Monday, June 22, 2009

Habari zaidi za Ze Utamu Kukamatwa

Haya, naona karibu tutasikia rasmi jina la aliyekamatwa. Na kweli huwezi kumchokoza mkuu wa nchi.

***************************************************************
Kutoka ippmedia.com

How `Ze Utamu` host was nabbed

Na Staff writer

21st June 2009

He rose suddenly from the IT World, conquering the corridors of celebrities in Tanzania due to his ability to post damning pictures online with some of these pictures showing celebs and politicians naked, before he was nabbed this week in Essex, UK.

The man behind the reckless website that has highly damaged the reputation of over 6,000 Tanzanians including the head of state was arrested in a well planned move coordinated by the Tanzania intelligence community and their counterparts from UK and Israel, The Guardian on Sunday has learnt.

According to the well placed sources within the Interpol, just a few days after the report that damning cropped pictures purportedly showing the head of state were posted online, the intelligence communities tasked its IT experts to track down the culprit behind the defamatory website.

To nab the host of the website, local IT experts from the intelligence communities contracted their counterparts from Israel who helped tracing the real host and author of the popular website known as ‘www.zeutamu.com’.

After conducting a thorough investigation to various local Internet Service Providers, it was concluded that the server that host the website originated in the United Kingdom.

This, according to sources, was reached after analysing over one hundred posts posted in the website whereby their origins finally showed the country’s code used in hosting internet services.

Following that link, local IT experts from Intelligence Communities contacted their counterparts in UK mainly from MI5, in order to establish the person behind the website.

The investigation within UK was conducted by experts whereby finally the real suspect behind the website was located after his Internet Service Provider was identified.

The ISP provider was interrogated thoroughly and finally the experts established the real identity of the man whose website has defamed and offended a total of 6,080 prominent Tanzanians, including politicians, celebrities and others.

The dramatic move by the local intelligence communities is the first to be done in East Africa in cracking down online crimes, sending an alarming message to the growing number of bloggers inside and outside the country.

Perhaps the most disturbing question is that the man behind this damning website is a highly trained IT expert who was educated by taxpayers’ money and has a link to some of the prominent political figures in the country.

The investigators are still conducting thorough investigations to establish other local suspects who have been collaborating with the blogger to post damning and defamatory pictures online during the past few months.

After concluding their findings, the investigators tipped Interpol as required by international law in order to arrest the suspect.

Interpol working on the tips from intelligence officials raided the home of the suspect early this week in Essex, UK, and arrested the suspect who is a Tanzanian national.

The Tanzanian national aged 39 years old is an expert in IT with strong command in both written and oral English, Chinese and Swahili languages.


When you rattle the snake get prepared for its reactions…You can’t mess around with people including the head of state and expect to walk freely, ” a senior official from the Interpol told The Guardian on Sunday under conditions of anonymity.

CHANZO: GUARDIAN ON SUNDAY

*********************************************
Mmiliki wa ze utamu adaiwa kukamatwa

Kutoka ippmedia.com

20th June 2009

Mtandao wa Ze utamu ambao mmiliki wake anasakwa kwaudi na uvumba.
Kuna habari kwamba Jeshi la Polisi nchini kwa kushirikiana na Polisi wa Kimataifa (Interpol) wamefanikiwa kumnasa mtu anayedaiwa kumiliki blog ya Ze Utamu ambayo imekuwa ikionyesha picha za kuwadhalilisha watu.

Miongoni mwa udhalilishaji huo ni kuwaonyesha watu wakiwa katika utupu na wengine wakifanya vitendo vya ngono.

Habari ambazo Nipashe ilizipata jana kutoka vyanzo mbalimbali, zilieleza kuwa aliyekamatwa ni raia mmoja wa Uingereza ambaye ana asili ya Tanzania.

Mmiliki huyo anadaiwa kuwa ni mtoto wa kiongozi mwandamizi mstaafu aliyewahi kuitumikia nchi katika nyadhifa kubwa, lakini ana uraia wa Uingereza. Kutokana na sababu za kimaadili hatuwezi kutaja jina lake kwa sasa, hadi vyombo vya usalama vitakapothibitisha.

Kijana huyo anatuhumiwa kwa kuendesha mtandao wa Ze Utamu, ambao umekuwa ukionyesha picha mbalimbali na hasa za watu maarufu, wakiwemo viongozi waandamizi serikalini wakifanya ngono.

Nyingi ya picha hizo na hasa za viongozi zimekuwa zighushiwa (doctored) ili kuwaonyesha kuwa wanafanya vitendo vya aibu kwa nia ya kuwadhalilisha.

Hata hivyo, Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba, alipoulizwa kukamatwa kwa mtu huyo nchini Uingereza, alisema kuwa ofisi yake haina taarifa kuhusu kukamatwa kwake.

"Ndugu mwandishi, suala la kushikiliwa mtu huyo ofisi yangu haina taarifa hizo, na pia habari kuhusu mtandao huo sizijui kabisa," alisema Manumba.

Mwishoni mwa Aprili, mwaka huu, Manumba alitangaza kuwa Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Polisi wa Kimataifa wanaendesha msako mkali dhidi ya wamiliki na watu wanaoendesha mtandao wa Ze Utamu.

Na ilipofika Mei 5, mwaka huu, Manumba alimwambia mwandishi wa Nipashe kuwa uchunguzi wa kuwanasa watu hao umefikia patamu.

Nipashe ilipowasiliana na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Said Mwema, ili kuthibitisha taarifa za kukamatwa kwa mmiliki huyo, askari mmoja aliyejitambulisha kuwa ni msaidizi wake, Joshua Mwangasa, alipokea simu ya IGP Mwema na kueleza kuwa yupo kwenye kikao, lakini akasema kuwa taarifa kuhusu blog ya Ze Utamu itatolewa wakati wo wote kama zipo.

Alipotakiwa kueleza taarifa hizo zitatolewa lini, Mwangasa alishindwa kuweka bayana suala hilo. Hata hivyo, alipoulizwa kama ni kweli wanamshikilia mmiliki huyo, Mwangasa alisema hana jibu hilo na akamtaka Mwandishi Wetu awasiliane na DCI Manumba.

Mwandishi alipomueleza kuwa tayari alishampiga simu DCI Manumba na majibu aliyotoa, Mwangasa alisema kama taarifa hizo kama zipo zitatolewa.

"Mwandishi kama taarifa hizo zipo, zitatolewa wakati wowote ila siwezi kudhibitisha kama anashikiliwa au zitatolewa lini," alisema.

Habari zilizopatikana kuhusu mmiliki huyo, zinaeleza kwamba ni mtaalamu wa kompyuta na ana uwezo wa kuzungumza na kuandika Kiingereza, Kiswahili na Kichina na ana makazi katika mji wa Essex nchini Uingereza.

Taarifa zilieleza kuwa wataalamu wa Idara ya Upelelezi kutoka Tanzania wakishirikiana na wenzao wa Uingereza, walifanikiwa kuonana na mmiliki wa blog hiyo na kupata ushahidi wa kutosha kwamba ndiye alikuwa mmiliki wake.

Habari hiyo ilidai kuwa Idara ya Upelelezi na Polisi wa Uingereza wameutaarifu Ubalozi wa Tanzania mjini London kuhusu suala hilo, ambapo baadhi ya maofisa wa ubalozi huo, Clement Kiondo na Amos Msanjila wanadaiwa kwenye taarifa zilizozagaa kwamba walifahamishwa kuhusu mmiliki huyo.

Nipashe pia ilifanya jitihada za kuwasiliana na ofisi ya ubalozi Tanzania London, Uingereza, ambako ofisa mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Mariam Kombo akidai ni Katibu wa Balozi wa Tanzania nchini humo, Mwanaidi Sinare Maajar, alisema ubalozi huo hauna taarifa ya kukamatwa kwa mmiliki huyo.

Kondo alisema Balozi Maajar alikuwa akihudhuria mkutano na maafisa wengine, lakini alithibitisha kwamba hakuna taarifa za kukamatwa kwa mmiliki huyo ambaye anadaiwa kwamba tayari amekwisharejeshwa nchini ili kujibu tuhuma za kuendesha mtandao unaowadhalilidha watu.

Imefahamika kwamba kuna malalamiko 6,850 yaliyoandikishwa juu udhalilishwaji wa watu uliokuwa ukifanywa na mtandao huo.

Mtandao huo ulisimamishwa mwanzoni mwa Februari, mwaka huu kwa maombi ya serikali ya Tanzania baada ya kutoa picha ya kumdhalilisha kiongozi mmoja mwandamizi wa serikali.

Ufuatiliaji uliofanywa baada ya picha hiyo ndio unaosemekana kufanikisha kukamatwa kwa mmiliki huyo.

Taarifa zaidi zinasema kwamba Polisi wa upelelezi wamewahojiWatanzania wengine wawili katika miji ya Wichita na San Diego nchini Marekani, ambao pia wanahusishwa na mtandao huo.

2 comments:

Anonymous said...

hivi umesoma gazeti la uhuru la jana?limesemaje?polisi, ubalozi hawana taarifa ya kukamatwa kwa mtu huyu na kwa taarifa tu mimi nimetoka kumtembelea kwake yuko mzima wa afya anaendelea na shuguli zake vyema tu. kabla hamjamuhukumu mtu au kusambaza vitu ambavyo hamna uhakika navyo ,ytakuja kuwatokea puani! read ur Bible...Psalm 55! ALl evils will die before their time! even liars will die before their time! ur a liar too coz unaandika habari ambazo huna uhakika nazo!we r sick of this BS seriously kama mnaleta habari muwe na uhakika sio kukurupuka tu na kuongea! siku ya kwenda kwa "pilato" pale bongo mtakapo kuwa sued ndo mtajua maharage nayo mboga!

Anonymous said...

Kwa vile mtoto wa mkubwa, KIMYAAAA!