Monday, June 02, 2014

Ubaguzi Marekani!

Mzungu Mbaguzi akilaani weusi kwa kutokupata msaada wa Serikali
Wadau, hapa Marekani watu weusi wana pambana na ubaguzi kila siku.  Hebu ona, huyo mzungu kaenda kuomba Welfare (Yaani hela ya kujikumu kutoka Serikali), kanyimwa halafu ana laani weusi. Huenda walimwona ni mtu mzima ambaye anaweza kufanya kazi ndo maana walimnyima! Au waligundua kaficha hela mahala.  Yaani hapa USA mzungu mchafu kama huyo akienda, akioga na kuvaa vizuri, halafu aende interview atapata kazi kulikwa wewe mweusi uliyesoma na una sifa zote za hiyo kazi!  Halau ana pochi ya bei mbaya! Khaa si aeuze hiyo pochi apate hela ya chakula!

Halafu wengine ni matapeli tu! Hawataki kufanya kazi, kazi kukaa barabarani na kuomba hela! Na hasa wazungu wanapata hela nyingi kwa kuomba! Tena hizo pesa wanazopata haitozwi kodi kama za mtu ambaye anafanya kazi.

1 comment:

Anonymous said...

Chemi, watu weusi wataheshimika Marekani pale tu watakapoanza kuwa influential nje ya michezo na sanaa. Barack Obama ameonyesha njia. Nimeshatembelea Marekani mara moja kwa hiyo may be I'm being ignorant or naive, lakini kwa kweli Wamarekani weusi sasa wanapaswa kuanza kushika nafasi nyeti katika makampuni na taasisi zinazoendesha uchumi wa nchji hiyo. Huwa najiuliza: hivi kuna Mmarekani mweusi hata mmoja katika ngazi za juu za uongozi katika Apple au Microsoft au Google au Facebook au Wall Street? Hii ni mifano michache tu. Mpaka hapo Wamarekani weusi watakapoanza kuchomoza nje ya sanaa na michezo wataendelea kudharaulika na kubaki katika kivuli cha Wazungu.