![]()  | 
| Opening of the National Defence College in Dar es Salaam in 2012 | 
Rais Kikwete Akusudia Kushika Chaki Tena
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete
 amesema kuwa anakusudia kurejea darasani kushika tena chaki kwa kuwa 
mhadhiri kwenye Chuo cha Taifa cha Ulinzi – National Defence College 
(NDC) cha Dar Es Salaam.
Rais
 Kikwete amelieleza hilo mchana wa leo, Ijumaa, Juni 20, 2014, wakati 
alipotoa Mhadhara (Lecture) kuhusu Usalama wa Taifa (The Security of the
 Nation) mbele ya wanafunzi wa Chuo hicho kilichoko Kunduchi, Dar Es 
salaam.
Rais
 Kikwete amewaambia wanafunzi wa kozi ya pili ya Chuo hicho kutoka 
nchini na nchi za jirani za Uganda, Kenya na Rwanda: “Najisikia mwenye 
raha sana kuweza kurudi darasani kutoa mhadhara huu. Tukio hili 
linanikumbusha enzi zangu katika Chuo cha Kijeshi cha Monduli (TMA). Ni 
matarajio yangu pia kuwa nitaweza kurudi kuwa mhadhiri katika Chuo hiki 
baada ya kukamilisha kazi yangu ya sasa.”
Rais
 Kikwete ambaye alizungumza kwa kiasi cha saa mbili, alianza mhadhara 
wake baada ya kupata maelezo kuhusu maendeleo ya Chuo hicho na baadaye 
akajibu maswali ya wanafunzi ambao walimwuuliza kuhusu mambo mbali mbali
 yanayohusiana na usalama wa nchi.
NDC
 kilianzishwa rasmi Septemba 2, mwaka 2012 na Chuo hicho kilizinduliwa 
Rais na Rais Kikwete Septemba 10, mwaka huo huo, 2012 wakati 
alipotembelea Chuo hicho kwa mara ya kwanza kufuatia juhudi kubwa za 
uongozi wake kuhakikisha kuwa chuo cha namna hiyo na cha aina yake 
kinaanzishwa nchini. Rais pia alifungua kozi ya kwanza ya Chuo hicho.
Kundi
 la wanafunzi wa kwanza kwenye Chuo hicho lilimaliza mafunzo yake Julai 
23, mwaka 2013 na sasa chuo hicho kinaendesha kozi ya pili yenye 
wanafunzi 30. Chuo hicho tayari kimepata usajili kamili wa NECTA ambako 
kina uwezo wa kutoa shahada ya uzamili katika masomo ya Strategic 
Studies.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
IKULU
DAR ES SALAAM
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
IKULU
DAR ES SALAAM
20 Juni, 2014




No comments:
Post a Comment