Saturday, February 18, 2017

Kinana Akutana na Waziri Mkuu Majaliwa Leo

KINANA AFANYA MAZUNGUMZO NA WAZIRI MKUU MAJALIWA,LEO LUMUMBA JIJINI DAR ES SALAAM
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimpokea Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa, alipowasili katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, leo, Februari 18, 2017, kwa ajili ya mazungumzo baina yao
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwa na Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa, alipowasili katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, leo, Februari 18, 2017, kwa ajili ya mazungumzo baina yao
Wakienda eneo la kufanyia mazungumzo
Wakiwasili eneo la mazungumzo Ofisini kwa Katibu Mkuu wa CCM.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (kulia) akizungumza na Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majaliwa, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, leo Feb 18, 2017. (Picha zote na Bashir Nkoromo)

Tuesday, February 07, 2017

Usiharibu Harusi Yako na Make -Up ya Ajabu!


Wasanii Wanaohusishwa na Madawa ya Kulevya Kisutu Court Leo!Ki


Rais Mstaafu George H.W. Bush ni Mzima!

Wadau, siku Rais Donald Trump anaapishwa tulidhani kuwa Rais Mstaafu George H. W. Bush, yuko mahututi atakufa dakika yoyote. Mke wa Barbara naye alikuwa hoi hospitalini. Ajabu juzi tuliwaona kwenye mchezo wa Super Bowl, wakitabasamu,kupungia watu na hata kufanya coin toss, kujua nani atarusha mpira kwanza. Wataishi maisha mrefu hao. Sasa watu wanafanya matani !😂😂😂
j

Monday, January 23, 2017

Mwanamke wa KiTanzania Apigwa Kwenye Treni na Mzungu Boston

Wadau, tumekuwa tukisema kuwa Rais Trump amefufua na kuhalilisha Ubaguzi Marekani
Kuna matukio mengi dhidi ya weusi na waspanish ambazo zimetokea.

Leo asubuhi, jumatatu 23/1/17, MTanzania, Stella Rupia, kasukumwa nje ya Treni na dume baguzi wa kizungu. Baada ya kusukumwa nje, alimwambia Stella," ita polisi basi!! " Mzungu baguzi kaendelea na safari yake.
Na kweli Stella kaita polisi na sasa Yule mzungu anatafutwa!! Ilitokea kwenye kituo cha MBTA Red Line, Cambridge, Massachusetts.
**********"*"*"**

The incident below happened to Stella Rupia today. God help  us.     This morning I got reintroduced to Trump's America.
I normally get off the Redline Central Sq station at around 6:30am then I catch the number one bus to go to work. So this morning around 6:35 as I was getting off the bus, this tall white guy leaned over and pushed me out of the train, when I turned to look at him before I could even open my mouth to say anything he yelled "Go on and call the police!" Just then the doors closed, the train moved. The few people who got off the train with me did not turn around as they were heading to the stairs, the people I don't think the people inside the train saw what he did, but it was sooo bizarre and shocking. Well, I made it to my bus and as I sat down in the bus that's when it dawned on me that He must be one of Trump's followers who has no balls to pick on someone his size SMH 😣

Saturday, January 14, 2017

WBZ News Radio Weekend Morning Crew

Kazini Leo!

Serikali Kuendeleza Mapambano ya Madawa ya Kulevya Nchini

 Waziri  wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba (katikati), akihutubia katika Maadhimisho ya Siku ya Familia ya Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni Dar es Salaam leo. Kutoka kushoto ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Kinondoni, Gift Msuya,Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ali Hapi, Kamanda wa Polisi Kinondoni, Suzan Kaganda na Meya wa Manispaa hiyo, Benjamini Sitta.
 Waziri  wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba, akimkabidhi zawadi Mkaguzi wa Polisi, David Mabula.
 Ofisa wa Polisi Hamad akikabidhiwa zawadi na Waziri Nchemba.
 Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani Sajeni, Moses Alphance Sinyagwa akipongezwa baada ya kukabidhiwa zawadi ya pikipiki kutokana na ufanyakazi bora.
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ali Hapi akitoa neno la shukurani katika maadhimisho hayo.
 Maofisa wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kinondoni wakiwa katika shindano ya kumkamata kuku kwenye maadhimisho hayo.
 Maofisa wa jeshi la polisi wakiwa kwenye maadhimisho hayo.
 Waziri Nchemba akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali.
 Waziri Nchemba akiwa katika picha ya pamoja na maofisa wa polisi waliotunukiwa vyeti.
 Hapa Waziri Nchemba akiwa katika picha ya pamoja na wadau 
kutoka akampuni yaliyodhamini maadhimisho hayo.
 Bendi ya Jeshi la Polisi ikitoa burudani.
Askari polisi, jamaa zao na waandishi wa habari  wakiwa kwenye hafla hiyo.

Na Dotto Mwaibale

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba amesema Serikali itaendelea kupambana wa waingizaji na wauzaji wa dawa za kulevya nchini.

Mwigulu alitoa kauli hiyo wakati akihutubia katika Maadhimisho ya Siku ya Familia ya Polisi Mkoa wa Kinondoni jijini Dar es Salaam leo ambapo alikuwa mgeni rasmi.

"Serikali imejipanga  kupambana na dawa za kulevya ambazo zimekuwa janga la kitaifa ambapo vijana wengi wanakuwa waanga wakubwa'' alisema Mwigulu.

Mwigulu alisema serikali ya awamu ya tano haitamfumbia macho mtu yeyote atakaye kwamisha jitihada za kupambana na uhalifu nchini ambao wamepanga kuupunguza kwa asilimia 10 ifikapo mwaka 2019.

Aliongeza kuwa kanuni na sheria zilizowekwa na mkoloni ambazo zinazotumika ndani ya jeshi la polisi zimekuwa na changamoto kubwa kwa askari polisi. 

Akitolea mifano kadhaa alisema askari polisi aliyekosa nyumba ya kuishi ya jeshi hilo anapaswa kupewa fedha za kulipia pango nje ya kambi ya polisi na suala hilo si la kumuonea huruma askari husika bali ni haki yake.

Alisema kwa upande wa askari polisi aliyeumia au kupoteza kiungo wakati wa mapambano dhidi yake na wahalifu askari huyo anapaswa kulipa fidia yake kwa wakati badala ya kuunda tume ya kuchunguza jinsi alivyoumia akiwa katika mapambvano hayo.

"Mambo mengine hayahitaji mpaka uwe na elimu kubwa askari amepambana na majambazi mbele ya watu lakini majambazi hayo yamemjeruhi fidia yake anashindwa kulipwa eti mpaka iundwe tume haya si mambo ya ajabu" alihoji Mwigulu.

Alisema kwa muda mrefu askari anapopangiwa kituo cha kazi amekuwa akijigharamia kwa nauli na fedha za kujikimu kwa zaidi ya miezi mitatu na zaidi bila ya sababu za msingi.

Alisema hali hiyo kama askari husika anakuwa si mzalendo anaweza kujiingiza katika tamaa na kutumia silaha aliyonayokufanya uhalifu hivyo akaomba wahusika kuliangalia jambo hilo kwa karibu kwani mshahara na posho kwa askari hao ni haki yao.

Mwigulu alisema serikali kupitia Rais Dk. John Magufuli imejipanga kuweka mazingira mazuri kwa askari polisi ikiwa ni pamoja na kujengewa nyumba na kuona namna ya kubadilisha sheria ambazo zinaonekana hazina tija kwa wakati huu katika kuliongoza jeshi hilo.

Saturday, January 07, 2017

Mchungaji Kulola wa EAGT Lumala Jijini Mwanza

Usikose kufuatilia maombezi na ibada ya neno la Mungu kutoka kwa Mchungaji Dkt.Daniel Moses Kulola wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya lililopo Sabasaba Jijini Mwanza, mubashara (live) kupitia ukurasa wake wa facebook.

Ni kila siku ya alhamisi kuanzia saa nane kamili mchana kupitia ukurasa wake wa facebook wa DANIEL KULOLA ambapo mahubiri na maombezi yatarushwa moja kwa moja (mubashara) kwa njia ya video.

Bodi ya Filamu Nchini Yawaomba WaTanzania Kuzipigania Kura Filamu za Kitanzania Kwenye Tuzo za AMV

BMGHabari
Bodi ya Filamu nchini imewahamasisha watanzania kuongera ari ya kuzipigia kura filamu za kitanzania zinazowania tuzo za Africa Magic Viewers Awards (AMVA 2017) za nchini Nigeria.

Katibu Mtendaji wa bodi hiyo, Bi Joyce Fissoo (pichani juu) ametoa hamasa hiyo hii leo, wakati akihojiwa kwenye kipindi cha Power Break Fast On Saturday kinachoendeshwa na watangazaji Philip Mwihava na Godfrey Kusolwa.

“Filamu hizo ni Naomba Niseme, Aisha na Home Coming ambazo zinawania tuzo za filamu bora na Siri ya Mtungi ambayo inagombea filamu bora ya lugha ya Kiswahili. Niwaase Wanzania, ushindi wa filamu hizi ni sisi kuwapigia kura hawa vijana wetu ambao wameshika bendera yetu kwenda kutuwakilisha kule Nigeria, niwasihi waweze kuzipigia kura na wahakikishe wanahamasisha marafiki zao pia kuzipigia kura ili nafasi zote tuzo zije Tanzania”. Amesisitiza Fissoo.
Naye Mtayarishaji wa filamu nchini, Staphord Kihole (pichani) ambaye pia alikuwa kwenye kipindi hicho, ametumia fursa hiyo kuwaomba watanzania kuzipigia kura filamu za kitanzania ili zishinde tuzo za Africa Magic Viewers Choice Awards ikiwemo filamu yake ya "Naomba Niseme" inayowania vipengele viwili, kikiwemo kipendele cha Best East Africa na Best All Africa kinachoamuliwa na majaji.

Ili kuzipigia kura filamu za Tanzania ambazo ni Naomba Niseme, Aisha na Home Coming, unapakua Application ya We Chat, unajisajiri kwenye Africa Magic kwa kutumia nambari ya simu na kisha unatafuta kipengele cha AMVCA na utaweza kupiga kura kadri upendavyo ambapo mtu mmoja anaweza kupiga kura hadi 100 kwenye filamu tofauti tofauti.
Bonyeza Hapa  Au play hapo chini kusikiliza sauti  Credit: Clouds Fm

Thursday, January 05, 2017

Aloanisha Kitanda katika Mapenzi

Kumbe staili zingine za ngono ni balaa!!!! 


Saturday, December 31, 2016

Heri ya Mwaka Mpya 2017!

Wadau, Mungu yu Mwema, tumefika 2017!

Nawatakia wadau wote Heri ya Mwaka Mpya! 


Saturday, December 24, 2016

Scrooge Albert Finney 1970 DVD - kwa Wenye roho Mbaya! Mtatubu!

Bing Crosby - It's Beginning to Look A Lot Like Christmas

Krismasi Njema!

Nawatakia wadau wote, Krismasi Njema! Mbarikiwe!

Merry Christmas!

Barua ya Kitapeli - Mtaibiwa Sana!

Nafahamu watu ambao wanadhani huo upupu ni kweli.  Eti utapata mamilioni ya madola ukitoa habari ya akaunti yako benki, au ukilipa dola $2000 ili upate mamilioni! Uchu wa pesa mbaya! Mtaibiwa sana!

********************************************

  • Dec 23 at 10:50 AM
Message body
HSBC BANK N.A.
140 Broadway
New York, NY 10005, USA

                                                          Payment Release Instruction from Federal Reserve Bank of New York

Acting on our capacity as the international correspondent bank to the International Monetary Fund Organization, this is to officially notify you that we have received a confirmation advice from the International Monetary Funds External Auditors Committee, World Bank, United Nations Organization and the Federal Reserve Bank of America respectively via International Payment Voucher Number: IMF/FRBWDC/BOA-93WB82UN567-G requesting our bank to direct the HSBC BANK USA N.A, a subsidiary of the Federal Reserve Bank of America to disburse your due wining/inheritance and contract payment valued at Ten Million Three Hundred Thousand United States Dollars (US10.3M) in your favor via their branch in New York.

In consideration of the above, you have been issued with this Exclusive Reference Identification Number (IMF/FRB-NY/9USXX10751/09), Vide Transaction No.: WHA/EUR/202 and Transfer Allocation No.: FRB/X44/701LN/NYC/US, Password: 339331, Pin Code: 78569, Certificate of Merit No: 104, Release Code No: 0876; Immediate HSBC Telex Confirmation No: -222568; Secret Code: XXTN014. Having received these vital payment numbers, you are instantly qualified to receive and confirm your payment within the next 72hrs. As necessary clearance has been granted from the International Monetary Funds External Auditors to release the funds to you with immediate effect.
In view of this directive received from the International Monetary Funds (IMF), we have on our own part verified your payment file as directed to us, and your name is next on the list of outstanding fund beneficiaries to receive their payment at this Third quarter of year 2016. With that being done, you are required to urgently contact the HSBC USA N.A. in New York through their International Funds Release Supervisor:

Contact Person: Sir Nelson Haggin.
(Head, Funds Release Supervisor)
Email: nelson.haggin116@gmail.com
Direct Office Line:  (+16465689796)

And reconfirm your international payment voucher number and your reference identification number respectively before that office with a view to the final remittance approval and subsequent crediting of your bank account to the tune of funds as stated herein.
We wish to inform you of the need for you to also re-confirm the following information before the HSBC BANK USA N.A. in New York to enable the officer in-charge to proceed with the preliminary arrangements that will enhance the immediate release of your funds. Owing to security reasons, be clearly informed that we will not respond to any phone calls/general inquiries placed to our bank with regards to the remittance of your funds by beneficiaries as we are barred from doing so, you are therefore advised to communicate only with the accredited officer for further remittance advice.

1) Full Name
2) Full Address;
3) Your contact telephone and fax number;
4) Your Age and Profession;
5) Copy of any valid form of your Identification;
6) Your Bank name;
7) Your Bank Address;
8) Account name and Number;
8) ABA/Routing Number;
10) Swift or Sort Code/IBAN

Thank you for your anticipated co-operation.
TREAT AS URGENT.

MIS. MARIE DUNCAN
DIRECTOR OF FUNDS CLEARANCE UNIT.
FEDERAL RESERVE BANK

Unyanyasaji wa Kijinsia: Mchango wa UMIss Tanzania Unaonekana?

Na Elias Muhongo

Tukiwa tunaangalia tangazo la biashara la ‘BIG BOSS’ nikashtukia mwanangu mmoja akilalamika: “Hapo si tunajinyanyasa kweli?”. Nikamuuliza ana maana gani? Akasema “ Baba angalia sana tangazo hilo. Huyu mama anamfahamu boyfriend wake lazima, ndiyo maana alikuwa hakupotea nyumba. Lakini kukutana na harufu ya manukato anayotumia boyfriend wake akaamua kuondoka na aliyejipaka (manukato hayo)? Ni unyanyasaji wa kijinsia na hapo tunajinyanyasa wenyewe”. Mjadala ulikuwa mkali lakini nikomee hapo na kuendeleza mawazo yangu kuhusu unyanyasaji wa kijinsia, hasa unyanyasaji wa wanawake.
Nimeangalia mijadala mingi kipindi hiki na kuilinganisha na kipindi fulani kilichopita. Wakati wa maandalizi ya mkutano wa Beijing 1990, nilishiriki sana maandalizi hayo hapa nchini. Nakumbuka akina mama kufikia hatua ya kuainisha aina mbali mbali za unyanyasaji unaowakabili wanawake. Kupigwa na waume zao. Kusafiri mbali kutafuta maji. Huduma duni za afya wakati wa uzazi na uzazi wa mpango, nakadhalika. Lakini pia walijiambia ukweli mwingine wasiojiambia siku hizi. Walijiambia jinsi inavyokuwa vigumu kukutana na mwanamke aliye madarakani. Jinsi ilivyo vigumu mwanamke kumpigia kura mwanamke mwenzake licha ya wingi wao.
Tulijadili na jinsi katika michezo kama dansi akina mama wanavuliwa nguo na kujianika huku wenzao (wanaume) wanacheza wamejivalia nguo.

Wagombea Miss Tanzania 2009

Ninaamini kuwa huenda baadhi ya manyanyaso yamepungua. Lakini ukichunguza sana utakuta yale wanayojinyanyasa yanaendelea na hayapigiwi kelele kama yale wanayonyanyaswa.
Tuangalie na huu unyanyasaji wa kijinsia kupitia ‘Miss Tanzania’. Nakumbuka katika historia ya Miss Tanzania tangu viruhusiwe baada ya utawala wa Mwalimu Nyerere, naweza kudhibitisha kuwa ni mwaka mmoja ambao Tanzania iliwahi kuwakilishwa na mtanzania halisi licha ya kupingwa na watanzania wengi. Ni mwaka Tanzania ilipowakilishwa na Mtanzania mwenye asili ya India. Huyo alionyesha asili yake na utanzania wake. Lafudhi yake ilikuwa ya mtanzania mwenye asili ya India. Myondoko yake ilikuwa ya Mtanzania mwenye asili ya India. Rangi ya ngozi yake iliwakilisha Mtanzania mwenye asili ya India. Nywele za kichwa chake ziliwakilisha mtanzania mwenye asili ya India.

Nani anitajie mwingine? Anitajie Mis Tanzania ambaye aliiwakilisha Tanzania nje ya Tanzania na waangalizi wakaiona Tanzania? Sitarajii. Maandalizi ya Miss Tanzania yanamuandaa mwakilishi wetu kuuondoa utanzania ndani mwake. Maandalizi huanzia Willayani. Yanapokamilika ngazi ya Taifa mshindi na washiriki wote wanakuwa wamekamuliwa utanzania ndipo (mshindi) anakabidhiwa bendera ya Tanzania kwenda kuwakilisha kitu kisichojulikana. Huwezi kuuona utanzania katika lafudhi yake. Huwezi kuuona utanzania katika myondoko yake (gait). Huwezi kuuona utanzania katika asili ya ngozi yake wala nywele zake. 

Lakini kila mashindano hayo na maandalizi yake yanapokuwepo hukosi kuhisi unyanyasaji wa wazi na wa siri. Mavazi wanayovaa ni unyanyasaji wa ajabu usioendana na Utanzania. Lakini wasikie waandaaji wakijitetea kuwa hakuna eushwa ya ngono zinazoendelea katika shughuli hiyo. Nani haoni kuwa hayo hayawezi kukosekana? Huu wote ni unyanyasaji wa kijinsia unaoendelea kwa hiyari ya wanyanyaswaji na wanaharakati usioweza kupigiwa kelele kwa sababu tu wafadhiri wa miradi ya uanaharakati ndio wadhamini wa unyanyasaji huo.

Kuna wakati niliwahi kufikiri badala ya mashindano ya Miss Tanzania kwa nini kusianzishwe mashindano ysa mapishi ya kitanzania. Inahitaji kuandaa vigezo vya kuamua namna ya kuamua kati ya chakula cha kihaya na kipare. Mpare atapika kande na mhaya ndizi zilizochanganywa magarage mabichi na nyama iliyokauka watu watakula na kuuona utanzania. Ikishindikana basi shindanisha wapishi mbali mbali wa chakula aina moja. Mapishi yetu hayawezi kuchakachuliwa kama ambavyo utamaduni wetu unachakachuliwa kupitia mashindano haya ya Miss Tanzania.

Elisa Muhingo

Thursday, December 22, 2016

Zanzibar ilitoa Msaada Kwa Uiingereza!!!!

Jamani tumezoea kuwa wapokea misaada. Lakini je, mlikuwa na habari kuwa wakati wa Vita Kuu ya pili vya dunia (World War 2) Zanzibar ilitoa msaada wa chakula Kwa waingereza wenye nja? Wakati Ile Zanzibar ni Sultanate.




Saturday, December 17, 2016

Zilipendwa - Pata Pata

Huu wimbo wa Pata Pata ilikuwa kiboko enzi zile. Uliimbwa na MSwazi, Miriam Makeba aka Mama Africa.



Namna na Kuepuka Matumizi Makubwa ya Fedha Kiindi cha Sikukuu


Na Jumia Travel Tanzania

Kwa kawaida kipindi cha sikukuu ni wakati ambao watu wengi huwa na matumizi makubwa ya fedha kwa ajili ya kusherehekea pamoja na wapendwa wao, famila, jamaa na marafiki.

Jumia Travel (www.travel.jumia.com) ingependa kukushauri kwamba ni vema ukawa na mpango madhubuti unaoeleweka wa namna gani pesa yako itakavyotumika ili pindi mwaka mpya utakapoingia uwe mwenye furaha na sio huzuni.

Tenga Bajeti Mapema

Kuna namna nyingi za kutenga bajeti kwa ajili ya matumizi yako kama vile manunuzi ya zawadi kwa watoto, wazazi, kutoa msaada pengine na mengineyo ndani ya nyumba. Endapo utapanga mapema itakusaidia sana kujua utahitajika kutumia kiasi gani kipindi hiki badala ya kukurupuka sikukuu zinapowadia.

Fuatilia Mwenendo wa Matumizi Yako

Kutenga bajeti pekee tu haitoshi bila ya kuwa na mbinu sahihi ya kufuatilia mwenendo mzima wa jinsi pesa inavyotumika. Tenga pembeni bajeti ya sikukuu kwa kufungua akaunti ya benki ili isiingiliane na ya matumizi ya kawaida. Unaweza kutumia mbinu mbalimbali kuhakikisha unafanikiwa katika hili, kwa mfano kuwa na programu ya simu, ambayo utakuwa unaweza kufuatilia kwa ukaribu mwenendo wa matumizi na kiasi cha pesa kilichobaki popote na muda wowote ulipo.

Punguza Matumizi Yasiyokuwa na Tija

Unaweza kuepuka au kupunguza matumizi ambayo si ya lazima ndani ya kipindi hiki ili kufidia gharama kwenye vitu vingine. Kwa mfano, kama ulikuwa na mazoea ya kwenda na familia yako kwenye hoteli ya kifahari kwa ajili ya mapumziko kila wikendi pengine gharama yake ni TSHS 100,000/- kwa wiki ambayo ni sawa na TSHS 400,000/- kwa mwezi, unaweza kuacha kwa mwezi huu ili kuitumia kwa mambo mengine.

Pendekeza Utaratibu wa Kununuliana Zawadi kwa Siri

Kwa bahati mbaya familia nyingi za kiafrika sio wenyeji wa utamaduni huu wa kununuliana zawadi kwa siri au ‘Secret Santa’ kama inavyojulikana kwa lugha ya Kiingereza.  Mbinu hii ina manufaa makubwa sana kama utataka kuepuka gharama kubwa za kumnunulia zawadi kila mwanafamilia, kwa mfano, pengine una baba, mama, kaka, dada, binamu, wajomba na mashangazi unaweza ukautambulisha utaratibu wa kila mtu kumnunulia zawadi mwenzio kwa siri na kumkabidhi siku ya sikukuu. Nadhani inaweza kuleta msisimko zaidi na kila mtu akafurahia.

Epuka Mila Zitakazo Kugharimu


Kuna baadhi ya makabila bado yana taratibu ambao huwalazimu wanakoo kukutana kwa pamoja ifikapo kila mwisho wa mwaka. Watu hulazimika kusafiri na kutumia gharama kubwa kwa karamu ambazo huandaliwa na kujikuta mwaka unaanza wakiwa hawana fedha za kutosha. Unaweza kuepuka hayo yote kwa kufanya vitu vya kawaida ambavyo familia yako itavifurahia na kuvipenda.

Kuwa Mwangalifu na Ofa za Mauzo

Inabidi kuwa makini sana na ofa zinazotolewa na wauzaji wa bidhaa mbalimbali ndani ya kipindi hiki cha sikukuu. Wafanyabiashara ni werevu sana kwani hutumia mbinu mbalimbali za kuuza bidhaa zao kwa kuweka mabango makubwa ya ‘Ofa Ofa!’ huku bei ikiwa ni ileile sawa na siku za kawaida. Kuepuka hili unapaswa kufanya tafiti mapema kwa kutembelea maduka au mitandao ili kujua kama ni kweli kuna unafuu kwenye hizo bei zinazotangazwa.

Jitahidi Kutokuzidisha Manunuzi Yako


Kutokana na ofa kemkem ndani ya kipindi hiki cha sikukuu wateja wengi hujikuta njia panda kwa kushindwa kujizuia kuzidisha manunuzi wanayoyafanya. Inashauriwa kuwa na orodha pamoja na bajeti ya vitu unavyotaka kwenda kuvinunua ili pindi umalizapo usizidishe kwa kutamani vingine. Kama ikiwezakana fanya manunuzi mapema kabla ya sikukuu yenyewe ambapo kutokana na punguzo kubwa la bei ukajikuta unataka kununua kila bidhaa.

Mwisho kabisa Jumia Travel (www.travel.jumia.com) 
inakukumbusha kufanya tathmini ya pesa na matumizi uliyoyafanya ili kujua kama ulikuwa ndani ya bajeti kama ulivyojipangia au la. Kwa kufanya hivyo, utakuwa na mkakati mzuri wa kuanza mwaka mpya bila ya msongo wa mawazo.