Monday, May 10, 2010

Lena Horne Afariki Dunia Akiwa na Miaka 92.

Lena Horne 1917-2010
(pichani Lena Horne akiwa na Bill Robinson aka. Bojangles na Cab Calloway mwaka 1943)

Wadau, leo tunamka kusikia habari ya kifo cha Lena Horne. Lena alifariki jana huko New York akiwa na miaka 92. Aliishi maisha marefu.

Lena alipambana sana na ubaguzi Hollywood. Alikuwa mweupe mno, na mara nyingi ilikuwa akiigiza katika sinema na wazungu ilibidi wampake make-up kusudi aonekane mweusi zaidi na wazungu wasidhani ni mzungu. Wakati huo sinema zilikuwa zinapigwa katika black & white.

Safari yake kwenda Hollywood ilianza mwaka 1933 alipokuwa katika stage show ya Cotton Club huko, New York. Lena aliigiza katika sinema, Cabin in the Sky. Katika hiyo ni kimada wa Little Joe. Walipiga scene ambayo Lena alikuwa anaoga katika bathtub huko akiimba akijiandaa kwenda kwa Little Joe. Scene ilikatwa eti kwa vile wazungu hawataamini kuwa weusi wanaoga!

Lena alikuwa mwimbaji maarufu pia. Aliimba katika klabu nyingi, na pia katika bendi za Noble Sissle, Duke Ellington na Cab Calloway. Alikuwa katika sinema The Wiz pia na Michael Jackson na Diana Ross.

Mwaka 2004 ilikuwa watengeneze sinema kuhusu maisha yake. Janet Jackson ndo alikuwa stelingi wake. Lakini baada ya Janet Jackson kuonyesha titi lake kwa umati akiwa kwenye Superbowl, Lena Horne alisema hataki "mtu mwenye fikra za kimalaya" aigize kama yeye. Alisha Keyes atakuwa stelingi wa hiyo sinema.

Rest in Peace Lena Horne.


5 comments:

Anonymous said...

Rest in Peace Ms. Horne!

Anonymous said...

Dr Remmy alisema kifo hakijali ubondia wako,uzuri wako,ugangwe wako.Kikikufikia hauna budi kufuata.Rest in Peace.

Anonymous said...

Rest in Peace Beautiful lady.

Anonymous said...

watoto wangapi kaacha, RIP

Anonymous said...

kwani alikuwa black?