Tuesday, December 02, 2008

Vilio Uwanja wa Ndege Dar

Nami nilivyokuwa Bongo 2006 na 2007 niliona mbinu huko Airport. Yaani wafanyakazi wengine hawana haya kabisa! Ni kama mradi vile kufanya kazi pale.

********************************************************************
Kutoka Michuzi Blog:

Michuzi,

Pole kwa vacation na pia kwa kukosa ndege. Nipe nafasi kidogo niongelee wizi mdogo mdogo hatimae mkubwa katika Julius Nyerere International Airport maana inakera na inauma ile mbaya Ni kwamba kuna utaratibu kwenye viwanja vya ndege kuzuia abiria kubeba vichupa vyenye vimiminika zaidi ya ml100. Kwa hiyo inalazimu abiria kulazimisha kupima mzigo hata kama una 6kg ili mradi kusalimisha mafuta na vi-manukato kwa namna moja ama nyingine.

Kitu kilichojitokeza pale ni kwamba kampuni ya kupakia na kupakua mizigo ya Swiss port imeshindwa kudhibiti wafanyakazi wake na hivyo kupoteza hadhi ya kuchukua dhamana ya mizigo ya abiria. Nilichokiona mimi ni kwamba wale jamaa wanaobeba mizigo hufungua zipu na kukagua kilichomo ndani. Wakiona kitu cha thamani wanaweka mifukoni mwao.

Na kinachoumiza ni kwamba kama kuna vitu vilikuwa kwenye mifuko midogo ndani ya begi ambavyo labda ulitaka visigusane na vingine basi utavikuta tofauti, maana wanachana vimifuko ili kutafuta wanachokitafuta wao (WIZI MTUPU), ustaarabu hakuna hata kidogo.

Sasa nataka kuuliza kuna usalama gani kama mtuu amepima mzigo ili kufuata sheria za usalama wa usafiri wa anga na hatimae wajinga wachache wapitie vitu vya thamani kwenye mizigo yake? Na je, hii itatoa picha gani kwa abiria wapendao kutumia viwanja vyetu kusafiri kwa kuchukulia kuwa ni salama kwa kwa mali na mizigo yao.
MIMI NI MDAU NA NIKO AIRPORT.

Naomba kuuongezea machache.Ni kweli kabisa,ni kweli tupu kuhusu huo wizi hapa Uwanja wa DIA...

Kweli huwa mabegi yanafunguliwa tena wana utaalamu kuliko unavyodhani wanafungua zipu bila kuiharibu,na wanatoa vile wanavyovitaka wao kama Camera,Simu ,I-pod ,Laptop... na biashara kubwa ya kuviuza inafanyika huko NJIA PANDA sehemu ya kwenye Bar na Makazi ya watu....na huwa wanajisifu sana, na isitoshe ni kweli wana maisha mazuri sana LOADER AMA PORTER WA BONGO NI SAWA NA PORTER AMA LOADER WA ULAYA nikiwa namaana ya kwamba maisha yao yako juuu na ni matawi kuliko hata Maboss wao waliopo maofisini ,maana wao hupata Pesa kila aingiapo Shift.

Kulikuwa na utaratibu wa kuwapekua wakati wakitoka kazini,lakini sasa hakuna ila hata hivyo ni wajanja sana mara nyingine wanauza humu humu jengoni.na tunapata sana malalamiko mengi kutoka kwa wageni wetu watakao na kuingia nchini.Binafsi inaniuma sana maana ni juzi tu nilitumiwa na ndugu yangu mzigo wa Camera na wakailamba.
Na Juzi kuna wawili walijaribu kuiba mzigo wa mama mmoja Mmalawi waliushusha kwenye Air Malawi wakadai kuwa unaenda na Precision Air lakini Askari aliwashuku na kuwakamata sasa sijui kesi imeendaje.... WIZI WIZI WIZI KILA KONA......

Nini kwenye mabegi ya abiria, na wizi wa mafuta ya ndege je??? tena hiii ni issue sana kubwa maana hadi baadhi ya watu ambao hawastahili kuwepo wanashiriki kwenye hiii....jaribuni kufuatilia.

USHAURI WANGU kwa TAA na SWISSPORT wangetengeneza bango kubwa kuwasaidia wageni wanaondoka Departure liwekwe Getini pale nje kabla ya security liandikwe kwa kiingereza na kiswahili hata french kuwa ABIRIA ASIWEKE CAMERA, SIMU, LAPTOP AMA HELA MAANA NASIKIA KUNA WATU HUWA WANAWEKA HELA KWENYE MABEGI...PLEASEACHENI AIRPORT IMEKUWA MBAYA..

NA ABIRIA WA KUTOKA NJE WATAJUA HILI SUALA TARATIBU TUWASAIDIE HAWA WAONDOKAO....

2 comments:

Anonymous said...

kweli inasikitisha . na inatia aibu si kidogo bali beyond imagination.
Kuhusu kukosa USTAARABU mimi naomba kutofautiana na wewe with all due respect.nafikiri hawa wafanyakazi wamekosa UUNGWANA na siyo ustaarabu.IN MY OPINION NIKIWA KAMA MWAFRIKA I REFUSE TENA STRONGLY, ETI KIPIMO CHETU CHA UUNGWANA KUWA NI UARABU.NO.NAFIKIRI USTAARABU UNAWAFAA WENYEWE WAARABU HUKO USHENZINI KWAO .IN MY OPINION THOUGH WAARABU SI WAUNGWANA ANY WAY .MY OPINION TU.
samahani kwa upuuzi wangu kama nitakuwa nimekukwaza mchangiaji.

KUHUSU WIZI AIRPORT
Kwa maoni yangu suala la wizi hapa nyumbani naliunganisha na tabia na utamaduni wetu wa kupenda kupata mali,faida ,fedha au chochote bila jasho.please correct me if am wrong
watanzania wengi wetu tunaona fahari tena tunajigmba kweli kwa tunapopata misaada ya bure,hela za bure,chochote kile bila kutoa jasho .hiyo mentality is so deep rooted leo hii utasikia mtu anasifia WAARABU eti wana mihela wana mafuta na utajiri .ukimwuliza so what? anakwambia tutapata misaada mingi ya bure tukiji-associate nao even if it costs an individual his democratic.social, spritual and cultural freedom ukiachilia consequences zingina nyingi udiserable to that individual.huu ni mfano tuu.hata ziara tuu za viongozi wa mataifa makubwa ,kwa maoni yangu nimeona watanzania wengi huzihusiha ziara hizo ,na kupewa misaada ya bure.utamaduni wakupenda vya bure bila kutoa jasho hauko tuu kwetu sisi watanzania ordinary kwa viongozi wetu huko juu ndio usiseme .na hii inajidhihirisha ktk rumours na allegetions nyingi tunzozisikia za rushwa ktk serikali na taasisi mbalimbali.
MAISHA
Maisha ya mtanzania wa kawaida hivi sasa in my opinion HAYAELEZEKI.maisha yamekuwa zaidi ya magumu sijui niite nini na opportunities na legitimate avenues za commom man to make ends meet are virtually non existent.to him the most possible solution is taking a risk.risk gani ? KUIBA .Kuiba comes in many shapes and faces.Call it naything pleasing .The truth is Kuiba Ni Kuiba tu
RAHISI.
-PESA NI CHAPCHAP
-NA BADO NINA MSHAHARA(PEANUTS !)
-I GOT NOTHING TO LOOSE (AM A DEAD MEN ANYWAY)
-NI NANI ASIYEIBA ?
-VIONDOZI, WANASIASA- WEZI
-NI UTAMADUNI WETU ,NI FAHARI,NI UJANJA
mimi hapa si condone wizi isipokuwa ninaona kwamba tunahitaji kufanya overhaul ya mfumo mzima wa maisha na mindsets
Mutabaruka once aliimba -The system is a fraud.
jamani mimi am not justifying kabisa tabia hii chafu .don misunderstand me isipokuwa najaribu kuiangalia deep.
Sometimes nafikiria wale wazee wetu waliopata shida ya kutafuta uhuru wa mtu mweusi kama wengiliona kwamba jasho na damu waliyoimwaga matokeo yake ni mfumo wa descrimintaion ya wenyewe kwa wenyewe ,matabaka ya kutisha ,mfumo usiojali wananchi ,mfumo wenye kuua wapiga kura wake ,mifumo isiyoruhusu mtu wachini kujisustain (leave alone kuendelea) basi labda wengefikiria otherwise. Ni maoni yangu .
wizi airport haukubaliki under any circumstances and equally wizi unaofanywa na wanasiasa,serikali,viongozi wa taasisi za dini,ngo, wasomi nk haukubaliki pia

Raceznobar

Anonymous said...

Watu wanaomba chai/chochote hivi hivi! Ni kweli! Ni aibu sana.