Tuesday, November 10, 2009

Bandari ya Manda

Ukitoka bandarini kuelekea kijijini unakutana na huo mbuyu mkubwa. Niliuliza vijana wenye mgahawa hapo historia ya huo mbuyu, wakasema ni mbuyu tu. Nahisi ina miaka kama mia 500 au zaidi. Lazima imeona mengi. Ingeweza kusema! Manda, ilikuwa makao makuu ya Nyasaland enzi za Mjerumani. Walipaita, Wiedhaven au Wiedhafen.


Hiyo ni gofu la bandari ya zamani.
Meli ndo inapiga nanga hapo usiku sana kwenye giza. Manda hakuna umeme. Tulifika saa nane ya usiku, lakini kulikuwa na mba la mwezi safi sana. Ziwa Nyasa ni kubwa kama bahari.

No comments: