Thursday, March 12, 2009

Aliyempiga Mwinyi Afungua Mdomo

Wadau, navyoona wasingempa nafasi huyo kijana aongee. Watatokea wengine wenye agenda zao na kufanya fujo. Mshenzi huyo anastahili kipigo cha nguvu! Nchi yetu Tanzania, ni nchi ya amani. Pia tunajivunia kuwa waKristo na waIslamu wanapatana na hakuna bugudha, Wenzetu barani Afrika wanatuonea wivu! Nina hisi huyo kijana katumwa na watu fulani!

****************************************************
Kutoka ippmedia.com

Aliyempiga Mwinyi afungua domo

2009-03-12
Na Waandishi Wetu

Wakati taasisi mbalimbali za kidini, wananchi wa kawaida na Kamati ya Bunge zikilaani kitendo cha Rais Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi, kupigwa kofi shavuni, muumini aliyefanya kitendo hicho, Ibrahim Said, ameeleza kuwa alifanya hivyo kupinga matumizi ya kondomu kwa waumini wa dini ya Kiislamu kwa madai kwamba, yanachochea vitendo vya zinaa.

Pia alisema alifanya kitendo hicho kupinga kuwapo kwa umoja kati ya Waislamu na Wakristo wakati wa kusherehekea sikukuu zao (Maulid, Idd, Krismas na Pasaka), uliozungumzwa na Mwinyi katika hotuba zake alizozitoa wakati wa mkesha Jumatatu usiku na kwenye Baraza la Maulid, jijini Dar es Salaam juzi.

Alisema hakuwa na nia ya kumdhuru Mwinyi na wala hamchukii, bali alikuwa na lengo la kufanya kituko chochote ili ujumbe wake uwafikie watu wengi.

Alitoa maelezo hayo alipohojiwa na polisi saa chache baada ya kufanya kitendo hicho wakati Mwinyi alipokuwa akihutubia Baraza la Maulid, katika Ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam juzi jioni.

Kutokana na kitendo hicho, Jeshi la Polisi, jana lilimpeleka kijana huyo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi wa akili na damu ili kubaini kama ana matatizo ya akili au la, kabla ya kufikishwa mahakamani.

Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa kijana huyo, ambaye anajulikana pia kwa jina la `Sultani`, alifanya tukio hilo juzi wakati Mwinyi akihutubia Baraza la Maulid katika ukumbi huo na alikuwa amekaa mstari wa tatu kutoka mbele.

Hata hivyo, alisema licha ya kumpeleka Muhimbili, wanatarajia kumfikisha mahakamani leo baada ya jalada la kesi yake kukamilika.

Alisema baada ya kufanya tukio hilo, kijana huyo alifikishwa kituo cha Polisi cha Salander Bridge na baadaye alihamishiwa kituo cha Polisi Kati kwa mahojiano.

``Nilimhoji kijana huyu ambapo katika maelezo yake alisema kuwa, yeye hakuwa na nia ya kumdhuru Mwinyi na hamchukii bali alikuwa na lengo la kufanya kituko chochote kile ili ujumbe wake uwafikie watu wengi. Alidai hakubaliani na hotuba za viongozi wa Kiislamu zinazosisitiza Waislamu na Wakristo kushirikiana kama vile kusherehekea kwa pamoja sikukuu za Maulid, Idd, Pasaka na Krismas,`` Kova alisema akimkariri kijana huyo.

Kova alisema kijana huyo aliendelea kumweleza kuwa, kwa maoni yake sikukuu za Kiislamu wanasherehekea wenyewe na Wakristo hivyo hivyo na sio kwa pamoja.

Kuhusu kondomu, Kova alimkariri kijana huyo akieleza kwamba, anapinga matumizi ya mpira huo kwa madai kwamba kuhimiza matumizi yake ni kuhalalisha uzinifu kwa Waislamu.

Hata hivyo, Kamanda Kova alisema katika mahojiano naye alimuuliza kwa nini aliamua kutumia njia hiyo kufikisha ujumbe wake, na yeye alieleza kuwa ujumbe wake usingefika kwa sababu ni mtu mdogo mwenye hadhi ya chini hivyo ungechelewa.

Akisimulia zaidi tukio hilo, Kamanda Kova alisema siku ya tukio kijana huyo alinyanyuka kwenye eneo alilokuwa amekaa muda mfupi baada ya waandishi wawili wa televisheni kurekebisha vipaza sauti vyao mbele ya Mwinyi, naye akijifanya anafanya hivyo (kurekebsiha kipaza sauti), lakini akaishia kumpiga kofi kiongozi huyo mstaafu.

``Mtu huyu baada ya kufika pale mbele alijifanya anarekebisha vipaza sauti kama walivyofanya waandishi, na alisogea karibu zaidi na Sheikh Mkuu na kujifanya anaongea naye ndipo aliponyanyua mkono wake wa kulia na kupiga kipaza sauti alichokuwa akikitumia Mwinyi na kiganja cha mkono sehemu ya nyuma ulimpata kwenye shavu la kulia,`` alisema.

Alisema kufuatia tukio hilo, uchunguzi unaendelea kufanyika ili kujua kama alitumwa na mtu au kikundi fulani au ni mwanaharakati.

Kutokana na tukio hilo, Kamanda Kova alisema wataangalia uwezekano wa waandishi wa habari pindi wanapohudhuria kazi za viongozi kuwa na kadi maalum za kuwatambulisha ili mtu yeyote asije akaonekana kama mwandishi.

Kamati ya Bunge ya Ulinzi, Bakwata walaani
Wakati kijana huyo akijieleza, Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Jumuiya inayoratibu safari za Hijja na Umra ya Taibah pamoja na Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata), zimelaani vikali kitendo cha Mwinyi kushambuliwa na kijana huyo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Wilson Masilingi alisema analaani vikali kitendo hicho kwa vile kimelitia taifa aibu.

``Nalaani vikali, kwani ni aibu. Ninawaomba wananchi watoe ushirikiano ili kitendo kama hicho kisijirudie katika siku za usoni,`` alisema Masilingi, ambaye pia ni Mbunge wa Muleba Kusini (CCM).

Hata hivyo, alisema hajui mazingira ya tukio hilo na kwamba, waliokuwapo katika eneo la tukio wana nafasi nzuri ya kueleza kama kuna uzembe wowote uliofanywa na vyombo vya ulinzi na usalama, na kutoa mwanya kwa mtuhumiwa kumshambuliwa Mwinyi.

Kutokana na hali hiyo, alishauri marais wote wastaafu waongezewe ulinzi kwa kuwa jambo hilo ni haki yao na ili kuepusha madhara makubwa yanayoweza kuwasibu baadaye kutokana na kufanyiwa vitendo vya kihuni kama hicho.

``Marais wastaafu wanastahili kuongezewa ulinzi. Ni haki yao. Kwani anaweza kutokea mwendawazimu katika dunia ya sasa, akaleta fedheha,`` alisema Masilingi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Taibah, Sheikh Ali Mubarak, alisema kitendo cha kushambuliwa kwa Mwinyi ni cha kulaaniwa na Watanzania wote wanaopenda amani na kuvumiliana katika masuala ya kila aina kwa vile kitendo hicho ni cha kinyama.

Sheikh Mubarak alisema mbali ya kuwa ni cha kinyama, kitendo hicho ni kinyume cha utamaduni wa Watanzania, hivyo kinapaswa kulaaniwa na kudhibitiwa ili kisitokee tena.

``Uongozi wote wa Taibah umepokea kwa masikitiko makubwa tukio la kushambuliwa kwa Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi wakati akihutubia maelfu ya waumini wa Kiislamu jana (juzi) ukumbi wa Diamond Jubilee. Kitendo hicho kwa vyovyote vile ni cha kulaaniwa na jumla ya Watanzania wanaopenda amani na kuvumiliana katika masuala ya kila aina,`` alisema Sheikh Mubarak.

Kutokana na hali hiyo, aliishauri serikali kuchukua hatua dhidi ya kitendo hicho ili kupata undani wa tukio lenyewe.

Alisema Taibah inampa pole Mwinyi, serikali na uongozi wake kwa vile inaamini kuwa kiongozi huyo ni mzee mwenye busara na anayetegemewa.

Naye Kaimu Mufti wa Tanzania, Sheikh Suleiman Gorogosi, alisema jana kuwa Bakwata inalaani vikali kitendo cha kushambuliwa Mwinyi kwa vile kitendo hicho ni cha kihuni na ni kinyume cha mafundisho ya dini ya Kiislamu.

Hata hivyo, Gorogosi ambaye pia ni Sheikh wa Bakwata Mkoa wa Lindi, alisema bado wana wasiwasi huenda mtuhumiwa aliyefanya kitendo hicho, ana matatizo ya akili, ingawa alisema kuwa uongozi wa Bakwata haumjui.

Kanisa lapigwa na butwaa
Nao viongozi wa dini nchini, wamesema kitendo cha Rais Mstaafu Mwinyi kupigwa kibao jukwaani, kimeidhalilisha Tanzania na kuwafedhehesha wananchi wote.

Aidha, wamesema kutokana na kitendo hicho hivi sasa ipo haja kupima na kutathimini kiwango cha amani na utulivu nchini.

Akizungumza na Nipashe jijini Dar es Salaam jana, Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam la Kanisa Katoliki, Mhashamu Methodius Kilaini, alisema kitendo hicho hakikumvunjia heshima na kumdhalilisha Mwinyi pekee bali Watanzania wote.

Alisema kwa kifupi Kanisa nchini limepigwa na butwaa na kubaki na mshangao.

``Lakini pamoja na hayo yote tunampa pole nyingi Mzee Mwinyi. Tunamtaka asifadhaishwe na kitendo hicho,`` alisema.

Kilaini alisema jambo hilo linashangaza zaidi na kulifanya Kanisa liwe kama limemwagiwa maji, hasa ikizingatiwa kuwa kitendo hicho kimefanyika katika shughuli za kidini.

Hata hivyo, alisema pamoja na dosari hiyo, bado anaamini kwamba Watanzania hawajawa na tabia ya hujuma na kujitoa mhanga kama hiyo.

``Naomba suala hili lichukuliwe kama ajali tu, kwa vile siamini kwamba hali ya amani katika nchi yetu imefikia hapo,`` alisema.

Askofu huyo alisema hakuna jambo lolote baya ambalo alizungumza Rais Mwinyi ambalo lilifanya iwe sahihi apigwe.

``Lakini jambo hili sasa lisipotazamwa kwa makini, mambo ya dini yatakuwa sio ya kuaminika tena kama ilivyozoeleka,`` alisema.

Alisema kitendo hicho kinaweza kuwaweka viongozi mbali na wananchi kwa kuhofia usalama wao.

Askofu Kilaini aliwataka Watanzania hasa watu wa dini, kujenga utamaduni wa kuheshimiana na kuvumiliana hata kama mtu anazungumza au anatoa msimamo ambao hukubaliani nao.

Naye Askofu Dk. Stephen Munga wa KKKT Dayosisi ya Kusini Mashariki, alisema wakati Kanisa limebaki mdomo wazi, kuna haja ya vyombo vya dola kuchunguza kwa kina jambo hilo na kulikomesha.

Alisema haelewi hasa lengo la muumini huyo lilikuwa nini, lakini akasisitiza kwamba huenda kuna kikundi au watu wapo nyuma ya `mbabe` huyo.

``Kama yale mambo ya kujitoa mhanga yameshaanza kuota hapa petu, basi ni ishara kwamba Watanzania tunaelekea gizani, jambo hili haliashirii mema katika nchi yetu,`` alisema.

Askofu Munga alisema Kanisa limepigwa na butwaa na kujiuliza kuwa mtu huyo aliyefanya kitendo hicho, amezaliwa katika nchi gani?

``Jambo hili lina maswali mengi kuliko majibu, kweli kijana wa Kitanzania aliyezaliwa hapa, hajui wala hajaona ustaarabu wetu wa kuwaheshimu viongozi kama ni Mtanzania, basi anao uovu mkali kichwani pake, ambao amepandikizwa na kikundi fulani. Haya kama kweli ni punguani kama wengine wanavyosema, huo upunguani umeanza lini, tunaambiwa amekuwa akihudhuria ibada zote za Maulidi, kwanini upunguani wake ukamsubiri hadi Mwinyi aongee? Kwa nini huo upunguani haujaonekana kwingineko? Ndio maana tunasema jambo hili lina maswali mengi kuliko majibu,`` alisema.

Hata hivyo, Dk. Munga alionya kwamba suala hilo ni kubwa hivyo lisitolewe majibu rahisi kwamba mhusika ni punguani.

Alimtaka Mzee Mwinyi kutofadhaika na kukata tamaa kwa vile bado Watanzania wengi wanamheshimu, kutokana na mchango wake mkubwa wa kisiasa, kujamii, kiuchumi na kiutamaduni alioutoa wakati wa uongozi wake.

UVCCM walaani
Baraza Kuu la Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), limetoa tamko la kulaani kitendo cha kupigwa kwa Rais Mstaafu Mwinyi, kilichotokea juzi wakati wa sherehe za Baraza la Maulidi.

Akitoa tamko hilo jana kwa waandishi wa habari kwa niaba ya Baraza hilo, Mwenyekiti wa Jumuiya ya UVCCM, Masauni Yusuf Masauni, alikiita kitendo hicho kuwa ni cha kihuni, udhalilishaji, fedheha na utovu wa nidhamu.

Alisema kwa kauli moja Baraza hilo limesikitishwa na kitendo hicho, hasa ukizingatia kuwa kimefanywa na kijana wa Kitanzania ambaye amewaaibisha vijana wote wa Tanzania, kwa kuonyesha kuwa hawana nidhamu.

``Kwa ujumla Baraza limepokea kwa masikitiko makubwa kitendo hicho cha kihuni, udhalilishaji na cha fedheha alichofanyiwa kiongozi wetu mpendwa Mzee wetu Alhaji Ali Hassan Mwinyi,`` alisema Masauni.

Aliongeza kuwa kitendo hicho kilichofanywa na kijana huyo ni kinyume cha maadili ya dini zote na utamaduni wa Kitanzania kwa wazee wetu, viongozi na jamii kwa ujumla.

Kutokana na kitendo hicho, Baraza hilo limeitaka serikali ufanyike uchunguzi wa kina na wa haraka ili kubaini nia ya kitendo hicho cha kihuni na hatua kali za kisheria dhidi ya mhusika, zichukuliwe mara moja.

Pia alivitaka vyombo vya ulinzi na usalama viimarishe ulinzi kwa viongozi wastaafu na waliopo madarakani, ili kusiwe na matukio ya namna hiyo tena.

Baraza Kuu la Jumuiya ya Umoja wa Vijana lilikutana mjini Dodoma kwa muda wa siku sita kujadili mambo mbali mbali yanayohusu mustakabali wa CCM.

Mbeya nao waja juu
Wananchi wakiwemo viongozi wa dini mkoa wa Mbeya wameelezea kusikishwa na tukio la kupigwa kibao Rais Mstaafu Mwinyi ambapo wamewatupia lawama walinzi wake kwamba walikuwa wazembe kwa kushindwa kumlinda kwa umakini kiongozi huyo.

Wakizungumza na Nipashe kwa nyakati tofauti walisema tukio la kupigwa Rais Mwinyi limeiweka nchi katika kashifa mbaya mbele ya uso wa dunia na Tanzania kuonekana ni nchi isiyokuwa makini katika kuwalinda viongozi wake.

Mmoja wa wananchi hao, Abdallah Bugano, akizungumza na Nipashe alisema mazingira ya jinsi tukio lilivyotokea yanaonyesha kuwa walinzi wa Rais Mwinyi hawakuwa makini na ndiyo maana mtu aliyefanya kituko hicho aliweza kujipenyeza hatimaye kumnasa kibao kiongozi huyo.

``Tukio hili walinzi wa Rais Mwinyi ni wazembe sana, kwanini yule kijana alikwenda pale kama vile anataka kurekebisha vipaza sauti, ina maana hakukuwa na watu maalum wanaojulikana waliowekwa kuifanya kazi ya mitambo, huu ni uzembe,`` alisema Bugano.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Maaskofu wa Makanisa ya Kipentekoste mkoa wa Mbeya, Askofu Amos Igundu, alisema Wakristo wamelipokea tukio hilo kwa maskikitiko makubwa na kwamba kuna haja kwa vyombo vya usalama kujipanga upya kwa namna ya kuimarisha ulinzi kwa viongozi wakuu, hususani kwenye mikutano ama sherehe zinazojumuisha watu wengi.

Askofu Igundu alisema tukio hilo limeitia doa nchi na hivyo ni jukumu la vyombo vya usalama kufanya uchunguzi wa kina sababu za kijana huyo kuamua kuchukua hatua ya kumpiga kibao Rais Mstaafu Mwinyi.

Naye Katibu wa CCM Mkoa wa Mbeya, Albert Mgumba akizungumza na Nipashe kwa simu akiwa wilayani Kyela, alisema kitendo kilichofanywa na kijana aliyempiga kibao Rais mstaafu Mwinyi ni utovu wa nidhamu na kwamba inabidi achukuliwe hatu kali.

Imeandaliwa na Muhibu Said, Romana Malya, Simon Mhina, Mary Edward na Thobias Mwanakatwe.

SOURCE: Nipashe

Wednesday, March 11, 2009

Aliyempiga Mzee Ruksa!


Pichani ni mtuhumiwa Ibrahim Said Sultan maarufu kama (Ustaadh) ambaye alimzaba Rais Mstaafu, Alii Hassan Mwinyi kibao akiwa jukwaani akihubiri kwenye sherehe za Maulidi.

Cheki wananchi walivyo na hasira! Mzee Ruksa anapendwa! Bahati katoka na uhai wake hapo!

Kwa habari na picha zaidi mtembelee Kaka Michuzi:

Mzee Ruksa Apigwa Kofi Jukwaani!


Hivi kama Rais Mstaafu, Mzee Mwinyi si ana kuwa na wanausalama wake? Halafu ajabu wanakataa kuwa jambo hiyo ilitokea...wakati waandishi wa haabri wengi walishuhudia!

********************************************************************
Kutoka Ippmedia.com

Rais Mwinyi apigwa kofi jukwaani

2009-03-11
Na Muhibu Said

Rais Mstaafu Rais Ali Hassan Mwinyi jana alipigwa kofi la shavuni na muumini wa dini ya Kiislamu katika Baraza la Maulidi mara baada ya kuwataka Waislamu kujikinga na Ukimwi kwa kutumia kondomu kuliko kuwaambukiza watu gonjwa hilo hatari kwa jamii.

Rais Mwinyi ambaye pamoja na mambo mengine, alizungumzia masuala ya uchumi yanayoikumba nchi, alianza kuzungumzia vita dhidi ya ugonjwa wa Ukimwi, kwa kusema kuwa zinaa katika Uislamu ni jambo haramu moja kwa moja.

Mwinyi aliendelea kudai kuwa mtu akifanya zinaa, kwa kutumia mpira (kondomu), atakuwa amefanya dhambi moja, lakini akifanya bila kutumia mpira, mtu huyo ni dalali wa kutembeza zinaa na Ukimwi.

Baada ya hapo akauliza mashekhe, kwamba kufanya dhambi Mungu anaweza akasamehe, lakini yule ambaye atafanya dhambi bila kondomu, bora ni vipi?

Mwinyi akaendelea kusema: ``Dharura ya mtu asiyeweza kujizuia na kufanya zinaa, mashekh na maulamaa tufanyeje hapo?``

Baada ya kusema hivyo, akatoka muumini mmoja akapanda jukwaani na kumpiga Rais Mwinyi kofi upande wa shavu la kuume, akapepesuka almanusra aanguke na kuokolewa na maafisa usalama.

Hali hiyo ilisababisha Mwinyi asitishe hotuba yake baada ya maafisa wa usalama na polisi kuvamia jukwaa na kumkamata mtuhumiwa aliyefanya kitendo kisicho cha kiuungwana.

Katika harakati za kumkamata, askari hao walianza kumpiga na ukumbi ukapatwa na taharuki kubwa.

Baada ya kumdhibiti mtu huyo ambaye alitia dosari sherehe hizo zilizokuwa zimeandaliwa vizuri, wanausalama hao walimpakia kwenye gari na kuondoka naye.

Baadhi ya waumini walitaka kukimbia, wengine wakaenda kuwasaidia maafisa usalama kumkabili mtu huyo aliyempiga Rais Mwinyi maarufu kama Mzee Ruksa.

Miongoni mwa watu waliomkabili kijana huyo ni pamoja na viongozi wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) na waumini wengine.

Taharuki hiyo ilisababisha waandishi ambao walikuwa wakifuatilia shughuli nzima ya Baraza la Maulidi, baadhi kutaka kukimbia na wengine kujua kulikoni.

Hali hiyo ilidumu kwa muda wa dakika mbili, huku viongozi wa Bakwata wakiwatuliza watu kutulia ili shughuli iendeleee.

Nipashe jana iliwasiliana na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, juu ya tukio hilo lakini akasema kwamba amewasiliana na Kamanda wa Polisi Ilala, na tukio hilo halijatokea.

Nipashe ilipomuuliza kwamba mbona waandishi wa habari wameshuhudia tukio hilo, na pia Kaimu Mufti, Sheikh Suleiman Gorogosi, amewaomba waumini radhi kwa rabsha iliyotokea, Kamanda Kova alisema`` ``Wasiliana na Kamanda wa Ilala kwa habari zaidi.``

Akiomba radhi, Sheikh Gorogosi alisema mtu aliyefanya kitendo hicho cha aibu ni kichaa. Hadi tunakwenda mitamboni jina la mtu huyo lilikuwa halijajilikana.
Baada ya hapo, Mwinyi aliendelea kuhutubia.

Baada ya hapo, Nipashe iliwasiliana na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Faustine Shilogile, ambaye alisema kwamba alikuwa hana taarifa kamili kwa kuwa alikuwa katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam.

``Ndio naelekea huko sasa hivi baada ya kuambiwa na askari waliokuwa huko Diamond Jubilee kupata habari kamili,`` alisema Shilogile.

Rais Mwinyi ni rais mstaafu anayependwa na wananchi kwa kiwango kikubwa, na kila anapohudhuria hafla mbalimbali amekuwa akishangiliwa kwa nguvu kutokana na mchango wake katika kubadili hali ya mambo nchini.

Ilikuwa ni chini utawala wake, akiwa Rais wa awamu ya tatu mageuzi makubwa ya kiuchumi na kisiasa yalianza kutekelezwa nchini ikiwa ni pamoja na kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi vya kisiasa.

Jina la Mzee Ruksa alipachikwa baada ya kuwa mkali kutokana na vitendo vya baadhi ya watu kuvamia na kuvunja mabucha ya nyama ya nguruwe, akiwakanya na kusema kwamba kila mtu ana ruksa ya kula atakacho.

Kutokana na utaratibu wa utawala wa kuachia wananchi uhuru wa kufanya watakalo ilimradi hawavunji sheria, alijiziolea umaarufu mkubwa na kupachikwa jina la Mzee Ruksa.

SOURCE: Nipashe

Tuesday, March 10, 2009

Kukandwa na Nyoka

Wazungu bwana! Yaani sasa unaweza kulipa hela kukandwa (massage) na mijoka! KHAA!

***********************************************************************





It's a massage that is sure to make most people's skin crawl, but one woman has got herself in a twist with her latest massage technique.
Ara Barak claims her pet snakes make the ideal masseurs as their slithering causes a massage sensation when placed on a person's skin.
Ms Barak said she discovered her pet's 'therapeutic value' after noticing her friends became more relaxed after holding them.

Meirav Stardinner receives a snake massage from Ada Barak who says her pets are high in 'therapeutic value' 'Some people said that holding the snakes made them feel better, relaxed,' she said. 'One old lady said it was soothing, like a cold compress.'
The owner of Israel's Barak's Snake Spa said her pets are able to give massage as their slithering causes a rubbing sensation on the body. Ms Barak had relied on exhibiting her scaly friends to make money, but found there is more cash rolling in from people wanting a massage - reptile therapy style.

Smaller snakes are used for lighter massage on areas such as the face while bigger ones are used to give deep tissue therapy The larger snakes are used for deep massage while the smaller creatures are used to give a lighter touch - all for a mere £30.
And those with a slight reluctance to have a snake massage will be pleased to know the reptiles are all non-venamous.

But if the thought of reptiles is too much, Ms Barak also offers a rodent-style massage where mouse and rats are placed on the bottom of people's feet instead.

Wodi ya Uzazi Hospitali ya Temeke


Wakinamama waliojifungua katika hospitali ya Temeke jijini Dar es Salaam hivi karibuni wakiwa wamejipumzisha kabla ya kuruhusiwa! Ninachojiuliza ni kwamba watu wanazaliana kupita kiasi, huduma ni hafifu ama kuna haja ya kupeana zamu ya kuzaa ili wake zetu wasilale chini?

Wadau kusema kweli hali hii inasikitisha kupita kiasi,kwa mtindo huu hata watoto wanaozaliwa hapo wanaweza kutoka salama kweli katika misingi ya yale magonjwa ya kuambukizana haswa katika msongamano kama huu,wengi watasema ati ni umaskini.! ni umaskini kweli huu.!????.Picha hizi kwa hisani kubwa ya mpoki.blogspot.com/
**********************************************************

Wadau, Mwaka 2009, bado tuna hali mbaya hivyo Bongo. Je, huko chooni/bafuni mwa hospitali kuna hali gani? Je, una uhakika utampata mtoto uliyemzaa au utapata wa mwingine hapo? Khaa! Wanawake wangapi wana share kitanda? Hivi na Mzee Bush si alitoa hela za misaada kwa ajili ya hopsitali hiyo alipotembelea Bongo mwaka juzi?

Inasikitisha

Translation:

Doctor - There is nothing more we can do for the patient. Try to treat him with your love.

Wife - All these hardships and poverty, where will the love come from?

Patient - When you hear talk like that know that you have been buried alive!

**********************************************

Ninakumbuka Bongo miaka ya 80, huko kwenye mahospitali walikuwa wanafukuza wagonjwa ambao wanajua watakufa. Walikuwa wanasema wazi kuwa hawawezi kupoteza dawa kwenye watu ambao watakufa wakati wanaweza kuwapa watakaopona.

Kipanya Leo


TRANSLATION:

When prisoners are allowed to meet with their husbands/wives.

Comment from Prisoner: My friends, please step out so that I may finish my business with my wife.

Ndege Imeanguka Ziwa Victoria!!!


Picha kutoka AFP
Kutoka ippmedia.com

Cargo Plane crashes in Lake Victoria, at least 7 die

2009-03-10
By ENTEBBE, Uganda

An Ilyushin cargo plane on a logistical mission to African peace forces in Somalia crashed into Lake Victoria yesterday after taking off in Uganda with 11 people on board, including three Burundian officers.

Seven of those on board were confirmed dead, and an aviation source said he feared all 11 had been killed. ``It plunged into the lake and went down deep,`` the source said.

Rescue boats and divers scoured the lake`s choppy waters for survivors some 7 km (4.3 miles) from Uganda`s main airport at Entebbe, where the plane began its flight. Two wheels and some wreckage were brought onshore.

Ugandan military sources had initially identified the aircraft as an Antonov, but the Ugandan government later said it was a chartered Ilyushin 76.

It was taking tents and water purification equipment to Somalia, where Uganda and Burundi both have soldiers in a small African Union peacekeeping mission, Ugandan officials said.

The aircraft burst into flames before plunging into the lake and hitting two fishing boats, injuring four fishermen, Uganda`s government spokesman said.

``We have not rescued anybody... Time is really working against us,`` said Information Minister Matsiko Kabakumba.
A Civil Aviation Authority spokesman said there were four crew and seven passengers on board the aircraft when it crashed.

A Burundi army spokesman confirmed three of its soldiers -- a brigadier general, a colonel and a captain -- had died.

``The information we have is that the plane crashed five minutes after taking off at Entebbe Airport. Burundi deplores the death of three of its officers who were on the plane,`` Adolphe Manirakiza told Reuters in Bujumbura.

There was no immediate word on what caused the crash.
``We`re not ruling anything out, and we`re not ruling anything in,`` Kabakumba said, adding that the plane had flown some 20 missions in recent weeks.

Russian media said the pilot and copilot were Russian citizens and the navigator and flight engineer were Ukrainians.

All four were killed in the crash, Ruslan Madiyev, an official at the Russian embassy in Kampala, told RIA news agency.

Uganda said the flight also carried one Ugandan soldier, an Indian citizen, a Ugandan loadmaster and a South African peacekeeper.

Africa`s air accident rate is six times worse than the rest of the world, the International Air Transport Association says.

SOURCE: Guardian

Mwanamke atapeliwa dola $400,000 na WaNigeria!

Ndio maana hao matapeli hawaachi mchezo wao. Wanajua watamnasa mtu!!!

*************************************************************************
Oregon Woman Loses $400,000 to Nigerian E-Mail Scam

Monday , November 17, 2008

An Oregon woman who is out $400,000 after falling for a well-known Internet scam says she wasn't a sucker or an easy mark.
Janella Spears of Sweet Home says she simply became curious when she received an e-mail promising her $20.5 million if she would only help out a long-lost relative identified as J.B. Spears with a little money up front.

Spears told KATU-TV about the scammers' ability to identify her relative by name was persuasive.

"That's what got me to believe it," She said. "So, why wouldn't you send over $100?"

Spears, who is a nursing administrator and CPR teacher, said she mortgaged the house and took a lien out on the family car, and ran through her husband's retirement account.

"The retirement he was dreaming of — cruising and going around and seeing America — is pretty much gone for him right now," she said.

She estimates it will take two years to clear the debt that accumulated in the more than two years she spent sending money to con artists.

Her family and bank officials told her it was all a scam, she said, and begged her to stop, but she persisted because she became obsessed with getting paid.

The scheme is often called the "Nigerian scam" and it's familiar to many people with e-mail accounts. It still exists and it still works.

Spears first sent $100 through an untraceable wire service as directed by the scammers. Then, more multimillion dollar promises followed so long as she sent more money.

The scammers sent Spears official-looking documents and certificates from the Bank of Nigeria and the United Nations. President Bush and FBI Director Robert Mueller were also involved, the e-mails said, and needed her help.

They sent official-looking documents and certificates from the Bank of Nigeria and even from the United Nations, saying her payment was "guaranteed."

But it wasn't and now Spears is paying the price for her costly lesson.

"The hope is [other people] are not going to fall as hard as I fell," Spears said

Sunday, March 08, 2009

Siku ya Kimataifa ya Akina Mama


Leo tunaahimisha siku ya akina mama duniani! Kwa vile wanaume bado hawatuthamini napendekeza akina mama wote kwa siku ya leo tu wakubali kunyima wanaume wao huduma ya kawaida. Yaani kupika, kufua, mapenzi, kuwachotea maji, kupokea wageni n.k. Hapo wanaume wataelewa thamani yetu!

********************************************************************************
Leo pia nakumbuka wimbo maarufu wa Helen Reddy. Inaitwa ' I am Woman' (Mimi ni Mwanamke). Huo wimbo unawapa nguvu akina mama wanaoisikia!

I Am Woman

-Artist: Helen Reddy from "Helen Reddy's Greatest Hits": EMI ST 11467
-peak Billboard position # 1 for 1 week in 1972
-Words and Music by Helen Reddy and Ray Burton

I am woman, hear me roar
In numbers too big to ignore
And I know too much to go back an' pretend
'cause I've heard it all before
And I've been down there on the floor
No one's ever gonna keep me down again

CHORUS
Oh yes I am wise
But it's wisdom born of pain
Yes, I've paid the price
But look how much I gained
If I have to, I can do anything
I am strong (strong)
I am invincible (invincible)
I am woman

You can bend but never break me
'cause it only serves to make me
More determined to achieve my final goal
And I come back even stronger
Not a novice any longer
'cause you've deepened the conviction in my soul

CHORUS

I am woman watch me grow
See me standing toe to toe
As I spread my lovin' arms across the land
But I'm still an embryo
With a long long way to go
Until I make my brother understand

Oh yes I am wise
But it's wisdom born of pain
Yes, I've paid the price
But look how much I gained
If I have to I can face anything
I am strong (strong)
I am invincible (invincible)
I am woman
Oh, I am woman
I am invincible
I am strong

FADE
I am woman
I am invincible
I am strong
I am woman


Friday, March 06, 2009

Open Casting Call 3-6-09

Mara Casting is looking for background actors for the ABC TV pilot See Kate Run. They are holding an open casting call tomorrow, Saturday, March 7, 2009 from 11:00 a.m. to 3:00 p.m. at 300 W. 1st St Boston, MA.

Here are the details:
(Yes, it is a warehouse- and looks like one!)It is at the corner of W. 1st St and E St.The entrance door faces W. 1st St and has a sign on it that says “300 W. 1st”.*If you are at a door that does not have this sign, please find the correct one…We only have access to that one door.*Parking is open and free. There are a number of parking lots around this entrance and we ask that you please park legally in one of them.

On-street parking may be limited to residents only.To be eligible to work as an extra on this pilot, you must be able to show proof that you are legally able to work for any employer in the U.S.What you should bring:-Completed sizecard (DOWNLOAD from maracasting.com/abc.html)-Headshot (or a recent photo, you MUST bring a photo)-Resume-Pen (Always, to casting calls and to the set, bring a pen)With so many people showing up at the casting call, those who come with what is asked are already ahead of the game!

ARRIVING EARLY DOES *NOT* GIVE YOU ANY ADVANTAGE!THIS ISN’T LIKE GETTING TICKETS TO A CONCERT,EVERYONES PHOTO/SIZECARD/RESUME, ETC. WILL BE PUT IN THE SAME BOX!

See Kate Run (formerly I, Claudia) stars Amy Smart as a young prosecuting attorney who one day is going to be a serious contender for president of the U.S.

Msiba Zimbabwe - Mrs. Susan Tsvangirai

Wadau, nimesoma kwa masikitiko habari ya kifo cha Susan Tsvangirai, mke wa Waziri Mkuu wa Zimbabwe, Morgan Tsvangirai. Alipata ajali leo huko Zimbabwe baada ya gari aliyokuwa anasafiria kugongana na lori. Majeruhi wengine ni dereva wa gari, msaidizi wa Mh. Tsvangirai, na Mh. Tsvangirai mwenyewe. Marehemu ameacha mume na na watoto sita.

Mungu awape nguvu famili ya Tsvangirai katika kipindi hiki kigumu. Mungu ailaze roho ya Dada Susan mahala pema mbinguni. Amen.

Natoa kumbukumbu ya Dada Susan hapo chini:


Kwa habari zaidi someni:

http://www.dailymail.co.uk/news/worldnews/article-1160066/Zimbabwe-PM-Tsvangerais-wife-killed-truck-smashes-official-car--escapes-minor-injuries.html

http://news.bbc.co.uk/2/hi/africa/7929136.stm

http://www.timesonline.co.uk/tol/news/world/africa/article5859954.ece
*********************************************************************************






Waziri Mkuu wa Zimbabwe apata Ajali ya Gari!

BREAKING NEWS: CNN wanasema kuwa mke wa Morgan Tsvangirai amefariki katika hiyo ajali!

Habari kutoka Zimbabwe zinasema kuwa Waziri Mkuu mpya wa nchi hiyo, Mh. Morgan Tsvangirai amepata ajali ya gari akielekea kwao Buhera, Zimbabwe. Nitaposti habari zaidi nikipata.

***********************************************


(CNN) — Zimbabwe’s new prime minister, Morgan Tsvangirai, has been hospitalized after his car collided with a large truck, officials with his party and his spokesman told CNN on Friday.
“Yes I can confirm that he was involved in a car accident along Harare-Masvingo road,” said Tsvangirai’s spokesman, James Maridadi. “He has been brought to Harare and doctors are looking at him at a hospital.”

Maridadi would not say how serious Tsvangirai’s injuries are as a result of the head-on collision. Tsvangirai was in the car with his wife, an aide, and the driver, he said. All four are being assessed by doctors.

They were en route to Tsvangirai’s hometown of Buhera, south of the capital, Harare, when the accident occurred, Maridadi said.

Steven Kanumba na Wema Sepetu


(Picha kutoka Global Publishers)

Wadau, wengi wetu tunaelewa mapenzi yanavyoenda. Leo unampenda mtu kupita kiasi, kesho unamchukia, huna hamu naye. Unaweza kumwona mtu na kumpenda mpaka unaona unachangayikiwa huwezi kufikiria kitu kingine. Na pia tunaelewa kuwa kuna yale mapenzi ambayo si mapenzi ila kutaka raha ya kimwili tu. Mtu akitosheka anaanza kwenda pengine. Unaweza kumpenda mtu mapaka ukaona wengine wana sura mbaya kama Chakubanga. Yaani mapenzi ni kitu cha aina yake. Lakini yakifa....mhhhh!!!




Hii picha ilipigwa mwezi Novemba mwaka jana. Unaweza kusoma maelezo hapa:
http://worldhotstars.blogspot.com/2008/11/mapenzi-ya-wema-sepetu-na-kanumba.html

Thursday, March 05, 2009

Yaliyompata Wema Sepetu

Sijui niseme nini. Naona macelebrity wetu wanataka kuanza kuwa na maskandali kama za Hollywood. Sina habari kamili lakini inaelekea Miss Tanzania 2006 Wema Sepetu, alichukua gari ya mwigizaji maarufu Steven Kanumba aka Denzel wa Tanzania, na kuliharibu. Kama ilikuwa ajali si amsamehe na wapatane kuhusu matengenezo? Kwa sasa macho yote kwao.

*********************************************************
mrembo wema sepetu akipewa pole na rafiki yake baada ya kuachiwa kwa dhamana leo mahakamani kinondoni anakikabiliwa na shtaka la kuharibu gari la mwigizaji steve kanumba. mrembo huyu aliyepata kuwa miss tz alikuwa rumande toka wiki iliyopita baada ya kukosa dhamana alipofikishwa kizimbani kwa mara ya kwanza
mama mzazi wa wema sepetu akisaidiwa na nduguye wa kiume ilibidi watumie nguvu wema aondoke nao wao na sio rafikiye ambaye alifika hapo mahakamani

**********************************************************************************


Former Miss Tanzania Charged

2009-03-04

By Hellen Nachilongo

Miss Tanzania 2006 Wema Sepetu was yesterday brought before the Kinondoni Resident Magistrate`s Court over allegations of malicious damage to a motor vehicle.

Sepetu (20), a resident of Tabata Senene, and Aisha Jumbe (23) appeared before the magistrate in charge Emilius Mchauru to answer the charges levelled against them.

Inspector of Police Nassoro Sisiwaya told the court that willfully and unlawfully the accused maliciously damaged a motor vehicle wind screen with registration no T 993 ASD Toyota RAV 4 brand, the property of actor Kanumba Stephen.

It was alleged that the offence was committed at Magomeni Mikumi area in Kinondoni District on January 1, this year.

However, the accused pleaded not guilty just after the charge was read to them and were returned to remand custody after failing to meet bail conditions.

The court required two reliable sureties working from any recognised or established company to sign a bond of 500,000/- for each of the accused. No body stepped up to rescue the charged duo.
The case was adjourned to March 18, this year when it comes up for mention. Investigation is still in progress.

SOURCE: Guardian
****************************************************************

Wema Sepetu atupwa Segerea

2009-03-04
By Adam Fungamwango

Miss Tanzania wa mwaka 2006, Wema Sepetu (20), jana alifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam akikabiliwa na shitaka la kuharibu mali baada ya kuvunja kioo cha gari chenye thamani ya Sh. milioni moja, mali ya muigizaji wa filamu, Steven Kanumba.

Sepetu alisomewa shitaka lake mbele ya Hakimu Emilius Mchauro, analiyesikiliza kesi hiyo.

Mwendesha Mashitaka Insepkta wa Polisi Nassoro Sisiwaya alidai mahakamani hapo kuwa, Sepetu na mwenzake Aisha Jumbe (23) wanadaiwa Janauari 29 mwaka huu, saa 3:00 usiku huko Magomeni Mikumi, walivunja kioo cha mbele cha gari la mlalamikaji chenye thamani ya Sh 1,000,000.

Ilidaiwa kuwa gari hiyo aina ya Rav 4, lenye namba za usajili T 990 ASD, ilivunjwa kioo na washitakiwa hao na kusababisha hasara ya fedha hizo.

Mahakama iliwataka washitakiwa kudhaminiwa na wadhamini wawili watakaosaini hati ya dhamana ya Sh. 500,000 kila mmoja.

Washitakiwa hao walikana shitaka hilo, na wamepelekwa gereza la Segerea baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana.

Aidha, mlalamikaji wa kesi hiyo Kanumba hakutokea mahakamani hapo.

Hakimu alimhoji mmoja wa aliyejitokeza kuwa mdhamini kama ana hati za dhamana, ambapo badala ya kuzitoa alidai kuwa amezisahau ndani ya gari.

Kwa kutumia busara, Hakimu Mchauro alimtaka mdhamini huyo azifuate, lakini alitumia zaidi ya dakika tano bila kurejea.

``Hii ni mpya, hakimu anamsubiri mdhamini aliyesahau hati ndani ya gari!.

Labda huyu mheshimiwa alitaka watu wajue tu kama na yeye ana gari,`` alisema Hakimu Mchauro. huyo.

Baada ya kusubiri vya kutosha Hakimu aliahirisha kesi hiyo hadi Machi 18 mwaka huu na hapo ndipo pakawa na ugumu wa wadhamini kukubaliwa dhamana kwa sababu tayari hakimu alikuwa ameshasaini.

Sepetu muda wote wa kesi hiyo ilipokuwa inasikilizwa alionekana kutokujali kufikishwa kwake mahakamani hapo, alikuwa yuko kawaida kama vile hakuna kilichotokea na hata baada ya kesi kusomwa alisikika akiwapigia kelele waandishi hasa wapiga picha wampige picha wanazotaka.

Na hata alipotolewa kwenye mahabusu ya polisi kupelekwa kwenye basi la jeshi la magereza, bado alikuwa akipiga kelele kwa waandishi akitaka waandike huku akiwataka askari waache wapiga picha wampige wanavyotaka, lakini haikueleweka alikuwa akisema hivyo kwa hasira au alipenda mwenyewe.

Kwa mara ya kwanza, kesi hiyo ilifikishwa kwenye kituo cha polisi Magomeni mwezi uliopita na Kanumba, ambapo Wema alitiwa mbaroni na kulala kituoni hapo kwa muda wa siku mbili.
Kesi hiyo itatajwa tena, Machi 18, mwaka huu.

SOURCE: Nipashe

Pia soma DAILY NEWS: http://www.dailynews.co.tz/home/?n=632

Wednesday, March 04, 2009

Mr. Bobos Class - Taarifa za Ajali

Habari ya kazi, napenda kukutaarifu kwamba nimekuwa nikishughulika katika sehemu inayohusiana na ajali kwa zaidi ya miaka 10.

Nimeshuhudia jinsi ajali zinavyowaathiri watanzania wengi kijamii, kiuchumi na kisaikolojia. Hivyo, ili kusaidia katika vita dhidi ya jinamizi la ajali, nimeamua kuanzisha Blog inayoitwa Mr. Bobos Class (http://ajali-traumaclass.blogspot.com), ni blog inayotoa taarifa mbalimbali juu ya madhara ya ajali mbalimbali zitokanazo na matumizi ya Magari na mashine, mbalimbali za kazi .Mbali ya kutoa taarifa pia ina lengo la kuwaelimisha waliopata madhara hayo ni jinsi gani wanaweza kupata msaada baada ya kuathirika kutokana na ajali mbalimbali.Blog hii itaungana na wadau mbalimbali wanaohusika na masuala ya ajali kwa njia moja au nyingine, kuelimisha na kutoa ushauri.

Tafadhali wajulishe watanzania kupitia blog yako juu ya hilo na kwamba michango yao inahitajika ili tuweze kupambana na hili jinamizi la ajali hasa ajali za barabarani.
Asante,naomba pia ushirikiano wako.

Mr. Bobos Class.

Tuesday, March 03, 2009

Msiba ITV - Rehema Mwakangale

Picha na maelezo kutoka Michuzi Blog:

Mtangazaji wa ITV Rehema Mwakangale (kulia) ametutoka leo asubuhi katika hospital ya Mikocheni alikokuwa amelazwa. Kwa Mujibu wa taarifa kupitia Radio One, mipango ya mazishi itakuwa kwa bibi yake Sinza karibu na Deluxe bar. Mola ailaze roho ya marehemu peponi. AMINA/AMEN.

Kwa habari zaidi soma:

http://www.ippmedia.com/ipp/guardian/2009/03/04/132754.html

Bandari ya Dar es Salaam mwaka 1866

Unakwenda kupanda Treni uende kazini halafu.....

Monday, March 02, 2009

Original Designs

Hello,

For anyone interested in Tshirts and other things with Swahili sayings and words and Tanzania inspired designs, go to;

http://www.cafepress.com/hiari

Thanks
Lora

Rais Castro wa Cuba alipotembelea Bongo 1977

Mimi nilikuwa Form One Zanaki Girls, wakati huo 1977. Tulikuwa tunasoma darasani kama kawaida. Ghafla Mwalimu Mkuu katuambia lazima tuende Ikulu kumpokea Rais Castro wa Cuba. Tuliaacha masomo, na kukaguliwa uniform. Tulitembea hadi Ikulu, na tulipangwa ndani ya geti ya Ikulu upande wa bahari. Nakumbuka Castro alikuwa amevaa magwanda ya kijani na mandevu yake halafu alionekana mrefu kweli alivyonipita. Alitupita sisi wanafunzi huko tukishangalia 'CASTRO - NYERERE'! Baadaye kulikuwa na maneno kuwa eti Rais Castro alijialika Bongo ndo maana watu walikuwa hawajajiandaa vizuri. Sijui kama ni kweli lakini. Lakini nikicheki uso wa Mwalimu kwenye hii picha...sijui.

*********************************************************

Kwa habari zaidi soma:

Skandali ya 'Radar' Bongo


Haya, nangojea kuona kama watu wataburuzwa mahakamani kama hao kwenye skandali zingine!

*************************************************************

Kutoka IPPMEDIA.Com

PCCB traces foreign links to radar scam

By Lydia Shekighenda

The Prevention and Combating of Corruption Bureau (PCCB) is now contacting various sources outside the country in a new buildup of `convincing evidence` in the on-going investigation into the controversial purchase of the civilian and military air traffic control (radar) system, `The Guardian` has established.

The anti-corruption watchdog confirmed last week to have received the radar case file from the Director of Public Prosecutions, Eliezer Feleshi, for further investigation.

PCCB Public Relations Officer Doreen Kapwani told `The Guardian` that the file has been returned from the DPP with instructions to carry out further investigations of the radar scandal.

``It is true, we (PCCB) have received the radar case file back from the DPP and we are now proceeding with the investigations outside the country,`` she said.

Over a week ago, a section of the local media speculated that the DPP had returned the radar case file to the PCCB because of insufficient evidence for the prosecution of the suspects implicated in the transaction of the military radar bought in 2002 at 52bn/-.

The DPP has instructed the PCCB to carry out further investigation on the circumstances leading to the transaction of the radar.

However, Kapwani would not state when the investigation will be completed and the file returned to the DPP.

``I am not in a position to state how long the investigation will take and when the file will be taken back to the DPP,`` she said.

She urged people to be patient while the corruption watch-dog was carrying out the investigation, saying that it would update the public on the progress once the process was completed.

Kapwani however, called upon the people and other stakeholders to co-operate in giving out information and evidence against the suspects whenever they will be required to do so.

The Tanzania government bought the radar from British Aerospace at a price of 52bn/- in 2002, but it was later established that the price was too high.

It was learnt that part of a `commission` fee of 16bn/- equivalent to 30 per cent of the total radar purchase price, paid to Envers Trading may have been used to bribe top government officials.

The PCCB concluded its investigation on the radar transaction scandal and handed the file to DPP in July last year, seeking formal consent to proceed with prosecution.

The key individuals being investigated by the UK`s Serious Fraud Office (SFO) include ex-attorney general Andrew Chenge, former Bank of Tanzania governor Dr Idris Rashid, and well-known local businesspersons Tanil Somaia and Shailesh Vithlani.

Both local and foreign investigations into the allegations forced Chenge to resign from a cabinet post last year.

However, ever since, there has been no reported progress of investigations on other individuals linked to the scandal.

SOURCE: Guardian

Rais Obama na Ndugu Zake White House

Pichani ni kaka yake Rais Obama, Abongo, Mama yake wa Kambo Mrs. Obama (aliyevaa nguo ya njano) anayekaa Uingereza kwenye nyumba za Council, kulia kabisa ni Mark Ndesanjo, na David Ndesanjo (mama yao ni mzungu aliyezaa na Barack Sr. ). Hebu cheki Mark anavyofanana na rais!

Unaweza kupata habari kamili kwa kubofya hapo chini:

http://www.dailymail.co.uk/news/worldnews/article-1158473/From-Bracknell-Kenya-Washington-First-picture-Obama-British-stepmother-inside-White-House.html

Kipanya Leo


Translation:
Leader sitting at Desk - In the past it was possible to steal from my office. Now, if I steal I will have to use my entire pension as bail!

Rais wa Guinea -Bissau Ameuwawa!

(pichani) Mkuu wa majeshi wa Guinea Bissau aliyeuawa jumapili na Rais Viera (kulia) Picha ya chini, Rais Viera na mke wake. Watu wanasema urafiki wao uliisha zamani!

Jamani fujo zinaanza tena barani Afrika. Kwa wadau waliokuwepo miaka ya sabini/themanini ilikuwa karibu kila siku unasikia rais huyo kauwawa, yule kapinduliwa, nchi imebadilisha jina n.k.
Leo, nimesoma kwa majonzi habari ya rais wa Guinea-Bissau , Mh. Joao Bernardo Viera, kauwawa na kundi la wanajeshi wa nchi hiyo! Aliongoza nchi hiyo kwa miaka 23.

Mungu ailaze roho yaka mahala pema mbinguni. AMEN.
*********************************************

Soldiers assassinate Guinea-Bissau President

Soldiers assassinated the president of Guinea-Bissau in his palace Monday hours after a bomb blast killed his rival, but the military insisted no coup was taking place in the West African nation.

A military statement broadcast on state radio attributed President Joao Bernardo "Nino" Vieira's death to an "isolated" group of unidentified soldiers whom the armed forces said they were now hunting down.

The capital, Bissau, was calm but tense despite the pre-dawn gunfight at the palace, which erupted hours after armed forces chief of staff Gen. Batiste Tagme na Waie — a longtime rival of the president — was killed by a bomb blast at his headquarters.

The former Portuguese colony has suffered multiple coups and attempted coups since 1980, when Vieira himself first took power in one. The United Nations says the impoverished nation on the Atlantic coast of Africa has recently become a key transit point for cocaine smuggled from Latin America to Europe.

Following an emergency Cabinet meeting on Monday, military spokesman Zamora Induta said top military brass told government officials "this was not a coup d'etat."

"We reaffirmed our intention to respect the democratically elected power and the constitution of the republic," Induta said. "The people who killed President Vieira have not been arrested, but we are pursuing them. They are an isolated group. The situation is under control."

The constitution calls for parliament chief Raimundo Pereira to succeed the president in the event of his death.

Prime Minister Carlos Gomes Jr. said the fact that the military did not go through with a coup deserves praise. "The military showed their patriotism by not seizing power," he said, adding that both Vieira and Waie will receive state funerals in the coming days.

Vieira had ruled Guinea-Bissau for 23 of the past 29 years. He came to power in the 1980 coup, but was forced out 19 years later at the onset of the country's civil war. He later returned from exile in Portugal to run in the country's 2005 election and won the vote.

The armed forces' statement dismissed claims that the military killed Vieira in retaliation for Waie's assassination late Sunday. The two men were considered staunch political and ethnic rivals and both had survived recent assassination attempts.

Vieira, from the minority Papel ethnic group, once blamed majority ethnic Balanta officers for attempting a coup against him, condemning several to death and others to long prison sentences.

Among them was Waie, who in the late 1980s was dropped off on a deserted island off the coast of Guinea-Bissau, according to Waie's chief of staff, Lt. Col. Bwam Namtcho. Waie was left there for years before he was allowed to return and officially pardoned by Vieira.

Namtcho said the bomb that killed Waie had been hidden underneath the staircase leading to his office.

Hours later, volleys of automatic gunfire rang out for at least two hours before dawn in Bissau and residents said soldiers had converged on Vieira's palace.

The Portuguese news agency LUSA reported that troops attacked the palace with rockets and rifles. The president's press chief, Barnabe Gomes, escaped but was struck by a bullet in his right shoulder, LUSA said.

It was the second attack on Vieira in recent months. In November, Vieira's residence was attacked by soldiers with automatic weapons who killed at least one of his guards. The president complained later that the army never intervened, leaving his presidential guard to fight off the attackers.

In January, Waie received a call from the presidency asking him to come at once, said Namtcho. But when Waie stepped outside to get into his car, unidentified gunmen opened fire on the car. Waie narrowly escaped and Namtcho says he assumed the attack had been ordered by the president.

Luis Sanca, security adviser to Prime Minister Carlos Gomes Jr., confirmed that the president had died but gave no details.

The African Union condemned the killings, calling them "cowardly and heinous attacks which have come at a time of renewed efforts by the international community to support peace-building efforts in Guinea-Bissau."

In Lisbon, the Portuguese Foreign Ministry lamented Vieira's death and said it was "fundamental that all political and military authorities in the country respect the constitutional order."

Portugal said it would call an emergency meeting of the Community of Portuguese-Speaking Countries, an eight-member organization based in Lisbon.
___

Associated Press writers Todd Pitman and Rukmini Callimachi in Dakar, Senegal and Daniel

Kwa habari zaidi someni:

http://news.yahoo.com/s/ap/20090302/ap_on_re_af/af_guinea_bissau

http://allafrica.com/stories/200903020710.html

http://news.xinhuanet.com/english/2009-03/02/content_10929438.htm

http://www.google.com/hostednews/ap/article/ALeqM5gJesugYieOra7PfjTwVraPl9gg_wD96LV7180

Saturday, February 28, 2009

Request for Participants


Kibira Films International is looking for participants in the upcoming documentary titled "TWO AFRICAS IN AMERICA"...One African, One American. This documentary will examine the relationships between Africans and African Americans in the United States.

If you have any opinion on this topic and would like to participate, please send your contact information to info@kibirafilms.com. We will contact you and make arrangements of how we can include your opinion in the documentary.
Thank you!

Kibira Films International

Wednesday, February 25, 2009

Kiwanda cha Crisps (Potato Chips) Bongo

(Picha na Maelezo na picha kutoka Lukwangule Blog)

Katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa, Getrude Mpaka (anayecheka) akiwa ndani ya kiwanda cha Crispo cha Iringa kinachotengeneza viazi vya kutafuna pamoja na Bodi ya wakurugenzi ya DANIDA iliyofadhili kiwanda hicho kupitia mpango wa B2B . Picha hii ni kwa hisani ya Frank Leonard ambaye ana makazi yake kwa watani zangu wala mnyama.
*********************************************************

Haya wapenzi wa crisps/potato chips mtafaidi sasa. Kiwanda cha kutengeneza snacks tamu kimefunguliwa huko Iringa. Frito Lay na Utz mlie tu.Mlioko huko Bongo hebu tuambie ladhaa ikoje. Nina imani zitakuwa tamu sana na zenye 'quality' safi.
Lakini natumani haitakuwa kama kile kiwanda cha SIHA mikate. Wadau mnaoikumbuka. Ilikuwa lazima itumie unga ngano kutoka Canada tu ndo mkate iwe nzuri. Je, hiki kiwanda cha Iringa kinatumia viazi kutoka wapi?

Sweet Eazy Jumamosi


Ndege Yanguka Uholanzi!

Wadau, ndege imeanguka huko Amsterdam, Uholanzi. Ilikuwa ndege ya Uturuki. Habari zinasema kuwa watu 9 wamekufa, na zaidi ya 5o wameumia. Ilikuwa imebeba watu 135. Ndege ilikuwa inatoka Uturuki kwenda Uholanzi na ilikuwa katika harakati za kutua kwenye uwanja wa ndege ya Schipol. Abiria waliopona wanasema kuwa wala hawakuonywa kuwa ndege inaanguka. Waliambiwa wafunge mikanda ya viti kwa ajii ya kutua.

Naona ndege zinafululiza kuanguka sasa. Ilianza na ile ya Continental Airlines Flight 1549 iliyoanguka mtoni New York. Watu 50 walikuwa baada ya ndege yao Continental 3407 kuanguka kwenye nyumba huko Buffalo, New York. Na kumekuwa na ajali kadha za ndege ndogo. Hata hapa Massachusetts ndege ndogo ilianguka na kwa bahati mwanamke aliyekuwa anaiendesha alipona na majeraha madogo.

Wadau, yaani wanasema kuwa kusafiri na ndege ni salama kuliko usafiri wa gari. Lakini mimi kila nikipanda kwenye ndege lazima niombe. Na tukitua salama lazima niseme sala ya shukurani.

Mungu alaze roho ya waliopoteza maisha yao katika hiyo ajali mahala pema mbinguni. Amen.

Kwa habari zaidi someni:

http://www.telegraph.co.uk/news/worldnews/europe/netherlands/4805195/Turkish-Airlines-plane-crashes-at-Schiphol-airport-Amsterdam-at-least-nine-dead.html

http://www.google.com/hostednews/ap/article/ALeqM5g_wBSqw0Ju245UxNtpJZ329K0LJgD96IK4780

Blonde Jokes




Hapa Marekani wanasema kuwa hao wanawake wa kizungu wenye nywele nyeupe (blonde), hawana akili. Ajabu hao wenye nywele nyeupe wanapendelewa kuliko hao wenye nywele nyekundu, brown, na nyeusi. Halafu hao wenye nywele nyeusi wanafanya bleachin ya nywele kusudi wawe blonde. Na siku hizi hata watu weusi wanapenda kuwa na nywele blonde. Hebu someni utani kuhusu blondes.

***************************************************************
Two blondes living in Oklahoma were sitting on a bench talking, and one blonde says to the other, 'Which do you think is farther away.... Florida or the moon?' The other blonde turns and says 'Helloooooooooo, can you see Florida ?????'


CAR TROUBLE

A blonde pushes her BMW into a gas station. She tells the mechanic it died. After he works on it for a few minutes, it is idling smoothly.
She says, 'What's the story?'
He replies, 'Just crap in the carburetor'
She asks, 'How often do I have to do that?'

SPEEDING TICKET

A police officer stops a blonde for speeding and asks her very nicely if he could see her license.
She replied in a huff, 'I wish you guys would get your act together. Just yesterday you take away my license and then today you expect me to show it to you!'

RIVER WALK

There's this blonde out for a walk. She comes to a river and sees another blonde on the opposite bank 'Yoo-hoo!' she shouts, 'How can I get to the other side?'
The second blonde looks up the river then down the river and shouts back, 'You ARE on the other side.'

AT THE DOCTOR'S OFFICE

A gorgeous young redhead goes into the doctor's office and said that her body hurt wherever she touched it.
'Impossible!' says the doctor. 'Show me.'
The redhead took her finger, pushed on her left shoulder and screamed, then she pushed her elbow and screamed even more. She pushed her knee and screamed; likewise she pushed her ankle and screamed. Everywhere she touched made her scream.
The doctor said, 'You're not really a redhead, are you?
'Well, no' she said, 'I'm actually a blonde.'
'I thought so,' the doctor said, 'Your finger is broken.'

KNITTING

A highway patrolman pulled alongside a speeding car on the freeway. Glancing at the car, he was astounded to see that the blonde behind the wheel was knitting!
Realizing that she was oblivious to his flashing lights and siren, the trooper cranked down his window, turned on his bullhorn and yelled, 'PULL OVER!'
'NO!' the blonde yelled back, 'IT'S A SCARF!'

BLONDE ON THE SUN

A Russian, an American, and a Blonde were talking one day.
The Russian said, 'We were the first in space!'
The American said, 'We were the first on the moon!'
The Blonde said, 'So what? We're going to be the first on the sun!' The Russian and the American looked at each other and shook their heads.
'You can't land on the sun, you idiot! You'll burn up!' said the Russian.
To which the Blonde replied, 'We're not stupid, you know. We're going at night!'

IN A VACUUM

A blonde was playing Trivial Pursuit one night.. It was her turn. She rolled the dice and she landed on Science & Nature. Her question was, 'If you are in a vacuum and someone calls your name, can you hear it?' She thought for a time and then asked, 'Is it on or off?'

FINALLY, THE BLONDE JOKE TO END ALL BLONDE JOKES!

A girl was visiting her blonde friend, who had acquired two new dogs, and asked her what their names were. The blonde responded by saying that one was named Rolex and one was named Timex. Her friend said, 'Whoever heard of someone naming dogs like that?' 'HELLLOOOOOOO......,' answered the blonde. 'They're watch dogs'!

Tuesday, February 24, 2009

Mzee Abdullah Riyami Afariki Dunia


Pole sana Khadija na wanafamilia. Nitamkumbuka Mzee Riyami kwa busara yake na mapenzi yake ya fani ya uandishi wa habari.

Mungu amlaze mahala pema mbinguni. Amen.


***************************

Picha na Maelezo ya chini kutoka Michuzi Blog:

Waombolezaji wakiwasili kwenye makaburi ya kisutu jioni hii na mwili wa Mzee Abdullah Ahmed Riyami aliyefariki mchana kwa kusumbuliwa na maralia kali na upungufu wa damu. Mzee Riyami, ambaye amefariki akiwa na umri wa miaka 87, alikuwa mkurugenzi wa mwanzo wa Idara ya habari ya Tanganyika, baada ya kupigana katika vita ya pili ya dunia. pia alikuwa mhazini wa chama cha waandishi wa habari (TAJA). Amecha watoto 10, wajukuu 18 naa vilembwe 10.

Hater - A Poem by Maya Angelou


Hii poem/shairi imetungwa na mtunzi maarufu Maya Angelou. Mjue kuwa hata waMarekani weusi wanatatizo kubwa ya chuki na wivu. Msidhani hiyo tatizo iko Afrika tu!

***********************************************************************

A hater is someone who is jealous and envious and spends all
their time trying to make you look small so they can look tall.
They are very negative people to say the least. Nothing is ever
good enough! When you make your mark, you will always attract some
haters…That’s why you have to be careful with whom you share your
blessings and your dreams, because some folk can’t handle seeing you
blessed…

It’s dangerous to be like somebody else…

If God wanted you to be like somebody else, He would have given
you what He gave them! Right? You never know what people have gone
through to get what they have.

The problem I have with haters is that they see my glory, but
they don’t know my story… If the grass looks greener on the other side
of the fence, you can rest assured that the water bill is higher there
too!

We’ve all got some haters among us! People envy you because you can:

Have a relationship with God
Light up a room when you walk in
Start your own business
Tell a man / woman to hit the curb (if he / she isn’t about the right thing)
Raise your children without both parents being in the home

Haters can’t stand to see you happy, Haters will never want to
see you succeed, Haters never want you to get the victory, most of our
haters are people who are supposed to be on our side. How do you handle
your undercover haters?

You can handle these haters by:

1. Knowing who you are & who your true friends are *(VERY IMPORTANT!!)
2. Having a purpose to your life? Purpose does not mean having a job.
You can have a job and still be unfulfilled. A purpose is having
a clear sense of what God has called you to be. Your purpose is not
defined by what others think about you.
3. By remembering what you have is by divine prerogative and not
human manipulation. Fulfill your dreams!

You only have one life to live…when it’s your time to leave this earth,
you ‘want’ to be able to say, ‘I’ve lived my life and fulfilled
‘my’ dreams,… Now I’m ready to go HOME! When God gives you favor, you can
tell your haters, Don’t look at me…Look at Who is in charge of me…’

Maya Angelou

http://simplybold.wordpress.com/2008/09/18/a-hater-by-maya-angelous

Monday, February 23, 2009

Mkutano Dallas


Jumuia ya Watanzania Dallas
Ndugu Wajumuia,

Kwa niaba ya mwenyekiti wa muda ndugu Simon Nkanda, napenda kuchukua fursa hii kuwakumbusha kuwepo kwa mkutano mkuu utakaofanyika Jumamosi ya tarehe 28, Februari 2009, kwenye ukumbi wa 12727 Hillcrest Dallas TX 75230. Mkutano huu utaanza saa kumi na moja jioni mpaka saa nne usiku. Tukio hili kubwa na la kihistoria lina nia na madhumuni ya kuimarisha jumuia ya Watanzania waishio jijini Dallas na vitongoji vyake. Katika harakati zake za kuunda jumuia hii mwenyekiti, katibu, na viongozi wa kamati mbalimbali wa muda walichaguliwa. Vilevile hatua nyingine ya kihistoria iliyochukuliwa ni kuundwa kwa katiba ambayo jumuia hii itafuata mwenendo, taratibu na muelekeo wa kimaendeleo. Mkutano huu utachukua fursa ya kutambulisha jumuia ya Watanzania hapa Dallas na vitongoji vyake umuhimu wa kuwa na amani, upendo, ushirikiano, umoja na kufuata tararatibu ambazo zitaimarisha jumuia hii. Katika mkutano huu, mwenyekiti, katibu, na viongozi wa kamati mbalimbali watatambulishwa. Vile vile katika jitihada za kuimarisha jumuia hii, hatua zimechukuliwa za kusajili jumuia hii, kuanzishwa mfuko wa dharura, kuanzishwa mtandao mpya, kutumia njia ya teknohama ili kuimarisha mawasiliano na kuutaarifu ubalozi wa Tanzania hapa Marekani tukio hili la kihistoria. Kiongozi wa ubalozi wa Tanzania huko Washington D.C. , Dr Mkama atahudhuria mkutano huu. Kijiweni restaurant wanafadhili mkutano huu na watatoa huduma ya chakula.. Kutakuwa na wageni kuoma miji mingine hapa Marekani ambao watahudhuria mkutano huu. Tunaomba Watanzania wote mliopo Dallas na vitongoji vyake mjitokeze kwa wingi ili tukamilishe jitihada hizi. Tukumbuke tena, “Our real values are expressed in our actions, in what we do and how we do it”.

Kwa maelezo zaidi tunaomba muwasiliane na:

Ndugu Simon Nkanda Ndugu Abdul Amiri
Phone: 469-585-8476 Phone: 214-535-6329
(Mwenyekiti wa muda) ( Katibu wa muda)

Academy Award Night

(Kutoka kushoto - Julia, Mimi, Janine, Sonya, Jacqui)

Jana nilienda kusherekea tuzo za Oscars, Academy Awards, na actors wenzangu wa Boston. Sherehe iliandaliwa na Casting Director wa Boston, Jodi Purdy Quinlan. Ilifanyika Mini Bar katika Copley Plaza Hotel hapa Boston.(picha ya chini -Kutoka kushoto, John A., Julia, Donna, Janine, mimi, John D.)

Hivi waSpanish wameanza kutapeli pia?

I am just dropping by on this kinkos store to email you and let you know
that I have just sent the payment via Western Union in your name as I do
not have your account details correctly.

I also want you to have the payment information below:

Money Transfer Control Number (MTCN): 947-281-7619
Amount Sent: $187,000 USD
Text Question: Favourite Colour?
Answer: Gold


You can go to any Western Union location right now and pick up the cash
quick. I hope that you have a Western Union card / Promo code? You will
need this to send or claim amount above $12,000 USD from any Western Union
agent location.
My company will be sending my team to Chile this week.

I am already on my way to join my team in completing the unfinished bridge
construction project in Chile. We may leave town tomorrow and I couldn't
go without dropping the payment information with you. We may spend 2 to 3
months there before the job would be completely finished. Remember that
if you do not claim the money before 9 days, they will call back the money
to my card. And if you do not have the Western Union Promo/Card, you
cannot pick up the cash. I may not be around to reply any of your emails
now, but I will talk to you as soon as I return.

If you do not have a Western Union Promo Code, you have to contact the
western union agent details below so that they will process and create a
Western Union card/Promo Card for you immediately and also send you a copy
of the voucher of the payment that I made upon request, via email.

Contact the office below for your Western Union card:
Contact Person: Thomas Green
Email: tg-western-union@live.com

Send the below details to him

Your Full Name:
MTCN number: (as above)
Telephone:
Address: (including state and zip code)

As soon as the office gets the above information, they will use the
credentials to create your Western Union Promo code right away without any
delay if you do not have the promo code. Note that you will have to
purchase the Western Union Promo code. That is all to it. I hope to talk
to you as soon as we are back on the errand or call it project.

Clause M. Halle Jr.

Saturday, February 21, 2009

MNigeria ajaribu kutapeli Citibank

Huyo MNigeria karibu aibe pesa za benki kuu ya Eithopia.

*****************************************************************

NEW YORK (AP) -- Prosecutors have accused a Nigerian man of trying to swindle nearly $27 million from an account in New York held by Ethiopia's central bank.

The U.S. Attorney's office in New York says Paul Gabriel Amos pleaded not guilty Friday to conspiracy to commit bank and wire fraud.

The government says the 37-year-old man sent fake documents to a Citibank office in New York where the National Bank of Ethiopia kept funds. The documents claimed to authorize transfers to accounts around the world controlled by Amos and coconspirators.

A complaint signed by FBI agent Bryan Trebelhorn said the fraud was discovered when the overseas banks returned funds to Citibank.
A court-appointed attorney said Amos was in plea discussions.

Friday, February 20, 2009

Weave yaokoa Maisha ya Mwanamke Huko Kansas City!

Wadau, kumbe hizi weave za nywele za akina mama zina faida zake! Huko Kansas City, Missouri mwanamke alipigwa risasi kichwani na boyfriend wake. Huyo jamaa alikuwa na hasira kwa vile walikuwa wameachana hivi karibuni!

Bado sijajua jina la huyo mwanamke ila ana miaka 20. Alienda supermarket na huyo jamaa kamfuata huko na kumpiga risasi kichwani. Kwa bahati risasi haikupenya kichwani shauri ya kukumbana na weave!!!! DUH! Ila dada mwenyewe anasema alisikia joto la risasi. Anasema alitumia hela nyingi kuweka hiyo weave kichwani bora imekuwa na faida kwake! Polisi walivyokuja walikuta risasi imenasa ndani ya weave.

Wazungu wamenichekesha kwenye taarifa ya habari leo. Wanauliza hiyo weave ni nini na inatengenezwa na nini! Je, inatumia gundi au chuma?

Kwa habari zaidi na kuona kideo, bofya chini:

Maiti Yakutwa Gesti Tabata!

Nadhani huyo jamaa alikuwa 'mule' (mtu anayesafirisha madawa ya kulevya). Kipaketi kilimpasukia tumboni. Rest in Peace.

********************************************************

Kutoka Lukwangule Blog:

Maiti iliyokutwa nyumba ya kulala wageni ya Big Brother iliyopo Tabata, Dar es salaam na fedha kibao za Marekani, Brazil, Kenya na Tanzania ilikuwa na kete 57 ya dawa za kulevya.

Kamanda wa Polisi kanda Maalumu, Suleman Kova aliwaambiawaandishi wa habari leo kuwa mtu huyo ambaye anasadikiwa amekufa kutokana na madhara ya dawa hizo.

Mtu huyo ambaye alijiandikisha kwa jina la Haji Hamis katika gesti hiyo alikuwa na hati ya kusafiria yenye jina la JordanBenedict (33).Inaaminika kuwa mtu huyo ni mfanyabiashara wa mitumba na mkazi wa Kijitonyama.

Maiti hiyo ilipatikana jana baada ya wenye gesti kuwa na mashaka baada ya mgeni wao kutotoka tangu ameingia chumbani mwake na kuwaita polisi.Kova alisema maiti huyo alikutwa amepiga magoti na kuegemea kitanda.

Chumbani kulikuwapo na chupa ya plastiki ya maji, hati ya kusafiria, dawa paketi tatu aina ya dawa za kuongeza nguvu baada ya kuharisha sana na pochi iliyokuwa na fedha za Brazil 2000, Kenya 2000, dola za Marekani 27,000 pamoja na Sh za kitanzania 150,000.