Saturday, May 31, 2008

Usivute Sigara Leo!




Leo ni siku ya kutotumia bidhaa za tumbaku kama sigara, cigar, pipe nk. Nichi nyingi wanakuwa na warsha za kuelimisha watu juu ya madhara ya kuvuta sigara na kutumia tumbaku.

Theme ya mwaka huu ni "Vijana kutokuvuta Sigara"

Sigara zinaua! Acheni kuvuta. Na tunajua wanaovuta sigara wananuka. Wanakuwa na harufu ya sigara kwenye nywele na nguo zao na pia midomo yao inanuka! Kwa nini mvuta sigara anakubali kuunguza mapafu yake huko mtengeneza sigara anatajirika. Mvuta sigara ana kohoahoa na anakuwa na makohozi meusi! Na ile kansa ya pafu ya sigara inaua haraka. Hapa Marekani wanasema kama kuna kitu ambayo ina uhakika wa kukua ni kuvuta sigara.
ACHENI KUVUTA SIGARA!

Kwa habari zaidi someni:

http://www.who.int/tobacco/wntd/2008/en/

http://www.dailytimes.com.pk/default.asp?page=2008%5C05%5C31%5Cstory_31-5-2008_pg13_7

8 comments:

Anonymous said...

Kweli kabisa! Kuna Minjemba inavuta sigara inajiona wa maana. Likifungua domo linanuukaaa!

Anonymous said...

Lakini tunajichanganya tunapowaambia watu wavute sigara huku tukihimiza wakulima walime tumbaku, na hapo hapo tunahimiza viwanda vya sigara viongeze uzalishaji ili uchumi ukue!

Anonymous said...

tatizo huko kwenu ulipo toka ndio wakataze kulima tumbaku alafu uone kama sigara itatengezwa

$ POLICE $ said...

THE ONLY WAY TO STOP USE OF SIGARA,IS TO MAKE IT ILLEGAL TO CONSUMER,JUST LIKE MARIJUANA.THIS IS THE ONLY WAY PEOPLE WILL STOP COMMITING SUICIDE KNOWINLGLY.

$ POLICE $ said...

please stop smoking.its suicide in other words.

$ POLICE $ said...

please stop smoking.its suicide.

Anonymous said...

please stop kuvuta sigara.

Anonymous said...

30 cigarettes @day and 1gram wead @2day. Which one is worse?
Help me sis...