Saturday, July 26, 2008

Tupinge Mauji ya maAlbino

Harambee tukusanye signature 100,000 za majina na ujumbe mfupi kwa ajili ya kuziwakilisha kwa vyombo husika kusaidia kampeni ya kupinga na kuachisha kabisa mauaji ya Albino.

Kila kukicha hii habari imekuwa ikiongelewa na kutunyima raha tulioko nje kwani tunashindwa kujibu tuhuma na kejeli hizi ambazo zinatupaka matope.

Kwa kutumia blog hii ya jamii shime wananchi andika jina na maoni mafupi hata kama ni sentesi mbili tupate signature 100,000 tuwakilishe kwa Waziri wa Mambo ya Ndani.

Kwa wanachama wa FaceBook group hii ipo na inakwenda vizuri pia ukiingia kwenye facebook (http://www.facebook.com/) serch kwenye albino utaipata.

Ref: Angalia hii Video ya Al Jazeera
http://youtube.com/watch?v=qKDwIiPw94I
Na hii ya The New York Times
http://youtube.com/watch?v=2iHu4NGDVno

Sikiliza ya BBC Hapa

********************************************************
Wadau, hivi kwa nini watu wanahofia maalbino mpaka wanadiriki kuwaua. Hata wazungu wanakuwa na maalbino lakini hawauliwi. Albino ni bindamu sema kakosa ile 'pigamentation' (rangi) kwenye ngozi yake. Lazima tupinge kuuliwa kwa malbino! Na hao wengi imani potofu waelimishwe!
Hebu someni jinsi maisha ya Mwandishi wa Habari, Vicky Ntetema, ilivyohatarishwa shauri ya kuwaumbua hao wanoaua malbino:
Maisha ya Mtangazaji Vicky NtetemaYapo Hatarini.. Baada ya kuwaumbua Wagaga(Wachawi) wanaotumia au Kuagiza wateja wao kuleta Viungo vya Maalbino nchini Tanzania kwa Tiba au Kupata Utajiri..Mtangazaji wa shirika la habari la uingereza BBC Vicky Ntetema amesema amekua akipokea vitisho kila kukicha juu ya maisha yake...Soma habari hapo chini upate ukweli wa mambo kutoka kwake..am living in hiding after I received threats because of my undercover work exposing the threat from witchdoctors to albinos living in Tanzania.I do not regret it, even if I am very scared.More Click Here.

1 comment:

Anonymous said...

Jirani yangu hapa Dar ana watoto wawili albino. Mbona ni watoto tu kama wengine. Nashindwa kuelewa hii tabia ya kutaka kuwaua.