Monday, May 24, 2010

Eti Venus Williams Alivaa Vibaya?



Wadau, huko kwenye French Open, bingwa wa mchezo wa Tennis, Venus Williams aliwatoa wazungu jasho. Wanalamika kuwa nguo yake, ilimfanya Venus aonekane kama yuko uchi. Mbona wazungu hawasemwi wakivaa vibaya kwenye michezo. Wengine wako uchi kabisa! Kwa mila na desturi ya tennis ni lazima uvae nguo nyeupe. Venus kavaa nyeusi.
***********************************************
BY MARK W. SMITHFREE PRESS WEB EDITOR

American tennis star Venus Williams is making some headlines this morning after donning a revealing outfit during her Sunday straight-set rout of Patty Schnyder at the French Open.
Williams, ranked No. 2 at the Paris tourney behind kid sister Serena, wore a black lace corset-inspired outfit with a flesh-toned undergarment that gave the appearance that the outfit was more revealing than it actually was.

Williams told the media that the outfit was all "about illusion,"
Kwa habari zaidi BOFYA HAPA:

13 comments:

Anonymous said...

nadhani hakuwatoa jasho wazungu tu,ni kila mtazamaji aliyekuwepo pale...mi nadhani da chemi umekaa sana kwenye nchi zenye ubaguzi, so u associate everything with balack and white...lol...
mi mwenyewe kufungua tu site yako nakutana na haya matako ya Venus,nkasema ooh nooo she didn't...this is not cute...
Poison.

Anonymous said...

Venus mtundu sana. Alijua hiyo suit itawatoa jasho!

Mashaka said...

Dada yetu kakomaa ona hiyo picha aliyoruka jasho linavyomtoka matakoni wallah

Anonymous said...

Aaa Chemi zungumza ukweli bwana....hujui figure ya mtu mweusi iko sexy zaidi kuliko ya mtu mweupe...wee unafikiri lingekuwa tako la mtu mweupe nani angestuka.....tena inaelekea kawafanyia kusudi

Kaka Trio said...

Kama hio bukta aliyovaa hapo chini ni sawa na hiyo aliyovaa hapo juu mie naona ni sawa tu. Kwani kwene bichi voliboli wanavaaga nguo za aje? si ni za uchi kabisa kuliko hata hiyo ya venus?

Watu wanazimia sana na matako ya kibongo ndio kwa shauri wanawashikia sana bango aho akina venus na mdogo wake manake yeye huyo serena ndio akivaa vivazi vyake basi akiinama kukachi brethi utaona kamera zinammulika matakoni, lakini wazungu hata wakimulikwa matakoni wao wenzangu wamepigwa pass saa zingine hata hunotisi kama kamera inawwangalia matakoni

Anonymous said...

Mila na desturi ni kuvaa nguo nyeupe. Yeye anavaa nguo nyeusi si mchokozi huyo!

Anonymous said...

Yuko uchi tu hapo hamna lolote.Ni picha ya pili ndo kinaonekana hicho cheupe lakini ya juu tuputupu.

Na wewe Chem acha kuongelea mambo ya ubaguzi hata palipo na ukweli.Mara nyingi nimekuona suala la ubaguzi umeliwekea kipa umbele hata pasipohusika.Mbona hata kwetu tunabaguana.Ukienda kuomba kazi mahali ambapo mkuu ni mchagga atakayepewa nafasi kwanza ni mchagaa mwenzake,Upo hapo???

Kaka Trio said...

Ukifuata mila na desturi basi hutacheza hio tenesi yenyewe kwani yaliyokuwa yanafanyika zamani hayafanyiki tena na sizani ni lazima uvae ngue nyeupe ndio ucheze kitenesi kama ingalikuwa hivyo ndivyo basi wachezaji wasingekuwa wanaruusiwa kuvaa nguo za rangi anuwai.

Sio kama Da Chemi anatunga mambo wengi wa watu wanawasema sana hao wadada, mara wana misuli kama ya wanaume, mara wanavaa vibaya, mara lololo, Serena ana matako makubwa ndio kwamaana Da Chemi anaona ni ubaguzi tu, na ubaguzi upo kweli wala si ulongo.

Anonymous said...

Angalia sana tabia hii ya kuona utupu kuliko mavazi..tujifunze kuona vilivyo sahihi kwanza..ni aibu na ajabu sana pale unapotazama UTUPU tu ilhali kuna mambo mengi sana ikiwa ni pamoja na urefu wake, picha ilivyo nzuri, jinsi alivyopiga mpira kimaridadi na mambo kadha wa kadha. Tujifunze kuona mambo chanya na tusitawaliwe na fikira hasi. Unakuta mwana dada kavaa gauni linafunika kifua chake,kiuna chake,makalio yake..utashangaa mdau anaibuka na kulaumu ufupi wa nguo..jamani hatujaona hayo mengine tualoliona ni mapaja yaliyo nje tu??

Anonymous said...

mashindano ya tennis yenye mila na desturi ya kuvaa nguo nyeupe ni yale ya "All England Club" au maarufu kama "Wimbledon".

Mashindano ya tennis mengineyo hayana desturi ya kuvaa nguo nyeupe.

Haka katoto kametaka tuu kuonyesha "nyeti" zake.

Anonymous said...

Mzungu aliyepiga hiyo picha kaona fahari kweli kupiga picha ya matako ya Venus. Anayatamani. Mzungu kwa kawaida kapigwa pasi.

Anonymous said...

Dada Chemi hakuna ubaguzi. hawa mabinti wacheza tenisi wanamatatizo ya vivwalo. Kuna mmoja walimnasa akipiga mpira wajuu na kichupi kikaenda pembeni. Ilikuwa aibu, lakini wapiga picha ndio zao siku hizi, hawaangalii mpira bali ukaaji vibaya!!Sensationalism.

Anonymous said...

Dada yaani wewe umekaa kibaguzi baguzi, kila mara kama kuna kitu kimesemwa kina muhusu mtu mweusi basi utasema "mbona wazungu" to me ni wewe ndiyo mbaguzi na siyo wao. Mwaka juzi walimsema Maria Sharapova, je yeye ni mweusi?

Mdau

Maryland