michuzi & Chemi


Kabla ya Kanumba na Ray kulikuwa na Chemi na Michuzi!

Wadau, kwenye mwaka 1992 nilishiriki katika sinema ya TAMWA, "The History of Khanga".  Hebu itizame, Utaniona mimi na Kaka Michuzi, "Tunajiandaa kulala"

Mwongozaji alikuwa Dada Fatma Alloo. Pia kuna mahojiano na marehemu Bibi Titi Mohamed.

Sinema sasa iko YOU TUBE kwa hisana ya Dada Fatma na Kaka Michuzi:

http://www.youtube.com/watch?v=jAuhAB0HeeA&feature=player_embedded

Friday, May 06, 2011

Bwana Arusi ana Miaka 100, Bibi Arusi Miaka 90!

Africa ukifika miaka 40, basi wewe mzee! Ukifikisha 70 basi unstahili kutotelewa nje na kuanikwa juani. Huna thamani tena. Mapenzi, ndo usahau kabisa, unabakia kukumbuka katika ndoto zako ujana wako!

Hapa Marekani, wazee Forrest Lunsway (100) na Bi Rose Pollard (90), wamefunga ndoa. Hebu cheki nyuso zao za furaha, mapenzi motomoto! Inasemekana wamevunja rekodi ya umri wa wafunga ndoa. Doh! Wamejuana karibu miaka 28. wote wanakaa kwenye nyumba ya wazee. Nawatakia maisha mema ya ndoa. Kumbe hata ukiwa na miaka bado wamo! Ila Zaeni matunda mema haifia kusemwa hapa.
***************************************************************************



(pichani wanaarusi Forrest (100) na Rose (93))


Kutoka YAHOO.COM

For some people, it's never too late for love.

That's certainly the case for Forrest Lunsway and Rose Pollard, an Orange County, Calif. couple who were married this March 19, Forrest's 100th birthday. With a combined age of 193--Rose is a spring chicken--they're believed to be the world's oldest newlyweds.

A spokesman for the Guinness Book of World Records said they had been informed of the wedding and are set to verify it as a record. For 27 years, Forrest smoked a pack of cigarettes a day, and he still drinks the odd glass of wine or whiskey and 7-Up, he said in a recent interview with the The Daily. He attributes his longevity to never having had a desk job: He spent his youth trapping animals and selling their fur in Kansas before moving to California, where he worked as a pipe welder.

You can watch a video of them here.

Both Forrest and Rose had been married before, but were single when they met back in 1983 at a senior's dance. Though they soon started dating, wedding bells seemed unlikely.

'I told him up front I had no intention of getting married," Rose said. "But then one day he asked me 'how come we never got married? and I said 'because you never asked me.'"

''So he got down on one knee and said, 'Well I'm asking you now, just set the date.' I told him, 'I'll marry you on your 100th birthday.' And I did."

And being on the older side, the couple also has some wisdom to share on how to make a marriage work. Rose, 93, told The Daily: 'Take your time and get to know one another. Get to know if you like all the things that person stands for. ... Be forgiving and patient and say I love you once in a while."

Rose also told The Daily that their advanced age means that she and Forrest don't have many of the anxieties that can be a challenge for other newlyweds. "That's one of the things we can forget about--time. Because time doesn't mean that much."

And it's time well spent together: They both love ballroom dancing, and they want to kayak in Alaska and walk the coast of California.

"We've got many happy years left as I intend to stick around until I'm at least 110," Forrest said. "You've got to use it or lose it."
(The Daily)

Tuesday, January 05, 2010

Mume Anapokimbia Mke Mjini Na Kuanza Maskani Mapya Kijijini!

SEMA DA FLORA WINGIA! SEMA!!!!!

************************************
Na Flora Wingia

Heri ya Mwaka Mpya 2010 mpenzi msomaji wangu. Tuna kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa kutuvusha mwaka huu. Naamini sote tumejipanga vema katika kufanikisha malengo mapya kwa mwaka mpya.

Wakati wengine wamepania kuboresha maisha ya familia zao, wengine wameamua kumeguka na kuanza maisha mapya kwingineko. Je, unajua ni kwanini? Hebu sikia kituko hiki cha kufunga mwaka 2009.

Ukiona mwanaume anaukimbia mji wake na kwenda kutafuta maskani mapya, ujue maji yamemfika shingoni. Katika hali ya kawaida ya maisha, mwanaume ndiye anayemkaribisha mwanamke nyumbani kwake na wakati mwingine huishia kumuoa.

Ukiona mwanamke anayemtunza mwanaume nyumbani kwake, huwa inaelezwa kuwa ‘mwanaume huyo kaolewa’. Lakini si unajua tena kupenda wakati mwingine mtu huwa zuzu au wengine huita zezeta. Hata akikemewa na wenzake yeye hujifanya hamnazo na kujikausha kwani anajua nini anachofaidi pale.

Pengine yeye ni kula kulala. Kila kitu anagharimia mke kuanzia chakula, mavazi na kadhalika. Mwanaume anayempata mwanamke wa aina hiyo, kwanini ajivunge?

Tukiachana na hayo, yupo mwanaume anayeoa mwanamke iwe ni kwa gharama kubwa au za kawaida, lakini baadaye mke huyo anamnyanyasa kiasi cha kumfanya auhame mji huo na kutamani mji mwingine. Hebu sikia kituko hiki cha funga mwaka.

Yuko baba mmoja nilikutanishwa naye hivi majuzi ambaye amelikimbia jiji la Dar es Salaam na kuhamia kijijini mkoa wa Pwani kutokana na manyanyaso anayopata toka kwa mkewe.

Baba huyu mwenye watoto wawili na mwanamama huyo, ameapa kumwachia mkewe kila kitu hapa jijini, na kisha yeye kuhamia kijijini kuanza maisha mapya mwaka huu mpya.

Baba huyu amenifurahisha sana. Wenzake wanahama vijijini kuja mijini lakini yeye anaamua kurejea maisha ya kijijini kutokana na suluba toka kwa mkewe.

Baba huyu anasema; “Heri kuishi peke yangu eneo la kijijini kuliko kuishi na mwanamke mwenye kero kama mke wangu. Nilimpenda mwenyewe, lakini sikujua kama angenifanyia yale niliyobainisha kwake.

“Mwanamke hataki kufanya kazi yoyote, yeye ni kwenda saluni, kukaa na kujipodoa tu. Nina mifugo, ng’ombe wawili wa maziwa, nguruwe na kuku wa kienyeji. Kutokana na mama huyo kutoonyesha nia ya kujishughulisha, nimeweka wafanyakazi wa kuhudumia mifugo hiyo.

“Akiamua hutoa nguruwe na kuuza na ninapomuuliza anakuja juu na kudai eti ni kwa matumizi ya nyumbani. Hata hivyo, kila siku lazima niache hela ya chakula mezani. Nikirudi nyumbani lazima aninuse eti kama nanukia marashi ya wanawake.

Wakati mwingine tunapopumzika hataki nimguse…hugeukia ukutani. Vituko hivi na vingine vinaninyima raha vibaya sana. Hadi najiuliza ni mwanamke gani huyu?Au anaye mwingine ampendaye?

“Nilimchangua mwenyewe, nikamuoa mwenyewe, lakini sasa nimefikia mwisho sina budi kumtosa. Sitamfukuza, lakini nitamwachia kila kitu, nyumba, mifugo na vitu vyote vilivyo mzunguka. Watoto nitapeleka shule za bweni. Ila mimi nakwenda kuanza maisha mapya”, anasema baba huyu.

Nilipomuuliza kama uamuzi huo amewajulisha wazee alisema; “Nilishaitisha kikao cha pande zote mbili kulalamika vituko vya mke huyu. Napo nilieleza msimamo wangu wa kutengana naye na kumwachia kila kitu. Ingawa hakukubaliana na hilo lakini niliungwa mkono na wajumbe wengi kwamba kwa kuwa hataki kujirekebisha, hakuna jinsi.

Mpenzi msomaji, kwa maelezo ya baba huyu, tayari ameshapata eneo katika kijiji kimoja mkoani Pwani ambako atajenga makao yake mapya na atajikita kwenye Kilimo Kwanza kwani anazo ekari 15 za ardhi. Hataki wala mwanamke wake huyu ajue huko kujiepusha na bughudha zake.
Ama kweli ‘mwenye bahati habahatishi. Mwanamke anapata mume mchakarikaji, lakini yeye anabweteka. Wapo wanaotafuta bahati ya aina hiyo bila mafanikio.

Nijuavyo mimi, mwanaume ni nguzo ya nyumba. Anapoondoka iwe ni kwa mfarakano au kwa kifo, hakika maisha katika nyumba husika huyumba na wakati mwingine hubomoka kabisa.
Mama yule anaonyesha jeuri ile kwa kuwa anamuona mumewe karibu, lakini atakapotokomea kijijini alikopania, mwanamama yule ambaye amekuwa mbwete, hataki kujishughulisha na miradi ya pale nyumbani, atajikuta naye pia akihangaika kama hayawani.

Ninachokiona kwa mwanamke huyu ni majuto mjukuu. Anachoshindwa kufahamu ni kwamba mwanaume wake huyo aliyepania kumponyoka ni hazina kwa maisha yake. Ni vema ajitambue kwamba pamoja na uvivu wake lakini bwana yule alimvumilia. Maandiko ya dini yameweka bayana kwamba ‘mwanamke mvivu na asile’.

Inapofikia hatua hata ile haki yake ya msingi ya ndoa anaikosa, je, baba huyu afanyeje? Ni mfanyabiashara anayekimbizana na kazi zake huku na huko ili aweze kutunza familia yake na pia kusomesha watoto, lakini mkewe hatambui hilo, anamchunguza chunguza eti leo ananukia marashi ya kike au kwanini umechelewa au kwanini umelala nje na kadhalika.

Ebo! Kama unamwekea vigingi kwanini asitafute starehe mahali pengine? Mambo mengine baadhi ya wanawake wanachangia. Mwanaume ni mvumilivu sana hasa inapohusu mambo ya familia yake.

Lakini ukiona mwanaume anasema ‘inatosha’ ujue amefikiria mbali. Amevuta pumzi hadi za mwisho. Kwa maoni yangu kuhusiana na mwanamama huyo ni kwamba kama kweli mumewe amepania kumwachia mji, na hakuwa makini, mali zote zinazomzunguka zitatoweka kama umande.

Inavyoonekana mume huyo amepania kutengana na mwanamama huyu kwa sababu hizo nilizotaja hapo juu huku akionyesha kuwa zipo sababu nyingine zilizojificha ambazo hakutaka kuzitaja hadharani. Ama kwa hakika Maisha Ndivyo Yalivyo.

Mpenzi msomaji wangu, hayo ndiyo yaliyojiri mwishoni mwa mwaka jana, baba huyu aliyepania kumkimbia mkewe na kuhamia kijijini kisa eti anamnyanyasa ikiwa ni pamoja na kumnyima haki yake ya unyumba.

Kama hayo ni kweli, basi mwanamama huyo amemkosea sana mumewe na anapaswa kujilaumu kwa uamuzi wowote atakaochukua. Kila mtu anapenda kuishi kwa raha bila bughudha. Maisha yenyewe ni mafupi sana hivyo hayahitaji masharti ya kisanii. Jipe raha na mpe pia raha mwenzako. Maisha Ndivyo Yalivyo.

fwingia@yahoo.com

Sunday, April 05, 2009

Mume Atalakiwa


Mume atalikiwa sababu ya "rungu" kubwa


Dar Es Salaam, Tanzania


Mwanamke mmoja amerudi kwa wazazi wake akilalamika kwamba "jogoo" la mumewe ni kubwa sana. Mwanamke huyo mkazi wa jijini aliwashangaza ndugu zake waliofika nyumbani kwake alipowatobolea kwamba hawezi kuvumilia "kugongwa" na "rungu" hiyo kubwa ya mumewe.

Awali gazeti la "Kasheshe" lilieleza kwamba, mume alilalamika kwa ndugu za mkewe akisema tangu wafunge ndoa miezi minane iliyopita, alifanikiwa kufanya nae tendo la ndoa siku moja pekee. "Mke wangu amenishangaza. Tangu tuoane miezi minane iliyopita alinipa unyumba siku tuliyofunga ndoa tu. tangu hapo amekataa kabisa kunipa haki yangu.


Kila nikimuomba anasema eti mimi si size yake", akalalamika mume. Mkewe alipoulizwa na ndugu zake sababu ya kumnyima mumewe chakula cha ndoa, aliwashangaza zaidi alipowaambia kwamba mumewe ana uume mkubwa sana ambao ameshindwa kuumudu.

"Aliniumiza sana siku ya kwanza na siwezi kuvumilia tena. Anipe talaka yangu nirudi kwetu", akasema mwanamke.Juhudi za ndugu hao za kumsihi dada yao ajaribu tena kufanya tendo la ndoa na mumewe wakimwambia atazoea maumbile yake, hazikufua dafu.

***********************************

Mmmh si aende kwa kungwi wamsaidie basi jinsi ya kuumudu! Huyo mume atampata mke mwingine hasa baada ya hii habari ya rungu kubwa kuenea! LOL!

Saturday, August 09, 2008

Tendo la Ndoa Uzeeni




Wadau, niliwahi kuposti mada hapa aliyoandika Kaka Lazarus Mbilinyi inatiwa 'Mawaidha Kuhusu Ndoa'

Sasa ameandikia kuhusu tendo la ndoa uzeeni.

Nadhani wengi tunadhani kuwa ukifikisha umri mkubwa ndo basi unaaga ngono/tendo la ndoa. Hiyo wazo inatia watu kiwewe. Kumbe wala, bado wamo! Asante sana kaka Mbilinyi kwa kuelimisha jamii kuhusu ngono tendo la ndoa. Natumaini watu hawatogopa kuzeeka sasa.

*******************************************************************
Na Lazarus Mbilinyi

Je, wazee wenye umri mkubwa bado huwa hamu kubwa ya tendo la ndoa? Utafiti wa sasa unaonesha kwamba jinsi mtu anavyozidi kuwa mzee uwezo wa kuonja, kunusa, kusikia na kuona hupungua. Pia uwezo wa kusisimuliwa kwa kuguswa hupungua pia.

Kiasili uwezo wa kusisimuliwa kimapenzi na uwezo wa kufanya tendo la ndoa pia hupungua (libido)Pia Utafiti unaonesha kwamba uwezo wa kufanya mapenzi huweza kupunguza kutokana na umri kuwa mkubwa ingawa pia umri kuwa mkubwa hauwezi kuzuia kabisa hamu ya tendo la ndoa (terminate).

Kuna ripoti kwamba wanaume na wanawake wenye umri wa miaka 50 hadi 80 bado wana hamu kubwa ya kufanya mapenzi (libido) na si kufanya tu bali kufurahia mno tendo lenyewe.

Kuna imani potofu nyingi kuhusiana na tendo la ndoa katika umri mkubwa zifuatazo ni baadhi tu ya hizo imani; Kushindwa kushiriki tendo la ndoa ni matokeo ya umri kuwa mkubwa.Tendo la ndoa ni hatari kwa wazee wenye umri mkubwa. Uwezo au hamu ya tendo la ndoa (libido) hupungua kwa kadri mtu anavyozeeka.

Yote hapo juu si sahihi kabisa. Hizo imani potofu zipo kwa muda mrefu na zimekuwa zikisababisha watu wenye umri mkubwa (wazee) kushindwa kufurahia tendo la ndoa au uumbaji wa Mungu.

Je, mabadiliko ya mwili kwa wanaume wazee huathiri vipi tendo la ndoa?

Kawaida wanaume wazee huhitaji muda mrefu ili kuweza kusisimka.

Kile kilichokuwa kinahitaji sekunde chache hadi dakika chache katika umri wa miaka 19 huhitaji zaidi ya dakika 15 katika umri mkubwa kwa mwanaume.

Wanaume wengi wenye umri mkubwa hupona ugonjwa wa Kukosa uwezo wa kufanya tendo la ndoa kwa kujifunza matokeo na athari za umri kwenda sana (Uzee) Katika umri ulioenda wanawake wazee wahahitaji kufahamu kwamba wanaume wazee huhitaji muda mwingi na wakutosha kuuandaa jogoo awike.

Mabadiliko mengine ambayo hutokea kwa mwanaume mzee sana ni kupotea kwa uwezo wa kufika kileleni tofauti na wakati akiwa kijana.

Hii ni kutokana na Kukosa hisia (sensation) za tendo la ndoa. Pia kiwango cha sperms anazotoa hupungua hivyo mwanamke mzee asiwe na mtazamo wa kudhani kuwa uwingi wa sperms ndio uzuri wa tendo la ndoa.

Mnaweza kumtembelea kwenye Blogu yake: http://www.mbilinyi.blogspot.com/