Wednesday, October 31, 2007

Mjue Msanii wa Vichekesho Bongo Kingwendu

Tanzanian Comedian Kingwendu Kingwendulile




Kabla ya Ze Comedy kulikuwa na Kingwendu aka. Kingwendu Kingwendulile (pichani). Yeye ni mchekshaji wa siku nyingi huko Tanzania. Anavyoongea inachekesha pia. Fani la uchekeshaji kinshamiri huko Bongo siku hizi. Watu wanauliza mbona hawamwoni Kingwendu zaidi?

Nimekuta clipu kadha kwenye youtube. Yeye Kingwendu ndiye star!

YOU TUBE CLIP 1

YOU TUBE CLIP 2

YOU TUBE CLIP 3

Kazi nzuri! Na kucheka nimecheka hasa!


Huyo Polisi Vipi?




Wema wa Denzel Washington





Hivi karibuni, mcheza sinema maarufu wa hapa Marekani, Denzel Washington na familya yake walitembelea Brook Army Medical Center, mjini San Antonio, Texas (BAMC). Hiyo hospitali ni ya jeshi na inahudumia hasa wagonjwa walioungua moto. Wengi wameumia katika vita vya Iraq na wamesafirishwa kutoka Ujerumani.

Kuna nyumba kadhaa za familia za wagonjwa kukaa wakiwa wamefika kuangalia wagonjwa wao.

Mara nyingi zinakuwa zimejaa. Familia wanakaa pale kwa gharama ndogo au bila malipo kutokana na uwezo wao. Ni bei rahisi kuliko kufikia hospitalini.

Denzel aliliuliza bei ya kujenga nyumba moja ni bei gani. Aliambiwa. Alishangaza wanajeshi alipotoa andika hundi enye pesa za kutosha za kujenga nyumba moja.

Sasa watu wanashangaa. Kwa nini akina Britney Spears, Madonna, Robert Downey Jr. , Tom Curise, wakifanya vituko wanatolewa ukurasa wa kwanza wa magezeti. Denzel akitenda wema wako kimya!

Wanaume wanavyotusema sisi Wanawake!


Nimepata hii kwa e-mail:


CHAGGA WOMEN

First Date: You get to buy her Amarula (or Redds), mbuzi choma and dance the whole night. You have to buy her credit, to organize for the second date.

Second Date: You get to buy her and her girlfriends Amarula (or Redds), mbuzi choma and dance to the whole night. You exchange your expensive phone with her nokia. Third Date: You get to pay her rent. Tenth Date: She tells you she is engaged and you are a kyasaka

ZIGUA/ DIGO WOMEN

First date: She wants your home address

Second date: She comes home for the date with her brother (who is looking for a job)

Third date: She ends at the door, her mother is waiting

Fourth date: You have sex and she tells you she is pregnant and want you to take her and her baby

WAHAYA WOMEN

First Date: You both get blind drunk as you dance to Saida Karoli and later have sex.

Second Date: You both get blind drunk as you dance to Saida Karoli and later have sex.

20th Anniversary: You both get blind drunk as you dance to Saida Karoli and later have sex.


SUKUMA WOMEN

First Date: You take her to a movie and an expensive restaurant.

Second Date: You meet her parents and her Mom makes ugali and chicken.

Third Date: You have sex, she wants to marry you and insists on a 3-carat ring.

4th Anniversary: You already have 3 kids together and hate the thought of having sex.

5th Anniversary: You find yourself a girlfriend.


HEHE WOMEN

First Date: You buy her an expensive dinner, get drunk on Guinness, and have sex in the back of your car.

Second Date: She's pregnant.

Third Date: She moves in. One week later, her two sisters, her brother, all of their kids, her two cousins, her sister's boyfriend and his three kids move in ... and you get to eat rice and beans for the rest of your life in your home that used to be nice before you met her .


ZARAMO WOMEN

First date: You get to buy her dinner, but you realize nothing is going to happen.

Second date: You wait for her in the same restaurant but she gets lost on the way.

Third date: She does not even remember to pick your calls.


NYAKYUSA WOMEN

First date: After a date of drinking several bottles of Fanta, you get to kiss her goodnight.

Second date: You get to grope all over and make out.

Third date: You get to have sex, but only in the missionary position.


ZANZIBARI WOMEN

First Date: You get dynamite head.

Second Date: You get more great head.

Third Date: You tell her you'll marry her and never get head again.


MAASAI WOMEN

First date: You get to buy her an expensive dinner, but nothing happens.

Second date: You buy her an even more expensive dinner. Nothing happens again.

Third date: You don't even get to the third date and you already realized nothing is going to happen.


MAKONDE WOMEN

First date: Meet her parents.

Second date: Set the date of the wedding.

Third date: Wedding night and you get to ask her, her name


PARE WOMEN

First date: She wants sex, no food or drink

Second date: She wants more sex

Third date: She only wants chuma mboga

Tuesday, October 30, 2007

Wazungu wakamatwa Chad wakijaribu kutorosha watoto 100!




Kuna kundi la wazungu wamekamatwa nchini Chad wakijaribu kutorosha watoto zaidi ya mia moja. WaChad wanadai kuwa hao watoto ni raia wa Chad. Hao wazungu wanasema ni yatima kutoka Sudan na walikuwa wanapelekwa Ufaransa kukaa na familia kadhaa kule.

Kuna kundi la ufaransa inaitwa Zoe's Ark, ndo ilikuwa imeleta ndege ya kusafirisha hao watoto.

Sasa hao wazungu wanaweza kufungwa kwenye gereza la Chad kwa miaka 20 na kufanyishwa kazi ngumu. Pia wameshika raia wawili wa Chad.

Baadhi ya hao watoto walidai kuwa walitekwa na hao wazungu. Walipewa pipi na biskuti na walijikuta wanatoroshwa.

Inasemekana familia kadhaa huko Ufaransa walilipa kati ya Euro 2,800 hadi 6,000 kumpata mtoto yatima kutoka Sudan.

Kwa habari zaidi someni:




Video

Oprah aomba msamaha!


Mnajua ile shule ya fahari ya wasichana ya Oprah huko Afrika Kusini? Kumbe baadhi ya wasichana wamebakwa na kufanyiwa vibaya na mfanyakazi wa kike huko!

Oprah amekuwa msiri na 'details' za matukio. Huyo mama aliyetenda mabaya amefukuzwa kazi na anachunguzwa na polisi wa Afrika Kusini.

Navyosikia sheria za hiyo shule ni kali sitashangaa nikisikikia kuwa wasichana wa shule hiyo wameshikwa na ugonjwa wa 'HYSTERIA'.


***********************************************************************************

Sexual abuse claims at Oprah's school

October 30, 2007

US talkshow queen Oprah Winfrey has tearfully begged for forgiveness after a staff member at a girls' school she funds in South Africa was accused of sexual abuse.

Winfrey rushed to the Leadership Academy for Girls, near Johannesburg, after the abuse claims surfaced.

She met with parents and assured them she would do everything possible to ensure prosecution, The Independent newspaper reported.

"I've disappointed you. I'm so sorry. I'm so sorry," Winfrey told the parents who attended a meeting in a packed marquee.

One of the matrons who oversees the dormitories has been accused of abuse.
Reports said the staffer grabbed one girl by the throat and threw her against a wall. The woman, who has not been named, has also been accused of sexually fondling at least one pupil.
The claims came after a student fled the school saying the situation had become unbearable. Winfrey has sent the accused woman on leave, along with the school's principal, identified only as Dr Mzimane, and one other staffer, the Independent said.

The alleged victims have accused Dr Mzimane of failing to act after students complained of abuse.

Police and special US investigators have been called in.

Winfrey, reportedly in tears, told the meeting: "I trusted her (Dr Mzimane). When I appointed her, I thought she was passionate about the children of Africa. But I've been disappointed."
One father responded by telling Winfrey it was not her fault.

Winfrey spent millions to build the school after former South African president Nelson Mandela asked her to become involved in education programs.

Kwa habari zaidi someni:



Mjue Msanii Mkongwe wa Bongo - Mzee Kipara


Msanii wa siku nyingi Tanzania, Fundi Saidi aka. Mzee Kipara yumo kwenye sinema ya Bongoland II.
Kwa habari zake zaidi Bofya Hapa!

Monday, October 29, 2007

Steven Kanumba aja juu katika sinema za Bongo









Is Steven Kanumba the Hardest working actor in Tanzania?

Kwa kweli nampongeza Steven Kanumba kwa sinema zake Tanzania. Nimeona website enye sinema zake kama 10 hivi. Kwa habari zaidi nendeni:

Sijawahi kuona sinema aliyoacti Steven hivyo siwezi ku-comment juu yake. Kama mmewahi kuona hizi sinema karibuni mtoe maoni.
Kusoma mahojiano na Bwana Kanumba someni hapa:

Mwanamke Mwafrika ajiua Luxembourg kisa Ubaguzi





Marehemu Maggie Delvaux-Mufu, aliamua kujitoa roho mbele za umati wa watu huko Luxembourg baada ya kuchoka na ubaguzi uliokumba yeye na familia yake huko. Kabla ya kujimwagia petroli na kuwasha kibiriti alipiga simu kwenye vyombo vya habari na kuwaelezea nia yake. Bila shaka wengine walimcheka. Lakini polisi walitumwa kumtafuta. Aliamua kujiwasha kabla ya kufika sehemu alipowambia. Kisa alisema kachoka ubaguzi. Yeye na mume wake walikuwa wamenunua gereji lakini walishindwa kuisajili kutokana na ubaguzi wa rangi. Hali yao kifedha ilikuwa duni.
Alikuwa ameambatana na mume wake. Nashangaa huyo mume alikubali muke wake afanye hivyo. Kwa nini yeye hakujichoma moto? Si ajabu kashaoa mwanamke mwingine!
Baada ya tukio alitembelea hospitali na moja wa familia ya wafalme Grand Duchess.
Wazungu huko Luxembourg walijiuliza, hivi kuna ubaguzi kweli Luxembourg haiwezekani. Tukio la huyo mama umesaidia kuonyesha dunia kuwa UBAGUZI UPO!
Marehemu Maggie alijiua Agosti mwaka 2004. Ajabu hivi karibuni ndo habari za tukio zimeanza kuongelea tena na kusambaa duniani baada ya kuchapishwa kwenye gazeti moja huko New York ya 'Media Take-Out" Sijui walikosa cha kuandika Walibadilisha tarehe ya tukio na kusema ilitokea 2007 badala ya 2004.
********************************************************************************

Belgians shoppers in the middle of Place d’Armes, Luxembourg City were witness to the most horrendous sight of a woman caught on fire by her own doing in protest of perceived racism against her. The 44 year old Belgian of Congolese descent is now in Bon Secours hospital in Metz fighting for her life. The Grand Duchess Maria Teresa visited her there.What could have driven this woman to take this desperate act to be heard and seen? Is it that the pain of exclusion, of racial discrimination could be more painful for her that hot fire burning her skin?
Maggie Delvaux-Mufu, a mother of three in her forties, and her husband had been facing financial difficulties, alerted several national newspapers late on Tuesday morning last week that she would be burning herself alive on place des Martyrs at 12.45 am, before setting out accompanied by her husband to walk through the centre of town to her macabre rendezvous.
The police were alerted and officers were deployed to the Rousegärtchen. But the woman changed her plan when she came across a group of journalists gathered to cover an event organized by the ‘Movement écologique’ on Place d’Armes, opposite the Cercle municipal. She soaked herself in petrol before confronting the members of the press, announcing that she was about to sacrifice her life to protest against racism. Moments later, she struck a match, turning herself into a human torch in front of hundreds of people.
The 42-year-old Belgian citizen and her husband had been facing financial difficulties. They had recently indebted themselves by buying a Citroën garage in Oberwampach, before realizing they were missing the documents that would allow them to set up a business.
Delvaux-Mufu wrote a letter to Le Jeudi recounting her story of bureaucratic difficulties and economic despair. “I’m against all forms of violence, but day after day, my family and I have to endure moral violence, discrimination, insults and much more from Mr Juncker’s administration”, she said in the letter published last week.

Boston Red Sox washinda Baseball World Series tena!



Boston Red Sox wameshinda World Series kwa mara ya pili katika miaka minne. Kabla ya mwaka 2004 walikuwa hawajapata ushindi kwa miaka 86. Watu walikuwa wanasema eti ni laana za Babe Ruth aka. Curse of the Bambino.
Babe Ruth aliwahi kucheza kwenye timu ya Red Sox lakini mwaka 1918 aliuzwa ghafla kwa timu ya New York Yankees. Watu walidai alilaani timu ya Red Sox na huenda ni kweli aliwalaani maana hawakupata ushindi wa World Series kwa miaka 86. Kila mwaka ilikuwa vichekesho maana watu walikuwa na vituko mpaka wachawi wakawa wanaenda Fenway Park kutambika!
Haya wameshinda tena. Nawapongeza ila naomba wa punguze bei ya tiketi za game zao Fenway kusudi watu wa kawaida waweze kwenda kushabiki. Tiketi za Red Sox ni za ghali kuliko timu zote za Baseball Marekani.
Nashinwdwa kuelewa kwa nini wakishinda lazima wajichafuana kwa kumwagiana chupa za champagne? Pia kwa nini ni lazima washibiki wapindue magari na kufanya uhalifu? Kuna maajabu.
ATTENTION RED SOX YOUR TICKETS ARE TOO EXPENSIVE AND YOU ONLY CATER FOR THE YUPPIES! NEXT TIME IT WON'T BE CURSE OF THE BAMBINO BUT CURSE OF THE AVERAGE MAN!

Saturday, October 27, 2007

Madereva waongea kuhusu ajali za Viongozi Bongo

Ukiendeshwa na dereva unaweka maisha yako mikononi mwake.

Miaka ya 80' kuna Prof wa Chuo Kikuu alikuwa kwenye ziara mikoani kukagua wanafunzi wake. Huyo Prof. alikuwa na briefcase imejaa malaki ya pesa. Ile gari land rover ilipinduka, Prof aliumia vibaya na pesa zile potea. Hakuna hatua iliyochukuliwa dhidi ya yule dereva. Sasa kuna siku nilikuwa kwenye warsha sehemu za Kurasini. Kulikuwa na kundi la madereva wa wakubwa nje. Nilikuwa karibu nao. Nilimsikia yule dereva aliyekuwa na yule Prof. akitamba mbele ya madereva wengine jinsi alivyopindua ile gari na kuiba zile pesa! Yule dereva naamini alikuwa na matatizo ya akili maana hakuna mwenzake aliyesema kitu bali walimtazama kama yeye ni mwendawazimu.

Kweli madereva wa chunguzwe kabla ya kupewa kazi ya kuendesha mtu.

******************************************************************************

From Gazeti la Mwananchi:

Madereva wajitetea juu ya za ajali za viongozi

Frederick Katulanda, Mwanza

WAKATI taifa likiomboleza kifo cha Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Salome Mbatia aliyefarika katika ajali juzi mkoani Iringa, baadhi ya madreva wameeleza kuwa ajali nyingi zimekuwa zikiwakumba viongozi wa serikali zinatokana na baadhi yao kutoawajali madreva wao.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana mjini hpa, baadhi ya madreva hao walisema ajali nyingi zimekuwa zikiwakumba viongozi kutokana na baadhi yao kuwafanyaisha kazi madreva wao wakiwa na njaa, usingizi, mawazo na hata matatizo ya kifamilia.

Akielezea ajali hizo dreva wa CCM mkoa Adamu Sudi, alisema kuwa viongozi wamekuwa wakiwatumia madreva bila ya kuwajali jambo ambalo ni hatari kwa usalama wao kwa vile dreva kuendesha akiwa na njaa inaweza kusababishia ajali na hata kupoteza maisha.

"Mfano tatizo linaloweza kusabaisha ajali kwa viongozi ukiondoa uzembe wa madreva, ni viongozi kutowajali madreva wao, huwezi kuendeshwa na dreva mwenye njaa, ama unamfanyika kazi hadi usiku wa manane na kisha untaka alfajili akuendeshe, anahitaji kupumzika," alisema.

Dreva James Lisalaka alisema huku akitoa mfano kuwa baadhi ya viongozi wamekuwa wakiwaangali madreva wao kama watu wasio na maana wakati wamekuwa wakilinda maisha yao katika safari na hivyo kusema kuwa wanapaswa kuwaangali na kujali afya zao.

"Madreva wanapokwenda safari baadhi ya viongozi wamekuwa wakishindwa kuwalipa hata posho, hatua ambayo imekuwa ikiwafanya baadhi yao kuishi katika mazingira magumu, wengine kulala katika magari, kushinda njaa," alisema.

Wamesema kuwa baadhi ya viongozi pia wamekuwa wakichukua madreva wasio na uzoefu mkubwa kutokana na kuwalipa gharama kubwa na matokeo yake kusababisha ajali.

Alifungwa miaka kumi gerezani - Kisa Ngono. Sasa ameachiwa huru.


Kijana Genarlow Wilson (21) ameachiwa huru baada ya kukaa gerezani mkoani Georgia kwa miaka miwili. Wilson alipewa kifungo cha miaka 10 ...kisa akiwa na miaka 17, msichana wa miaka 15 alikutwa anamnyonya ume wake!

Kwa kweli naona ni vizuri hao vijana wakifanya ngono wenyewe kwa wenyewe kulikoni huyo binti wa miaka 15 angekutwa na jibaba wa miaka 40! Lakini sheria za kule kusini mwa Marekani ni kali hasa mahakama wakiamua kuzitekeleza.

Kesi ya Wilson ilikuwa machoni mwa waMarekani toka itokeee. Na sasa Georgia wamebadilisha sheria. Kama vijana wamepishana umri hadi miaka minne hakuna kosa. Yaani tuseme moja awe na miaka 20 mwingine miaka 16.

Hapa Marekani lazima watu wawe waangalifu na sheria. Vijana wa miaka 18 wanaweza kufungwa wakikutwa wanafanya ngono na wasichana chini ya miaka 15 na states zingine hata miaka 16! Pia wanaitwa 'Sex Offender' daima.

Je, Afrika hizo sheria zingekuwepo ingekuwa balaa!

Friday, October 26, 2007

Heshima za Mwisho - Mheshimiwa Salome Mbatia



Rais Mstaafu Benjamin Mkapa na Mke wake wakitoa heshima za mwisho.
Baadhi ya waombolezaji.

Picha zote kwa hisani ya Michuzi Blog

Leo watu walitoa heshima za mwisho nyumbani kwa marehemu Mheshimiwa Salome Mbatia, huko Oyster Bay. Marehemu atazikwa kesho kwao Kirua, Moshi.

Thursday, October 25, 2007

Mheshimiwa Salome Mbatia afariki dunia katika ajali ya gari





Picha za ajali kwa hisani ya Mheshimiwa Zitto Kabwe

Picha ya Mh. Salome Mbatia kwa hisani ya Food For Thought blog:

Nimepokea habari za kifo cha aliyekuwa Naibu Waziri wa Maendelo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Mheshimiwa Salome Joseph Mbatia (55) kwa huzuni mno. Dada Salome alifariki jana jioni huko Kibena mkoani Iringa kwa ajali baada ya gari alilokuwa akisafiria kugongana uso kwa uso na lori aina ya Fuso. Madereva wote wawili pia walipoteza maisha.

Dada Salome alikuwa Iringa, kwenye ziara maalum ya kuelimisha akina mama juu ya mila na desturi mbovu zinazochangia vifo vya akina mama na watoto.

Pamoja na majonzi niliyonayo kwa kweli nimekasirika mno. Hayo magari yalikuwa yanaenda mwendo gani? Je, dereva wa gari alikuwa amekunywa pombe au kutumia madawa ya kulevya. Najua Tanzania kuna tabia, oh kafa hatarudi hata ukifanyeje lakini....

Naomba wana usalama barabarani na pia serikali wachunguze ajali hii!
Akina mama wote wa Tanzania tumepata hasara na kifo cha Dada Salome. Mungu awape familia yake hasa watoto wake na mume wake nguvu katika kipindi hiki kigumu.
Mungu ailaze roho yake mahali pema mbinguni. AMEN.
******************************************************************************
Ajali ya Mhe. Mbatia Sumaye, Zitto chupuchupu
2007-10-25 Na Emmanuel Lengwa, Jijini

Waziri Mkuu mstaafu Mheshimiwa Fredric Sumaye, Mbunge Machachari wa Kigoma Kaskazini Mheshimiwa Zitto Kabwe na Naibu Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mhe. David Mathayo ni miongoni mwa watu walioponea chupuchupu kupatwa na ajali iliyotokea jana jioni na kusababisha kifo cha Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto Marehemu Salome Joseph Mbatia.
Bw. Sumaye, Zitto na Mathayo walikuwa kwenye magari tofauti wakiongozana katika barabara moja na gari la Mhe. Mbatia lililopata ajali, bila wao kufahamiana. Kwa mujibu wa watu walioshuhudia ajali hiyo wanasema lori aina ya Fuso liligongana uso kwa uso na gari la Mhe. Mbatia, ndilo lililopoteza mwelekeo na kusababisha ajali hiyo.
Kwa vile magari yaliyokuwa yamewabeba waheshimiwa hao yalikuwa yakiongozana, basi kama lori hilo lisingegonga gari la Mheshimiwa Mbatia huwenda lingeyavaa magari ya waheshimiwa wengine. Akizungumza na Alasiri kwa njia ya Simu leo asubuhi, Mheshiwa Zitto amesema gari lililokuwa limembeba marehemu Salome Mbatia lilikuwa mbele yake wakiongozana barabarani, lakini hakujua kuwa aliyekuwamo alikuwa ni Naibu Waziri Salome Mbatia.
`Gari hilo lilikuwa mbele yangu, nililiona lakini kwa vile marehemu alitumia gai binafsi, sikujua kuwa aliyekuwemo alikuwa ni Mhe. Mbatia,` akasema Zitto.
Akasema Mheshimiwa Zitto kuwa yeye alifika ndani ya muda wa dakika tano baada ya gari la Mheshimiwa Mbatia kupata ajali, lakini kwa jinsi gari hilo lilivyokuwa limepata ajali hakuwe . Zitto amesema muda mfupi baadaye wakati wakiendelea kuwatoa majeruhi kwenye magari,likafika gari lingine alilokuwemo Bw. Mathayo, ambaye alimtambua moja kwa moja Naibu Waziri Salome Mbatia, kwa vile alikuwa na taarifa za safari yake hiyo na alilijua gari hilo lililopata ajali. `
Mheshimiwa Mathayo ndiye aliyemtambua Marehemu Mbatia,` akasema. Kwa mujibu wa Bw. Zitto wakati wakiendelea kuiondoa miili ya marehemu kwenye magari, pia likafika gari lingine alilokuwemo Waziri Mkuu Mstaafu, Bw. Fredrick Sumaye ambaye pia aliungana nao katika kusaidia kuitoa miili ya marehemu kwenye magari ambayo yalikuwa yamepondeka vibaya.
Bw. Zitto akasema baada ya kuona ajali hiyo akaamua kukatiza safari yake na gari lake likatumika kuwakimbiza majeruhi wengine hospitalini. Wakati huo huo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa Bw. Advocate Nyombi amesema dereva wa gari aina ya Fuso liligongana na Gari la Naibu Waziri huyo na kusababisha kifo chake amenusurika.
Kamanda Nyombi ameiambia Alasiri kwa njia ya simu leo asubuhi kuwa aliyekufa papo hapo katika ajali hiyo ni Utingo wa Fuso hilo aliyemtaja kwa jina la Castory Kilagwa, 22, ambaye ni ndugu wa mmiliki wa Fuso hilo. Amesema hata hivyo Dereva huyo inadaiwa kuwa alikimbia au aliondolewa haraka eneo la tukio, na hivyo hajulika alipo na Jeshi la Polisi linaendelea kumsaka.
Kamanda Nyombi amesema Polisi imemkamata mmiliki wa Fuso hilo aliyemtaja kwa jina la Jackson Kilagwa ili awaaidie kumpata dereva wake.
`Tunaamini hawezi kumkabidhi mtu mali yake ya thamani kiasi kile bila kujua mahali anapoishi, ndio sababu tunamshikilia mmiliki wa gari hilo ili atusaidie kumpata dereva wake,` akasema Kamanda Nyombi.
Jina dereva wa Mama Mbatia ambaye naye alifariki katika ajali hiyo ni Anaclet Mongella.

Wednesday, October 24, 2007

Nyumba za Matajiri zaungua moto California!


Jamani mnakumbuka Hurricane Katrina. Ile kimbunga iliyoleta balaa mji wa New Orleans na kusambaza watu wake. Wengi waliathirika kule New Orleans walikuwa ni weusi maskini.

Sasa moto mkali unateketeza maeneo ya matajiri huko California. Misaada ya kila aina wamepatiwa mara moja. Hata kwenye shelters zao wanafanyiwa catering na Legal Seafoods na Au Bon Pain, na kulalia magodoro na siyo cots!

Watu wawili wamekufa, zaidi ya 50 wako mahututi hiospitalini na zaidi ya watu nusu milioni wamekimbia! Nyumba kadhaa za ma celebrity zimeungua na pia Hollywood wamesimamisha kupiga filamu na show za TV kwa vile wafanyakazi wengi wameathirika au sehemu walizotaka kupigia zimeathirika.

Ajabu kwa sasa sehemu ziliathirika zaidi kule California ni maeneo ya wapiga kura Republicans!

Kwa habari zaidi someni:

Monday, October 22, 2007

Panda Teksi za Madereva unaowafahamu Bongo

Nimepata hii habari kwa e-mail. Ilitokea usiku wa kuamkia Ijumaa mjini Dar es Salaam.

********************************************************************

Dear all,

Jana I happen to come across a very sad event:

Nilikuwa narudi nyumbani around saa moja jioni kwa kutumia njia ya Chuo Kikuu, kuna njia ya mkato inayopita changanyikeni na kutokea bahama mama. Kuna bonde na daraja na si sehemu salama sana wakati wa usiku.

Nilisimamishwa na dada mmoja aliyeonekana kuchanganyikiwa akiwa ameshika viatu mkononi. Kwa sababu nilikuwa mwenyewe, nilimpita kwanza then nikasimama ili nione kama kuna watu wengine. Yule dada alikuja akiwa analia akasema ameibiwa kila kitu na dereva taxi ambae alimtisha kwa kisu na kumsukuma nje ya gari na dereva kuondoka kwa kasi. Lakini pia, dada huyo alikuwa na mwenzake kwenye gari (mdada pia) ambae alishindwa kutoka na dereva huyo aliondoka nae. Wakina dada hao walikodi taxi hiyo kutokea Msasani wakielekea Ilala.

Nilimsaidia huyo dada hadi Kimara police post na ku-report. Nilimsaidia kufanya mawasiliano na kaka yake na kuwaacha.

Mpaka saa 5 usiku jana walikuwa hawafanikiwa kumpata huyo dada mwingine. Leo asubuhi nimepata habari kuwa, yule dada mwingine alipatikana usiku wa kama saa sita. Alikuwa na hali mbaya sana, kwa maelezo yake..aliingiliwa na watu 9 kimwili. Kesi ipo polisi na kijana mmoja amekamatwa.

This is very sad..sad indeed. Jamani wandugu�.tuwe makini sana na Taxi�

GJ

Tahadari mnaotaka kununua magari ya South Africa


Nimepata hii habari kwa e-mail. Imeandika na Dr. Anthony Masaka.

************************************************************************

Dear all,

Nimeona kwenye taarifa ya habari( ya ITV ya jana usiku) na magazeti jinsi wabongo 'walivyonunua' kesi za wizi wa magari ya south Africa.

Nafikiri sio mbaya kuelezana( kwa wasiofahamu) kamchezo fulani wanakofanya hawa wenzetu wa SA juu ya magari.

Hawa jamaa wa-SA, wanauza magari yao wenyewe kwenye agents(makampuni ya huuzaji na ununuaji magari), ili huwa ni 'deal' kati ya muuzaji(mwenye gari) , mnunuaji(kampuni) , na "corrupt polisi".

Ishu ni gari litauzwa kwa mteja wa nchi ya nje anayenunua gari SA( through kampuni ya uuzaji magari),likishauzwa na kuvuka boarder tu , mwenye gari anaenda polisi ku-report gari limeibiwa!!, anapewa polisi report, gari linatafutwa, insurance yake inamlipa( that means kauza gari mara2!!). au mengine yameibiwa SA,yanabadilishwa namba na rangi na kuvushwa nchi nyingine( Botswana, Zambia,Namibia, Angola etc hata Tanzania).

Kisheria ukinunua gari lolote kabla hujalisajili au kubadilisha Card, lazima upate clearance ya interpol . Kwenye nchi nyingi za Afrika tunatumia CID , wanaweka chasis number kwenye mtandao wa interpool, baada ya 36hours linakuwa cleared.

Nchi kama Botswana na SA huwezi kulipia ushuru hadi clearance ya interpol.

Process hizi huwa zinarukwa na baadhi ya watu au police wanahongwa au uzembe wa polisi kutohakiki gari interpol na kutoa clearance certificate.

Baada ya muda ndio mambo yanaibuka!!, unaambiwa gari liliibiwa miaka kadhaa iliyopita!!! Wakati wewe umenunua kihalali!! Na papers zote unazo!!

Linarudishwa kwa mwenyewe( wa SA), na wewe kununua kesi!! Unaambiwa kama una madai au swali uliza kwa aliyekuuzia, na kwa sasa wewe ni mtuhumiwa hadi ushahidi ukamilike!! Nafikiri ndio yaliyowapata baadhi ya ndugu zetu.

Na ndio maana kuna magari kama Benzi, BMW X5, Pajeros, RAV4 etc nyingi za ki-south ambazo zinauzwa bei nafuu!!,unaweza kupata X5 hata kwa 5mil tzsh , ni kamchezo ka wajanja tu!

Watu wengi wakinunua haya magari(bila kujua)wanakimbilia kwa mawakili ambao uthibitisho wanataka Card ya gari,unalipia, linakuwa lako!! Umeshanunua kesi!!

Take care.

Ishu hii nimepewa na jirani yangu m-SA, ambaye kamchezo haka amekafanya mara2.

Dr.A.A Masaka.


Tamasha la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo

Mambo si ndo hayo!

Namwona classmate wangu wa TSJ, msanii Elangwa Mtahiko hapo kwenye kona akicheza ngoma.

Nawatakia Tamasha njema.

Wasichana wadogo wawili wabakwa hadi kufa!

Jamani dunia inaenda wapi? Nawauliza tena mwanaume anakuwa na nyege kiasi gani mpaka kutaka kumbaka mtoto mdogo ambaye nyeti zake hazijakomaa kumudu tendo! Na hata kama ni mkubwa na hajakubali anaweza kuchanwa uke! Si uwongo! Kateni boro za hao wanaume wahalifu maana hawastahili kuwa nazo! Na wanyongwe hadharani!

Na mtasoma chini, wananchi wenye hasira hawakusubiri mkondo wa sheria na hii kesi!

********************************************************************************
Kutoka Freemedia.com

Wanafunzi wawili wafa kwa kubakwa

na Jumbe Ismailly, Singida

MWANAFUNZI wa darasa la sita katika Shule ya Msingi Mrama, iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Singida na mdogo wake aliyekuwa akisoma shule ya awali katika shule hiyo, wamefariki dunia baada ya kubakwa na kulawitiwa na watu wasiojulikana.

Wanafunzi hao wametajwa kuwa ni Twaiba Athumani (13) anayesoma darasa la sita na Zulfa Athumani (7), aliyekuwa akisoma shule ya awali.

Akizungumzia tukio hilo jana, baba wa watoto hao, Athumani Jumanne, alisema tukio hilo lilitokea juzi, kati ya saa 12 jioni na 2 usiku, umbali wa kilomita takriban mbili kutoka nyumbani kwake, kwenye eneo la shamba la viazi la mkazi mmoja wa kijiji hicho.

Alisema kabla ya tukio hilo watoto hao walitoka nyumbani majira ya saa 10:30 jioni kwenda kisimani kuchota maji kwa ajili ya kufulia nguo na kwamba mpaka inafika saa 2 usiku walikuwa hawajarudi.

Alisema, baada ya kuona hali hiyo waliamua kuwafuatilia, lakini hawakuwaona, hali iliyosababisha kwenda kutoa taarifa kwa mjumbe wa nyumba 10, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa na baadaye Kituo Kidogo cha Polisi Ilongero.

“Mpaka saa mbili asubuhi walikuwa hawajarudi...ilibidi tuwafuatilie hadi kwenye eneo lililokuwa na korongo na ndipo tulipookota kiatu cha tairi cha mtuhumiwa mmoja na tulipoendelea kufuatilia hadi kwenye shamba la viazi ndipo tulipoikuta miili ya marehemu ikiwa imetapakaa vinyesi na damu.

“Tuliweza kutambua viatu vya mmoja wa watuhumiwa baada ya kufuatilia nyayo na tulipofuatilia hadi kwa mmoja wa watuhumiwa, Hamisi Msaghaa, mkazi wa Kijiji cha Mrama tulimkuta akifyatua matofali na kumchukua hadi kituo kidogo cha polisi Ilongero,” alifafanua baba wa watoto hao.

Naye Mwenyekiti wa Kijiji, Issah Swedi, alisema mtuhumiwa Mile aliyetoroka inasemekana alitoka gerezani hivi karibuni baada ya kumaliza kutumikia kifungo kwa makosa ya ubakaji na kwamba amekuwa na uzoefu wa kuishi gerezani kuliko uraiani.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Ilongero, Greace Kishindo, alithibitisha kupokea maiti hizo huku zikiwa zimetapaa damu na vinyesi.
Polisi mkoani Singida wamethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba inamshikilia Msaghaa kwa tuhuma hizo na bado wanamtafuta mtuhumiwa mwingine aliyetambulika kwa jina moja la Mile aliyetoroka baada ya kufanya tukio hilo.

Kwa habari zaidi someni:

http://www.freemedia.co.tz/daima/2007/10/17/habari31.php

********************************************************************************
From Ippmedia.com

Wavamia polisi na kuua mtuhumiwa 2007-10-22 08:47:45

Na Elisante John, PST, Singida

Mamia ya wananchi wenye ghadhabu wamevunja mahabusu ya kituo cha polisi cha Ilongero kilichoko wilayani Singida Vijijini, wakamtoa nje na kumpiga hadi kufa mtuhumiwa wa mauaji ya watoto wawili wa familia moja.

Aliyeuawa usiku wa kuamkia juzi ni Mile Nkindwa (20), mkazi wa Ilongelo wilayani hapo, aliyekuwa ametorokea kijiji jirani baada ya kufanya mauaji. Mtuhumiwa huyo alifikishwa kituoni kwa tuhuma za mauaji ya watoto wawili wa kike kwa kuwabaka, kuwalawiti na kuwanyonga kisha kuwatumbukiza ndani ya korongo na miili yao kugundulika ikiwa imetapakaa kinyesi na damu.

Habari kutoka kituo hicho zilisema Nkindwa baada ya mauaji hayo alitoroka na kujificha katika kijiji cha Mughamu. Hata hivyo, mtuhumiwa mwenzake Hamisi Juma Msaghaa (33) amefikishwa mahakamani mjini Singida kujibu mashtaka ya mauaji.

Akielezea tukio hilo, diwani wa Kata ya Ilongelo, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri wa Wilaya ya Singida, Bw. Ramadhan Samwi, alisema mauaji dhidi ya mtuhumiwa huyo yalifanyika juzi saa 4:00 usiku nje ya kituo hicho. Alisema pamoja na kuwepo askari wa kutosha kutoka Singida mjini waliokwenda kituoni hapo kumchukua, wananchi walivamia kituo hicho kuanzia saa 3:00 usiku na kuwataka askari wamtoe mtuhumiwa aliyehusika na mauaji ya watoto hao.

Bw. Samwi aliongeza kuwa pamoja na askari kugoma kumtoa mtuhumiwa, wananchi walishinikiza atolewe hatua iliyosababisha wapige risasi hewani ili kuwatawanya lakini wananchi waliwazidi nguvu polisi na kuvunja milango na kumburuza nje mtuhumiwa na kumpiga hadi alipokata roho. Aliongeza kuwa wanakijiji hao walimshambulia kwa mawe, marungu, fimbo na kila silaha waliyoiona hadi akaaga dunia.

Akifafanua zaidi, diwani alisema marehemu Mile alikamatwa baada ya baba yake akiongozana na mwenyekiti wa Kijiji cha Itamka Bw. Mamu Mloya, kwenda katika kijiji cha Mughamu ambako mtuhumiwa alijificha kwa jamaa zake baada mauaji hayo. Alieleza kuwa walimnasa na kumfikisha kituo cha polisi cha Ilongelo ambako jioni yake ndipo alipouawa na wananchi hao waliokerwa na mauaji hayo ya kikatili.

Waliokufa katika mkasa huo ni mwanafunzi wa darasa la sita katika Shule ya Msingi Mrama iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Singida pamoja na mdogo wake aliyekuwa akisoma masomo ya awali shuleni hapo. Watoto hao ni Twaiba Athumani (13) na Zulfa Athumani (7).

Watoto hao wa Bw. Athumani Jumanne, walikumbwa na vifo hivyo vya kikatili Jumatatu iliyopita kati ya saa 12:00 jioni na 2:00 usiku katika shamba la viazi la mwanakijiji mmoja, umbali wa kilomita mbili kutoka nyumbani kwao, wakati walipokwenda kisimani kuchota maji.

Hili ni tukio la tatu katika mwezi huu la wananchi kujichukulia sheria mikononi kwa kuvamia vituo walimowekwa watuhumiwa wa mauaji kwa lengo la kuwaua. Mwanzoni mwa mwezi huu, wananchi wa wilaya ya Chato mkoani Kagera walivamia makao makuu ya polisi na kuchoma moto kituo kwa lengo la kumuua mtuhumiwa.

Katika tukio hilo, kulikuwa na uvumi kwamba kuna mwanamke kituoni hapo anashikiliwa na polisi baada ya kukutwa akiwa na ngozi ya binadamu. Hata hivyo, habari za kipolisi zinaonyesha kuwa uvumi huo haukuwa wa kweli. Wiki iliyopita, tukio kama hilo lilijiri mkoani Tanga ambapo watu wasiofahamika walivunja ofisi ya kijiji cha Nkogoi wilayani Lushoto na kumuua mtuhumiwa wa mauaji aliyekuwa amefungiwa ofisini humo.

Mtuhumiwa huyo aliyekuwa akisubiri kupelekwa polisi ni kijana wa miaka 22, Yahaya Omari. Yeye anadaiwa kumuua kwa kumpiga rungu kichwani Muhsin Rashid (15). Marehemu Muhsin alikuwa mwanafunzi wa darasa la sita katika Shule ya Msingi Mavumbi.

Saturday, October 20, 2007

Mark Curry nchini Tanzania

Actor maarufu wa Hollywood, Mark Curry aliyecheza kama Mr. Cooper kwenye sitcom ya miaka ya tisini, "Hanging with Mr. Cooper" alitembelea Tanzania na kufanya maonyesho huko juzi kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee.

Hivi karibuni alichekesha umati wa watazamaji wa show, Fat Actress, stelingi Kirstie Alley, alivyocheza kama mwanaume anayependa wanawake wanene.

Hapo juu ni moja ya picha aliyepiga na washabiki wake wa Bongo wakiwemo rafiki yangu, Michuzi.

Friday, October 19, 2007

Mwimbaji Lucky Dube auwawa Afrika Kusini




Mwimbaji maarufu wa Afrika Kusini, Lucky Dube, ameuwawa kwa kupigwa risasi na majambazi walioteka nyara gari lake jana jioni. Alikuwa anawapeleka watoto wake nyumabni kwa ndugu yake ndipo katekwa nyara na kuuliwa. Binti yake mdogo alikuwemo kwenye gari na alishuhudia tukio.

Lucky Dube alikuwa mwanamuziki wa kwanza kutoka Afrika Kusini kupata mkataba na kampuni maarufu ya muziki hapa Marekani, MOTOWN.
Afrika tume pata hasara katika dunia ya muziki. Lakini jamani ujambazi unazidi Afrika Kusini! Ile sinema ya Tsotsi si uwongo ni picha halisi ya hali ilivyo kule.
Mungu ailaze roho yake mahali pema mbinguni. Amen.
**************************************************************************

S. African Reggae Star Lucky Dube Killed in Attempted Car-Jacking

By Scott Bobb Johannesburg 19 October 2007

South African Reggae star Lucky Dube has been killed in an apparent car-jacking attempt. The 43 year-old musician was shot Thursday night in a suburb south of Johannesburg. Correspondent Scott Bobb reports from our bureau there.

South African police say the renowned Reggae musician was shot by three gunmen as he dropped off his son in the Rosettenville suburb of Johannesburg.

Police spokesperson Lorraine Van Emmerick told national radio that Lucky Dube's daughter also witnessed the shooting.

"He was hijacked. He was able to flee from the scene," said Van Emmerick. "His children were out of the vehicle at the time Mr. Dube was shot. He was declared dead at the scene by the paramedics."

Lucky Dube achieved world fame through music with a social message such as this 2003 song about the ravages of AIDS, called "Number in the Book."

He received some 20 awards during his 25-year career and was the first South African musician to be signed by the Motown recording label in the United States.

Born in 1964 to an impoverished family in northeastern Mpumalanga Province, Lucky Dube released his first album at the age of 18 years. He began his career performing the urbanized Zulu music called Mbaqanga. But he also recorded albums in Afrikaans, the language of the white minority.

Dube made his mark on the international scene with Reggae music and became one of the best-known African vocalists of the genre.

His first Reggae album, Rastas Never Die, was banned by the apartheid government in the mid-1980s.

The spokesman for Dube's Gallo music label, Arnold Mabunda says Dube was one of the country's most successful musicians.

"He was one of the biggest contributors in the South African music industry. Yeah. And now we are saddened," said Mabunda.

South Africa has one of the highest murder rates in the world, with nearly 20,000 homicides last year. Many of the killings occur during robberies and hijackings. These are common in a country where one-half of the population lives on less than $2 per day.

Wednesday, October 17, 2007

MKenya aua mama watoto wake mjini Lynn, Massachusetts

Marehemu Esther Kinyanjui na wanae

DUH! Haya sasa waKenya wako kwenye taarifa ya habari tena hapa Boston. Safari hii huyo jamaa aliyekuwa na mazoea ya kumpiga mama watoto wake kaamua kumtoa roho kabisa! Kamchoma huyo mama kisu zaidi ya mara ishirini!

Mungu ailaze roho yake mahali pema mbinguni. AMEN.

*********************************************************************************
A 28-year-old father was in Lynn District Court Wednesday, charged with the stabbing death of the mother his two children. Patrick Waweru, 28, of Lynn, is charged in connection with the stabbing of Esther Kinyanjui, 31, the mother of his children.

The victim's sister, Margaret Kinyanjui, 27, was also injured in the attack and the family was speaking out at the courthouse. NewsCenter 5's Pam Cross reported that Esther Kinyanjui was hiding inside her sister's apartment at 4 Kingsley Terrace when her estranged boyfriend broke in. He had allegedly made threats to kill in the past.

Kinyanjui was stabbed in the basement apartment with her youngest child nearby. Her sister and mother tried to stop the attack."I tried to hold the knife and I was cut here. Then he got that knife and then ... do that," Ruth Kinyanjui said, making a gesture of a knife being drawn across the throat."

She was the most loving person. She was helping all of us. Myself, my mother, the children. She loved her two children very much. She obviously loved the father of the children and that's why she was always covering for him," Margaret Kinyanjui said.

Family said the pair had a long history of domestic violence dating back until at least 2000. They said Esther would often bail him out after he hurt her, but she moved to Delaware five months ago in an attempt to get away from Waweru. She apparently was lured back, this time to her death.

Waweru pleaded not guilty to murder, kidnapping, two counts of assault and battery with a dangerous weapon and six counts of armed assault in a dwelling and home invasion. He was ordered held without bail and sent to Bridgewater State Hospital for observation.

Concert ya Rose Muhando Dallas, Texas



Kanisa la wa Tanzania na watu wote wanaotumia lugha ya kiswahili wanapenda kuwatangazia wadau wote wa blog hii popote walipo kwamba yule mwanamzuki machachari wa nyimbo za injili kutoka nyumbani Tanzania Dada ROSE MUHANDO atakuwa na onyesho kabambe katika kanisa hilo.

Onyesho hili la aina yake litaanza saa kumi kamili jioni siku ya jumapili tarehe 21.10.2007. Dada ROSE MUHANDO ni muimbaji aliyetokea kupendwa ndani na nje ya Tanzania, uimbaji wake wa nguvu na hisia kali unavutia watu wengi.

Rose Muhando ameshashinda tuzo mbali mbali za uimbaji.
Kwa wale watakaopenda waandaliwe malazi tunaomba wawasiliane nasi kupitia:
Email: umojachurch@yahoo.com,
Simu: 214 554 7381,
682 552 6402,
au 214 341 7287.
Kanda zote za Rose zitauzwa moja kwa moja kutoka ukumbini.
Kanisa lako ulipendalo la Umoja.

ANWANI NI:

Trinity Hillcrest Church

12727 Hillcrest Road • Dallas, TX 75230

Bongoland II


Habari niliyopata leo ni kuwa sinema ya Bongoland II itatoka hivi karibuni!
Kwa habari zaidi nenda: http://www.kibirafilms.com

Tuesday, October 16, 2007

Sinema kuhusu M.V. Liemba



Kuna sinema aina ya Documentary, itatoka hivi karibuni kuhusu ile meli maarufu ya ziwa Tanganyika, M.V. Liemba. Hiyo meli bado ni imara na inaendelea kufanya kazi japo ina miaka karibu 100!
Kwa habari zaidi na kuona clip nenda: http://www.liemba.org/

Saturday, October 13, 2007

Mwandishi wa Habari Nellie Kidela amefariki dunia.

Leo nimepata habari kuwa mwandishi wa habari na mtangazaji wa siku nyingi wa Radio Tanzania Dar es Salaam, Nellie Kidela, amefariki dunia.

Dada Nelly ni moja wa waanzilishi wa chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania, TAMWA. Mkutano wa kwanza kabisa ulifanyika nyumbani kwake.

Taarifa niliyonayo ni kuwa Dada Nellie alifariki siku ya Jumatatu tarehe nane Oktoba na alizikwa, jumatano tarehe 10 Oktoba katika makaburi ya Kinondoni. Alikuwa ameugua ugonjwa wa kansa siku nyingi. Na miaka ya nyuma aliwahi kupata matibabu hapa Boston.

Dada Nellie alikuwa mama yake mzazi na Nuru Mkeremi wa hapa Boston, Massachusetts.

Mungu ailaze roho take mahali pema mbinguni. AMEN.

Mkono wa Iddi


Nawatakia wapendwa wasomaji waislamu Eid Mubarak!
Hapa Boston leo kuna Suala kwenye msikiti kubwa iliyofunguliwa hivi karibuni Roxbury Crossing. Vyombo vya habari vinasema wana tarajia zaidi ya waislamu 6,000 kuhudhuria. Kuna wazungu wameingia na hofu kuwa na waislamu wengi hivyo katika eneo moja wanasema kumbuka 9/11. Ubaguzi hauishi jamani!
Na pia kuna sherehe iliyoandaliwa na waTanzania hapa Boston leo jioni ya kusherekea Eid.
Time: 6pm to 12am
Address: BROMLEY HALL
10 LAMARTINE STREET
JAMAICA PLAIN MA 02130

Thursday, October 11, 2007

Bado Hajashiba!

Snoop Dogg na wembamba wake kamaliza fillet mignon, prime rib sijui. Bongo watu wangapi wangepata dishi hapo?

Wednesday, October 10, 2007