Friday, December 12, 2008

Zilipendwa ziko kwa Da Subi

Zilipendwa za RTD hizi hapa...

Zimepatikana zile za enzi ile ya External Service of RTD, Kijaluba hoyeee, (na watangazaji mahiri Mikidadi Mahamoud, Uncle J Nyaisanga...) na matangazo ya Vicks Kingo na sijui Meza Action mara ukiumwa na misuli tumia Salimia Liniment... tangazo la Revola (Vipi Mama Mariam! mbona unalalamika hivi? Ah, nguo hizi, kila ninapokazana kuzifua, hazitakati sijui nitumie nini?)...., zile hadithi za Bi Deborah Mwenda za Ua Jekundu, Binti Chura, Mbalamwezi Nyota Begani nk..... kiasi zipo: http://nukta77.com/burudani.aspx ama http://nukta77.blogspot.com/ (mwisho wa ukurasa).....Wikiendi njema! -Subi

Asante sana Da Subi!

8 comments:

Subi Nukta said...

Shukrani nawe Da Chemi kwa kuwafahamisha na wengine!

Anonymous said...

Mimi huwa nikitembelea blog ya huyo Subi huwa siingii, ameweka vikwazo. Sio rahisi kuona blog yake kama ilivyo kwa Chemi.

Anonymous said...

blo yake haileweki inahusu mambo gani, zilipendwa, soka, phd scholarships, picha..i got confused! not easy to navigate also. just check it yourself.

Subi Nukta said...

Anon December 13, 2008 6:29 AM,
Pole kwa usumbufu unauopata lakini SI KWELI kuwa blogu imewekwa vikwazo, huenda tu ni muda wa kufunguka unakuwa mrefu na huwezi kuvuta subira lakini haina vikwazo.

Anon December 13, 2008 8:38 AM
Blogu nilipoanza nilikuwa naweka habari za nafasi za masomo, lakini kuanzia mwezi Novemba 2008 nilibadili na kuanza kuandika kila nililopenda hasa baada ya kuwa nataka mwenyewe kupata urahisi wa kurejea kusikiliza redio za KiSawhili ama kutizama TV nk. Yaliyobaki ni ziada ya kutaka kujifunza ama porojo za hapa na pale.

Subi Nukta said...

You are very welcome Maggie. I am glad that you enjoyed the clips.

Anonymous said...

subi sijui nikupe nini! kwa kweli umenikuna na nimefurahi sana kwa mara ya kwanza kuweza kusikiliza music ina real sense of art(hasa zile za tabora jazz,kilwa jazz,moro jazz) na ofcourse nyimbo zingine za kigeni hasa za kikongo na south afrika .kwa kweli aliyesema old is gold hakukosea ,zimenikumbusha nyumbani back in the days pale forodhani secondary,mambo ya rungwe oceanic,bahari beach,msasani beach club.na mambo ya Mnuso au kifanngshen (miaka hiyo)
Pia ule mziki wa makwizi Athumani(kitanzania) umenikumbusha sana kinyakyusa na anti yangu Tabia Mwanjelwa Ahsante sana Subi.kazi nzuri
RacezNoBar
E-Town
Canada

Subi Nukta said...

RacezNoBar,
Umeshanipa shukrani ya kutosha, roho yangu nyorrrrrroro kwa ulivyoandika jinsi zilivyokukumbusha mbali nyimbo zile.
Daima pamoja waTz!

Anonymous said...

I'm just being curious. Subi, are you married?