Saturday, May 31, 2008

Australian Scholarships

Asante Da Subi kwa kunileta habari hizi:

General information on this Scholarship:

http://www.adsafrica.com.au/scholarships/adsSouthEastAfrica.cfm

Applications NOW OPEN for the 2009 intake!

Priority sectors:

Public health (Including child & maternal health, HIV/AIDS and public sector management aspects of the sector

Environment (Including water & sanitation)

Number of scholarships available for 2009 intake : 12

Category:Public - The public category of scholarships is intended to strengthen public sector capacity in Africa. Public sector applicants are employees from various government departments and para-statals. Applications must be nominated and endorsed by the relevant nominating authority in each of the African countries.

Closing date : 13 June 2008

Eligible Tanzanian Nationals are invited to foward the following documents for consideration:
A completed Expression of Interest (click here)
A current cirriculum vitae
Certified copies of university degree(s) and transcripts
A one-page summary of the reasons for wishing to undertake postgraduate training in Australia and how this training will benefit Tanzania.
Failure to complete the application form and submit all documentation requested will lead to automatic disqualification. No undergraduate or PhD nominations will be considered.

Submit to:Dr. Faissal H. Issa
Permanent Secretary Public Service ManagementPresidents OfficeP.O. Box 2483 Dar-es-SalaamTanzania
Tel: +255 (0) 22 212 2908 Fax: + 255 (0) 22 213 1365
IELTS:
It is preferred that applicants have a level of English language competency as indicated by an overall band 6.5 in the IELTS. Alternatively, candidates may present an official letter from the institution where they last studied, indicating that the medium of instruction was English.
For further Information on IELTS click here

Other requirements:Applicants must have a minimum of two years' work experience, preferably five, and possess undergraduate qualifications at a minimum of upper second class honours level (with a minimum average academic mark of 65 per cent).

Pre-Departure Briefings for the 2009 intake:
Date: TBA

Usivute Sigara Leo!




Leo ni siku ya kutotumia bidhaa za tumbaku kama sigara, cigar, pipe nk. Nichi nyingi wanakuwa na warsha za kuelimisha watu juu ya madhara ya kuvuta sigara na kutumia tumbaku.

Theme ya mwaka huu ni "Vijana kutokuvuta Sigara"

Sigara zinaua! Acheni kuvuta. Na tunajua wanaovuta sigara wananuka. Wanakuwa na harufu ya sigara kwenye nywele na nguo zao na pia midomo yao inanuka! Kwa nini mvuta sigara anakubali kuunguza mapafu yake huko mtengeneza sigara anatajirika. Mvuta sigara ana kohoahoa na anakuwa na makohozi meusi! Na ile kansa ya pafu ya sigara inaua haraka. Hapa Marekani wanasema kama kuna kitu ambayo ina uhakika wa kukua ni kuvuta sigara.
ACHENI KUVUTA SIGARA!

Kwa habari zaidi someni:

http://www.who.int/tobacco/wntd/2008/en/

http://www.dailytimes.com.pk/default.asp?page=2008%5C05%5C31%5Cstory_31-5-2008_pg13_7

Thursday, May 29, 2008

Baraka Cafe


Hii Cafe iko mtaa wa Pearl St. hapa Cambridge, MA. Wanauza chai na vyakula vya Middle East. Na hapo saloon ya nywele usiende na chini ya dola $100!

Ajali ya Treni Boston

Marehemu Terrese Edmonds



Wadau, hapa Boston mwezi huu kumekuwa na ajali kadhaa kwenye usafiri wa treni. Juzi kulitokea moto kwenye njia ya kupita treni chini ya ardhi (subway) maeneo ya Park Street. Bahati mbaya ilitokea rush hour wakati watu wanatoka kazini. Nilipata shida sana kufika nyumbani siku hiyo lakini nilifika.

Jana, maskini kwenye Green Line, treni mbili ziligongana. Kwa bahati nzuri ajali ilitokea karibu mwisho wa njia hivyo watu wengi walikuwa wamekwishashuka. Bahati mbaya, dereva wa treni iliyogonga lingine, alifariki. Watu zaidi ya kumi waliumia na ilibidi wapelekwe hospitalini kwa matibabu.

Dereva ametambulika kama Bi Terrese Edmonds alikuwa na miaka 24. Ni Mmarekani mweusi. Na tayari wanaanza kuelekeza chanzo cha hiyo ajali kwa Bi Terrese. Kuna watu amabao wanadai alikuwa anatumia cell phone yake wakati anaendesha treni. Maiti haiwezi kusema ilitokea nini.

Mungu ailaze roho yake mahala pema mbinguni. AMEN.

Jana stesheni za TV zote za Boston walikluwa na live coverage ya ajali na jitihada za kumwokoa Bi Edmonds. Kwa muda mrefu MBTA waliktaa kusema hali yake, ndipo nikahisi kuwa huyo dada alishakata roho.

Baba yake mzazi alikuwa kwenye TV akisema kuwa anamtafuta binti yake, ni dereva wa treni amepita hospitali kadhaa kumtafuta na hakumpata, simu yake hapokee. Alisema aliamua kwenda kwenye ajali baada ya kuambiwa na mfanyakazi mwenzake Terrese kuwa yeye ndiye alikuwa anaendesha hiyo treni.

Baba yake aliwaambia waandishi wa habari kuwa binti yake alipenda sana kazi yake na alikuwa ameifany kwa miezi sita tu. Nilichukia sana kusikia waandishi wa habari wakimchimba huyo mzee kuhusu habari zake binafsi. Mfano, je, una kaa na mama yake? Jamani! Mtu ana huzuni na wasiwasi halafu mnaanza kumchimba tena kwenye TV!

Kwa habari zaidi someni:

http://www.necn.com/Boston/New-England/Area-hospitals-prep-for-victims-of-train-accident/1212016597.html

Zimamoto Cambridge


Jana kulikuwa ni fire alarm kwenye jengo nalo kaa hapa Cambridge. Jirani yangu aliunguza chakula alichokuwa anapika. Moshi ulisababisha alarms za jengo ziwake! Wakaja zimamoto. Huyo ni mmoja wa waliokuja. Bahati mbaya sikupata jina lake.

Wednesday, May 28, 2008

Shairi - I Might Not Be a South African



I Might Not Be A South African..


I might not be a South African

But I'm black, my skin is the same as yours

My colour is the same as yours

My genes are African, nothing but African

When your leaders were beaten by whites

I was there to shelter them

I was patient with them

I offered them food, shelter,

Most of all, I offered them protection


I might be a South African


I can't speak Zulu, cause I'm Vhenda

I can't speak Zulu, cause I'm Shangaan

I don't know what an elbow is in Zulu

As much as you don't know it in my language

Since when was Zulu the only South African language?

Yes……………I'm not from Gauteng

I was not born here, but I'm South African

Where should I go if you beat me

I'm not beating your father, mother, brother or sister who works at my area in the mines

I'm not calling them makwerekwere

though they can't speak my language.


I might be dark in complexion


I might have the foreigners looks

I might have the foreigners body structure

Now I am scared to go to the only place that I call home

I'm scared of working down the street without my ID

Whites wanted me to do that centuries ago

Now you, my black brother is acting white


Why should you Black South Africans do this?


What makes you think that you better than me?

Who told you that I'm responsible for your unemployment?

Who told you that I'm less human

If I need to go back to Vhenda…….

let all the Zulus go back to KZN

Let all the Tswana's go back to Botswana

Let all the Sotho's go back to Lesotho

Let all the Ndebele's go back to Kwandebele

Let all the Xhosa's go back to Eastern Cape

Yes…………let all the Swati's go back to Swaziland


Is this not ignorance?

Your unemployment is your responsibility

Use your intellect

Get up and work

Let education empower you

Seek humanity


Before 1994 you blamed whites


Now you are blaming me

Who are you going to blame after chasing me away?

Who are you going to blame after killing me?

For what it's worth…………………..I'm sorry I was not born here

I'm sorry I can't speak Zulu

I'm sorry for being too dark for your Joburg

I'm sorry for cleaning the toilets you don't want to clean

I'm sorry for doing your garden

I'm sorry for repairing your shoes

I'm sorry for protecting your leaders while they were in Exile

Yes…………………what you call Exile………..is my country


And most of all…….I'm sorry for building South African infrastructure


Please my brothers let there be peace and prosperity amongst black African people.


Written by a Black African …………………Deejay

Mkapa Hajajibu Hoja - Prof. Baregu

Prof. Baregu hachoki! Mwaka jana aliuliza maswali kadhaa kuhusu enzi za Mh. Mkapa. Hakupata majibu. Na jana kaongea tena!

*************************************************************

Kutoka ippmedia.com

Mkapa hujajibu hoja - Baregu

2008-05-28

Na Lucy Lyatuu

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Mwesiga Baregu, amemshangaa rais mstaafu Benjamin Mkapa kwa kutoa majibu ya jumla dhidi ya tuhuma nzito zinazomkabili. Alikuwa anazungumza na Nipashe kwa njia ya simu kuhusu utetezi alioutoa Bw. Mkapa huko Masasi mkoani Mtwara kuwa wanaodai kuwa ni `fisadi` wana chuki binafsi kwa vile aliwanyima madaraka akiwa Ikulu.

Profesa Baregu ambaye ni mtaalamu wa sayansi za siasa alisema tuhuma dhidi ya Rais mstaafu zinajulikana na zinaeleweka, hivyo hakutakiwa kutoa majibu ya jumla na ya juu juu. Alimtaka kiongozi huyo kuweka wazi idadi ya watu aliowanyima vyeo au madaraka wakati akiwa madarakani ili kuipa nguvu hoja yake.

``Kwa mfano mimi sijawahi kutafuta kazi kwake sasa atatoaje majibu ya jumla kuwa wanaotoa madai hayo wana chuki binafsi wakati masuala ya Benki M na mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira unafahamika?`` alihoji Profesa Baregu.

Aliongeza kuwa kama Bw. Mkapa anataka kujibu tuhuma dhidi yake azungumze kwani mambo mengi yameandikwa kwenye vyombo vya habari. Alimtaka asiandame watu kwa ujumbe mbaya na kumkumbusha kuwa ni vyema akafahamu kuwa majibu ya jumla hayamsaidii.
" Asitake kumuua tarishi kwa kuleta ujumbe mbaya,`` alisema Profesa Baregu.

Kwa upande wake, Waziri Mkuu wa awamu wa pili, Jaji Joseph Warioba alipohojiwa hakuwa tayari kutoa maoni na kuongeza kuwa yaliyosemwa dhidi ya kiongozi huyo yanatosha. Rais Mkapa alipochukua madaraka mwishoni mwa 1995 alianza kazi kwa kuunda Tume ya Kuchunguza Kero za Rushwa iliyoongozwa na Jaji Warioba.

Mkapa aliyeingia madarakani kwa jina la aliyetakata (Mr Clean) aliahidi kutumia ripoti ya Jaji Warioba kupambana na rushwa na kuondoa ufisadi serikalini, kitu ambacho hakikuwahi kuonekana waziwazi.

Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Wilbroad Slaa, akizungumzia utetezi huo alisema , Bw. Mkapa hajajibu hoja badala yake ameleta propaganda na poroja za kisiasa. Akitoa maoni yake kwa njia ya simu kufuatia majibu ya Rais mstaafu, alisema Bw. Mkapa alitakiwa kujibu taarifa zilizopo kuwa amesajili makampuni wakati akiwa Ikulu na sio kuleta hoja za kwamba kuna waliokuwa wakitaka madaraka.

``Kama itakumbukwa, mwaka jana Septemba 27. mimi na Bw. Tundu Lissu, tulikuwa watu wa kwanza kutaja orodha ya mafisadi 11 akiwemo Bw. Mkapa,`` alisema. Alisema binafsi hajawahi kupiga magoti akimuomba Bw. Mkapa ampe cheo au madaraka na alichonacho ni uchungu na rasilimali za Watanzania.

Alisema Bw. Mkapa akiwa madarakani alisajili makampuni ya ANBEN na Tanpower Resources Ltd ambayo rais huyo mstaafu na Waziri wa zamani wa Madini na Nishati, Bw. Daniel Yona walitajwa kuwa na hisa ndani ya Tanpower Resources.

Aliongeza kuwa hajawahi kufanya kazi serikalini na hategemei kuwepo na pia hana chuki ya kutokuwa na madaraka kama anavyodai Bw. Mkapa, kwa misingi hiyo anadhani kauli aliyoitoa haina ukweli.

Alisema anachotakiwa kufanya mtuhumiwa huyo ni kujibu hoja ya kwamba ni kweli alisajili kampuni hizo kwa anuani ya biashara ya Luthuli Street namba 15 ambayo ni ya Ikulu.

``Tunataka tu kujua alilipa kiasi gani kama gharama ya pango la kutumia Ikulu?`` alihoji. Dk. Slaa aliongeza kuwa jambo lingine ambalo alitakiwa kujibu ni umiliki wa ANBEN, kampuni iliyokopa Sh. milioni 500 NBC na kushinikiza benki hiyo ibinafsishwe.

Aidha alisema jambo lingine ambalo anatakiwa kujitokeza na kulijibu ni nyaraka zilizoko kwa Wakala wa Kusajili na Kutoa Leseni kwa Kampuni (BRELLA) kwamba anamiliki makampuni hayo akiwa kama mjasiriamali.

Alimtaka kujitokeza hadharani na kujibu hoja hizo ili zionyeshe wazi ukweli wa kauli alizozitoa. Jitihada za kuwapata kwa simu Mwenyekiti wa CHADEMA Bw. Freeman Mbowe na Katibu Mwenezi wa CCM Bw. John Chiligati hazikufanikiwa.

SOURCE: Nipashe

Wayehudi wachoma moto Biblia huko Israel


Leo kuna habari kuwa huko Tel Aviv, Israel, wayehudi wenye siasa kali wamechoma moto biblia kadhaa zenye Agano Jipya. Agano Jipya inahusu Bwana Yesu Kristo, na wayehudi hawaamini habari zake.
Watu wanauliza kama wayehudi hawaoni kama kuchoma Biblia ni sawa na jinsi Hitler alivyochoma moto Torah zao.

Sasa wakristo wanaoenda kuhiji huko Israel kuona sehemu Bwana Yesu alipozaliwa wameanza kuwa na wasiwasi na usalama wao.

Habari pia zinasema kuwa kundi la Messianic Jews (wayehudi wanaoamwamini Bwana Yesu) ambao ni wachache huko Israel nao wameanza kuwa na hofu kuhusu usalama wao na haki yao ya kuabudu. Wengi wa Messianic Jews ni Wayehudi kutoka Eithiopia ambao ni weusi!

Messainic Jews huko Israel wamekutwa wakibaguliwa na Wayehudi wengine. Pia miezi miwili iliyopita, mtoto wa mchungaji wa Messianic aliumizwa vibaya baada ya kufungua barua enye bomu iliyotumwa kwa baba yake.
Nchi ya Israel ilianzishwa mwaka 1947 na wayehudi kutoka Ulaya waliyokuwa wananyanyaswa vibaya. Karibu wayehudi milioni 6 waliuliwa na Hitler. Waliteka nchi ya Palestina kwa vile ilikuwa nchi ya mababu zao tangu enzi za Musa na ni chanzo cha matatizo kati yao na waarabu hadi leo.

Kwa habari zaidi someni:

Tuesday, May 27, 2008

2008 African Summit, Boston, MA


2008 African Summit

Hosted by Sibusiso’s Boston Bridging Program

Working collaboratively with Community Leaders and Providers Linking Sub Saharan Africans to comprehensive services

Saturday June 14, 2008
9:00 a.m. – 3:00 p.m.
Brookline Holiday Inn
1200 Beacon Street, Brookline MA

Program Overview

Presentations on Sub Saharan Health Initiatives

Personal reflections on living with HIV

Workshops reviewing critical resources for:
*Health Insurance *Immigration *Negotiating Health & Faith



Targeted Audience: African Community, HIV & Hepatitis Providers, and interested community members are welcome to attend

Meals: Breakfast and lunch provided

Parking: Hotel lot, on street meters , accessible by Green Line – C

Cost: Free to all participants

To register or obtain more information: http://www.sibusiso.org/

email: cmcmahon@sibusiso.org / dschiano@sibusiso.org

Or call: 617-620-7278
Registration Deadline – Monday June 2, 2008

Serikali Inajikanganya - Kifo cha Dk. Ballali

Misa ya Kumwombea Mzee Ballali huko Washington D.C. (picha kutoka Michuzi Blog)

Wadau, lazima niseme kuwa bado kuna maswali mengi kuhusu kifo cha Mzee Ballali.

************************************************************
Kutoka ippmedia.com

Serikali inajikanganya kifo cha Ballali - Slaa

2008-05-27

Na Simon Mhina

Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilbroad Slaa, amesema hoja za Waziri wa Mambo ya Nje, Bw. Benard Membe kwamba serikali haihusiki na kifo cha Dk. Daudi Ballali, hazijaisaidia serikali, badala yake zimezidi kuleta mkanganyiko.

Alisema yeye pamoja na wapinzani wengine, walijenga hoja kwamba ni kwa nini wanaihusisha serikali na kifo hicho, tofauti na Bw. Membe ambaye amekanusha bila kujibu hoja zao na wala hakutoa maelezo ya msingi.
Dk. Slaa, ambaye pia ni Mbunge wa Karatu, alisema waziri huyo amezidisha kiwango cha wasiwasi walichonacho watanzania, pale aliposhindwa kutoa maelezo kwamba Dk. Ballali alikuwa amelazwa hospitali gani na ugonjwa gani.

Alisema hoja ya Bw. Membe kwamba wanaotoa tuhuma dhidi ya serikali wanafanya hivyo kwa hisia, haina msingi na inadhihirisha jinsi waziri huyo anavyobabaika. ``Yaani ugonjwa wa mtu mkubwa mwenye tuhuma nzito kama Ballali, umefichwa, kifo chake kimefichwa, mazishi yake yamefichwa, hata Maiti yake haikuonekana, halafu anasema tuhuma zetu ni hisia? Huu ni upotoshaji mkubwa na kuzidi kujikanganya,`` alisema.

Mbunge huyo alisema kitu ambacho kingeweza kuinasua serikali katika tuhuma hizo, ni Bw. Membe kutaja sehemu aliyokuwa amelezwa Dk. Ballali. ``Tangu lini hospitali ikawa ni sehemu ya siri, kwa nini hawataki kusema?`` Alihoji.

Alisema madai aliyotoa waziri huyo kwamba mwenye vielelezo toka kwa daktari vinavyoonyesha kwamba Dk. Ballali alikufa kwa sumu avitoe, au yanaonyesha kwamba kweli kifo cha Gavana huyo wa zamani wa BoT kilipangwa. ``Mtanzania wa kawaida atawezaje kumpata daktari aliyemtibu Ballali wakati hata hospitali alipokuwa amelazwa panafichwa?

Kumbe wameficha kwa makusudi ili Watanzania washindwe kupata vielelezo?`` Alihoji na kuongeza: ``Serikali haihitaji vielelezo, bali ndiyo iliyofanya njama za kuhakikisha hakuna kielelezo chochote ambacho kinahusiana na kifo hicho kinachoweza kupatikana.``

Alisema kama kweli serikali inasisitiza kwamba haihusiki, itaje hospitali ambayo Dk. Ballali alikuwa akitibiwa na ugonjwa uliomsibu. ``Bw. Membe anasema mwenye vielelezo apeleke? Kazi yake kama waziri wa Mambo ya Nje ni ipi hasa?
Yeye ndiye alitakiwa azungumze na Balozi wetu kule Marekani ili aeleze habari za ugonjwa na baadaye kifo chake, kama mtu mkubwa kama Ballali anaweza kufikwa na kifo nchi za nje bila watu kujua, sembuse mtu wa kawaida?`` Alihoji.

Dk. Slaa alisema ili serikali ijisafishe, ni vizuri ikasema ni kwa nini hata hapa mjini, matanga ya marehemu huyo yalikuwa ya siri na majirani walikatazwa kuingia huku waandishi wa habari wakifukuzwa.

``Tunataka iundwe tume huru ya kuchunguza kifo hicho, kwa vile hadi sasa serikali haijatoa maelezo yanayojitosheleza. Tunataka tume kwa vile pesa za EPA bado ziko mikononi mwa mafisadi, ambao huenda ni marafiki wakubwa wa serikali,`` alisema.

Watoto wadogo walazimishwa kufanya ngono ili wapate Chakula!


Jamani! Unaweza kulia baada ya kusikia habari hizi! Kumbe huko Haiti, Sudan, Ivory Coast na nchi zingine watoto wadogo wenye miaka sita wamelazimishwa kufanya ngono na kupiga picha za uchi kusudi wapate chakula kutoka kwa wafanyakazi wa vyama vinavyotoa misaada.
Wanasema kuwawalinda amani (Peacekeepers), na watoa misaada wa vikundi mbalimbali wamo kwenye orodha ya wanaonyanyasa watoto wadogo. Wanasema kuwa mara nyingi uhalifu kama huo unatokea kwenye makambi ya wakimbizi. Huduma mpaka kwa ngono! Habari zinasema wamelazimisha hata watoto wenye miaka sita kufanya ngono!
Huko Haiti binti wa miaka kumi na tano alisema kuwa alikuwa antembea na rafiki zake. Wakakutana na kundi la wafanyakazi wa chama kimoja cha misaada. Walitoa bolo zao kwenye suruali na kuwaambia wazinyonye ili wapate hela. Yule binti alikataa lakini rafiki zake walikubali na kupewa vihela na pipi.

Ubaya zaidi ni kuwa ingawa wenyeji wanajua inatokea nini, hawasemi kitu. Wanaogopa kuwa kama wakilalamika misaada itaacha kuja.

Lakini hebu mjiulize. Ni watu gani wanaofanya kazi kwenye hizi kundi? Mara nyingi ni watu waliokosa kazi kwao! Je, wanapimwa akili kabla ya kupewa kazi muhimu kama kwenda kugawa chakula au kulinda amani.

Lazima nisifu ripoti waliotoa Save the Children. Wamefanya kazi nzuri mno ya kuumbua hao washenzi!
Kwa habari zaidi someni:



Mtalii wa kiMarekani afa baada ya Kugongwa na Treni Italia


Leo kuna habari za kusikitisha kutoka Italy. Mzee wa kizungu kutoka California, Frank Phel, (74) na mke wake walikuwa wanatalii huko Ulaya. Walikuwa wamemalzia cruise ya meli kwenye bahari ya Mediteranean, na walifika Roma, Italia.

Walikuwa wanasubiri usafiri wa basi asubuhi kwenda Poland. Basi ilikuwa inaondokea huko kwenye kituo cha treni. Ugomvi ukatokea katika ya kundi fulani. Wale wazee walianza kuwa na hofu. Akatokea Mzee wa KiItalia na kuanza kuongea nao na kujifanya rafiki. Akawaletea vinywaji aina ya cappucino. Kumbe mle yule baba alitia madawa ya kulevya. Wale wazee walikunywa zile cappuciono. Walivyolala, yule mzee wa kiItalia kawaibia kila kitu walichokuwa nacho. Kuamka asubuhi, na kuona hawana kitu, yule mzee alimwambia mke wake kuwa anaenda kutafuta mizigo yao, huko bado kalewa yale madawa. Alikuwa anatembea kwenye njia ya treni ndipo aligongwa.

Kwanza polisi wa Italia walidhania kuwa yule Mzee alijiua. Baada ya kuchunguza video ya stesheni waliona yule MwiItalia anawapa zile cappucino na kuwaibia.

Hivi sasa, yule MwiItalia amekamatwa na polisi. Sijui sheria za Italia lakini huyo mshenzi anastahilia dhabu ya kifo! Habari zinasema huko Roma, kuna vibaka na wezi wengi wanaovizia watalii!

Halahala mkienda ugenini.

Kwa habari zaidi someni:


Monday, May 26, 2008

Sherehe za Kuadhimisha Miaka 10 ya International Gospel Church



Bango Nje ya Kanisa
Wakati wa Chakula cha Mchana

Pastor Jared Mlongecha na Mgeni kutoka Canada
Les Mas wakiimba
Pastor Jared na Mke wake wkikabidhi Vyeti


Baadhi ya waimbaji wa Kikundi cha Yuaja wa IGC

Hema tuliyofanyia Sherehe nje ya Kanisa




Pastor Jared na Mke wake wakifurahia zawadi kutoka kwa Waumini wa Kanisa
Keki ya Kusherekea Miaka 10 ya Kanisa
Pastor Pacific Zagabe akiongoza Maombi
Pastor Jared na Mke wake wakiwa Meza Kuu (High Table)




Les Mas wakiimba wimbo wao Njaa



Kikundi cha Les Mas wakiimba wimbo wao 'Njaa' wakati wa sherehe za miaka 10 ya International Gospel Church, siku ya jumapili Mei 25, 2008.

Saturday, May 24, 2008

Mkutano wa International Gospel Church

Hizi ni baadhi ya picha nilizopiga jana jioni kwenye mkutano mkuu wa International Gospel Church huko, Chelsea, MA. Unahudhuriwa na wageni /waumini wengi kutoka nchi mbalimbali.

Kesho ni siku ya mwisho wa mktano na sherehe ya kuadhilisha miaka 10 ya kanisa.

Kijana Felix wa IGC akiburudisha wakati wa kutoa sadaka

Pastor Jared Mlongecha akitafsiri maneno ya Evangelist Clint Rodgers

Evangelist Clint Rodgers akiongea na moja wa waumini aliyetoka Maryland
Evangelist Clint Rodgers akisoma kutoka Biblia

Wachungaji na waimbaji, 'Les Mas' kutoka Ubelgiji

Evangelist Clint Rodgers akielezea jinsi alivyokoka na kumjua Bwana Yesu

Baadhi ya washiriki./waumini wa Mkutano



Wachungaji kutoka Canada

Mchungaji Joel na mke wake Hilda kutoka Birmingham, Alabama

Felix wa IGC akiburudisha waumini kabla ya Sermon

Obama Hatarini?!

Kava ya mbele la gazeti Roswell Beacon (Georgia) iliyotoka May 15, 2008


Ukiwa mgombea rais mweusi uko hatarini kuuliwa. Kwa kujua hivyo, Secret Service walitoa ulinzi kwa mgombea rais wa chama cha Democrats mapema. Obama amekuwa akilindwa kwa mieza 18 sasa.

Nchi hii kuna wabaguzi hasa. Yaani white supremacists wanaoamini kwamba mtu mweusi si bindamu na hasthili kuwa na chochote. Huwezi kuamini kuwa mwaka 2008 bado wapo. Sehemu zingine hapa Marekani huwezi kwenda na kuwa na uhakika wa kutoka na maisha yako ukiwa mweusi.

Ajabu, mpinzani wa Obama, Senator Hillary Clinton, amesema kuwa si ajabu watu kugombania nafasi ya mgombea hadi mwezi June, na kusema habari ya kuuliwa kwa Senator Robert F. Kennedy mwaka 1968. Sasa watu wameshutuka! Wametafsiri kuwa Clinton aikuwa na maana kuwa wakimwua Obama, yeye yupo kushika nafasi ya mgombea rais. DUH!

Kwa kweli watu wamemkasirikia Hillary kwa maneno yake.

Kwa habari zaidi someni:

http://blogs.abcnews.com/politicalpunch/2008/05/assassination-d.html

http://afp.google.com/article/ALeqM5jbMPoA_wjG3rgLbbsD-mT30oWfZA

http://ap.google.com/article/ALeqM5g-qGLDs-gAnZiUXD2NU51ry3j3dwD90RJVIO0

Waliomsulubu Chatu Watafutwa Boston!


Huko Lawrence, Massachusetts nyoka aina ya chatu alikutwa kwenye nguzo ya simu amepigiliwa misumari mitano. Waokoa wanyama hapa wanasema kuwa angebaki huko muda mrefu zaidi angekufa.

Hivi sasa huyo chatu yuko kwenye hospitali ya wanyama hapa Boston akipewa dawa ya kupunguza maumivu.

Kuna reward ya dola $5oo kwa ambaye atamwumbua aliyemtesa nyoka huyo. Wanasema aliyemtesa nyoka huyo ana roho mbaya kupindukia! Unaweza kupiga simu namba 617-522-6008 kutoa ripoti kama unajua aliyemtesa!

*****************************************************
Python found nailed to telephone pole

May 24, 2008

LAWRENCE, Mass., May 24 (UPI) -- A 2-foot python found nailed to a telephone pole in Lawrence, Mass., is recovering at a Boston animal hospital.

The snake was discovered Wednesday, attached to the pole by six 2-inch roofing nails, the Boston Herald reported. Investigators say it may have been there for as long as 20 hours.Brian Adams of the Massachusetts Society for the Prevention of Cruelty to Animals said the snake is still in considerable pain."

People seem to think that animals don't feel pain," he said. "They absolutely do, and snakes are no different."The snake has been nicknamed Trent by its caretakers at the Angell Memorial Animal Medical Center.

Veterinarians said none of its internal organs were damaged.The MSPCA has offered a $500 reward for information leading to the arrest of the person who nailed the snake.
Kwa habari zaidi someni:

Friday, May 23, 2008

Balali Aliagwa Jumanne!

Kutoka Ippmedia.com

Balali Aagwa

2008-05-23 22

Na Mwandishi Dar, Mashirika

Aliyekuwa Gavana wa Tanzania, Dokta Daud Balali aliyefariki Ijumaa iliyopita huko nchini Marekani, hatimaye ameagwa rasmi na ndugu na wapendwa wake, kabla ya mwili wake kupelekwa kwenye makazi yake mapya atakapopata pumziko la milele.

Taarifa za mtandao zilizothibitishwa na baadhi ya jamaa wa gavana huyo waishio Marekani zinadai kwamba, familia ya yake iliyo huko majuu na watu wa karibu, waliaga mwili wake Jumanne wiki hii. Kwa mujibu wa taarifa hizo, Jumanne ndiyo ilikuwa fursa pekee ya watu maalum waliopewa kibali kuona mwili wa Dk. Balali.

Imedaiwa kuwa leo, hakutakuwa na uwezekano wowote wa waombolezaji kuonyeshwa mwili wa marehemu. Kwa mujibu wa taarifa hizo, misa ya kumuombea marehemu ilitarajia kufanyika leo kuanzia saa 4:00 asubuhi (kwa saa za huko) katika kanisa la St. Stephen Martyr lilililo Pennsylvania Ave, NW Washingiton DC.

Ilielezwa kuwa mazishi yatafanyika katika makaburi ya ``Lango la Mbinguni\'\' yaliyopo eneo la Silver Spring, mjini Washington leo mchana. (kwa saa za kule). Taarifa zaidi zinadai kuwa shughuli hiyo nzima ni marufuku kwa wazamiaji ambao hawajaalikwa na kwamba ni maalum kwa ndugu, jamaa, na marafiki wa karibu.

Habari za mtandao zinasema bado haijajulikana kwa uhakika kama mwili wa marehemu utazikwa ardhini kama ilivyo desturi ya Kiafrika au utateketezwa kwa moto kwani makaburi hayo yanatoa huduma hiyo pia.

Kama ulikuwa ni wosia wake kuteketezwa, basi kwa kanuni za Kanisa Katoliki shughuli hiyo, itafanyika mara tu baada ya ibada. Kwa kanuni za Kanisa Katoliki mwili uliolazwa kwa njia ya kuteketezwa kwa moto mabaki yake (majivu) hawapewi familia, kusambazwa au kugawanywa katika mafungu madogo madogo na badala yake ni lazima viwekwe ardhini au kwenye sehemu maalum inayotumika kwa maziko ya namna hiyo.

Dk. Ballali ambaye amefariki akiwa amezungukwa na wingu kubwa la kashfa dhidi yake na dhidi ya taasisi aliyoingoza inasemakana aliacha wosia uliotaka atakapofariki basi azikwe Marekani.

Taarifa zaidi zimedai kuwa ibada ya mazishi inatarajiwa kuhudhuriwa na watu mbalimbali wakiongozwa na Balozi wa Tanzani nchini Marekani Bw. Ombeni Sefue, watumishi wa idara mbalimbali alizowahi kuzitumikia ikiwemo IMF, ndugu zake ambao waliwasili siku chache zilizopita, na baadhi ya Watanzania kadhaa waishio maeneo ya Washington DC.

Balali alizaliwa mwaka 1942 huko Iringa. Baada ya Elimu ya msingi na sekondari alipata shahada ya kwanza katika Uchumi mwaka 1965 toka Chuo Kikuu cha Howard nchini Marekani na kupata shahada ya pili toka Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Marekani miaka miwili baadaye.

Alijiunga na Benki Kuu ya Tanzania mwaka 1967 na kupanda ngazi taratibu hadi kufikia cheo cha Ukurugenzi wa Utafiti mwaka 1973. Baada ya hapo ndipo alipoanza kazi katika shirika la Fedha Duniani, IMF hadi mwaka 1997 alipoitwa nyumbani na Rais Mkapa na kuteuliwa kuwa mshauri wa Rais mambo ya Uchumi. Mwaka 1998 aliteuliwa na Rais kuwa Gavana mpya wa Benki Kuu

Ballali ameacha mke na familia.

SOURCE: Alasiri

Mkutano Umeanza - Karibuni!

Pastor Jared and Mrs. Gisele Mlongecha, together with the Family of the International Gospel Church invite you to join us as we celebrate our ‘10th Year Anniversary’. Our Annual Conference also coincides with our Anniversary. WELCOME!Dates:Thursday, May 22, 2008 – Sunday, May 25, 2008Venue:International Gospel Church85 Crescent AvenueChelsea, MA 02150For more information call: 617-884-1951

*************************************
HARVEST RAIN MIRACLE CONFERENCE PROGRAM
Friday, May 23rd, 2008
9:00am – 2:00pm In Depth Biblical Teaching
6:00pm – 9:00pm Miracle Service
Saturday,May 24th 2008
9:00am – 2:00pm Workshops Couples, Singles, Youth (Teens)
6:00pm -9:00pm Miracle Service
Sunday, May 25th, 2008
10:00am – 1:00pm Worship Service

Anniversary Celebration

6:00pm - 10:00pm
Sit Down Dinner

Live Concert featuring Les Mas, Wimbo Mpya
and IGC Worship Team
Suggested Donation
Adults $20.00 Children $10.00

Mwanamke aliyekufa Afufuka!



Ama kweli maombi yanasaidia. Huko Cleveland, Ohio Bibi Val Thomas (59) alikufa hospitalini. Ubongo wake uliacha kufanya kazi masaa 17, moyo ulisimama mara tatu na mwili ulianza kuganda (rigor mortis) na kubadilika rangi.

Bibi Thomas alikuwa kwenye life support, wakati wanafamilia na madatari wanamua wanfaye nini kuhusu Organ donation, yaani kutoa moyo, mafigo, ini, mapafu nk. kwa ajili ya watu wengine wanayezihitaji.

Walizima mashine, huko watu wanalia. Alishagwa na kusomewa sala za mwisho. Ndipo yule mama alianza kuongea na kufungua macho! DOH! Maombi yalijibiwa. Sasa madaktari wanasema atakuwa mzima tu hatakuwa na aathari zozote mwilini kutokana na kifo.

Bibi Thomas anasema anashukuru kuwa yu hai na kuwa lazimaMungu ana mpango naye, kuna kitu ambacho Mungu anataka afanye.

Kusoma habari zaidi na kuona video BOFYA HAPA:

Thursday, May 22, 2008

Mwalimu Obain amekuwa DEPORTED!

Maandamano nje ya Ofisi za INS mwaka 2005
Mwalimu Obain (pichani)



Yaani kuna ushenzi na washenzi kwenye ofisi za INS (Uhamiaji) hapa Boston! Leo tumepata habari kuwa Mwalimu Obain Attou0man (raia wa Ivory Coast) alikuwa DEPORTED jana. Tena INS walimtorosha kimya kimya!
Kisa, mwaka juzi walipotaka kumdeport wanafunzi wake na watu wengine waliandamana kwenye ofisi za INS Boston. Pia walimwomba Senator Kerry na Senator Kennedy waingilie kusimamisha deportation order. Senator Kerry aliingilia na walitoa amri kuwa apewe residency (haki ya kukaa Marekani). Congress walilalia na ile order ilikwisha juzi, haikupita. Hivyo Mwalimu Obain alivyoenda kureport kama kawaida huko Ofisini INS Boston walimkamata!

Ameonewa huyo kaka! Ni mtu mwema, ni mwalimu mzuri sana wa hesabu Fenway High School (na hapa Marekani kuna upungufu). Ajabu ameoa mMarekani lakini bado wamemfukuza.

Haya sasa kampeni imeanza ya kumrudisha Marekani. Arudi kwa wanafunzi wake hapa. Yaani wanalia si mchezo. Na lazima niseme, siku hizi ni walimu wachahe sana hapa wanaopendwa na wanafunzi.
Kwa kifupi alfika Marekani kama mwanafunzi miaka ya tisini. Aliomba hifadhi (political asylum). Alikosea kusoma tarehe ya hearing kwenye notisi. Ndo walianza kumdeport.

Habari zinasema kuwa amefika salama huko Ivory Coast.

STAY STRONG Mr. OBAIN! You are not a criminal, you are a law abiding, caring and skilled person who does not deserve to be treated like you have. Our children need postive black role models like you!
Kwa habari zaidi BOFYA HAPA:

Kifo cha Mzee Ballali kimetangazwa Rasmi Washington D.C.


Daudi Timothy Said Ballali

Viewing: PrivateService: May 23, 2008 @ 10AM
Location: St. Stephen The Martyr

Daudi Timothy Said Ballali
On May 16, 2008 of Washington, D.C.
Husband of Anna Ballali

Mass of Christian Burial will be offered on May 23, 2008 at 10AM at St. Stephen, Washington, D.C.
Interment Gate of Heaven Cemetery


http://www.devolfuneralhome.com/index.asp?sid=6&formid=102&serviceid=960

REST IN ETERNAL PEACE, Mzee Ballali.

Eti Balali Amefariki hapa Boston, MA?

Wadau, tangu juzi nimepigiwa simu na wadau wengi kuniuluiza kama Mzee Balali alikuwa hapa Boston, Massachusetts kwa matibabu. Ukweli sijui na wala sikuwahi kusikia kama yupo hapa. Niliambiwa kuwa alifariki Washingtion D.C. siku ya Ijumaa iliyopita.

Kwa kawaida mtu akifariki hapa kuna kuwa na matangazo kwenye gazeti kama Boston Herald na Boston Globe. Bado sijaona Obituary yake. Kama nikiona nitaiposti hapa.

Sasa nashangaa jana Ippmedia.com walisema kuwa serikali imetangaza kuwa Mzee Balali alifariki Washington D.C., leo wanasema amefariki hapa Boston. Niko confused sasa. Juu ya hayo kuna mtu alisema Mzee Balali yu mzima na anategemea kuwasili Dar es Salaam kesho! Heh!

Mnaonaje hii issue wadau?

***********************************************************************
Kutoka ippmedia.com

Yes, Ballali is dead - BoT

2008-05-22

By Angel Navuri and Correspondent Njonanje Samwel

The Bank of Tanzania confirmed yesterday that its immediate former governor, Daudi Ballali, is dead. A section of the media broke the surprise sad news yesterday morning, as the nation awaited word on developments relating to a saga on grand corruption allegations involving him.

A statement issued by BoT said the office of central bank Governor Benno Ndulu had learnt with shock on Tuesday night that Ballali died on Friday last week in Boston, the US, where he was understood to have been undergoing treatment.

``We at the Bank join the late Ballali`s family in mourning his death and pray to God that his soul rest in eternal peace,`` read part of the statement. Neither Foreign Affairs and International Cooperation minister Bernard Membe nor his deputy, Seif Ali Iddi, could be reached for comment on the issue yesterday.

However, a man who identified himself as a close Ballali relative said in an interview with this paper that the former governor died last Friday in the US ``after long but undisclosed illness``. At the residence of Ballali's sister at Boko in suburban Dar es Salaam, The Guardian found scores of people assembled to mourn his death.

The woman was identified only as Eliza, while the people at her residence were said to be family members, close relatives, family friends and neighbours. ``It`s true that Ballali is no more. We are gathered here as family members to discuss what to do,`` said an informer, who flatly refused to give his name.

According to a close Ballali relative, family members were having a hard time planning how to break the sad news to the former BoT chief's ailing mother. She is said to have heart problems and is currently cared for at Eliza`s residence.

Ballali was taken to South Africa last year after developing health problems. He was later flown to Boston for further medical attention, where he was subsequently admitted. Last December doctors there released him after his condition improved, instructing him to stay home for three months - until March this year - before returning to the hospital.

But his condition soon reportedly began deteriorating, forcing his doctors to order his re-admission. President Jakaya Kikwete relieved Ballali of his duties after revelations that the former governor had occasioned a loss amounting to billions of shillings through shady dealings with phony companies in 2005. Sooner after, the president named Prof Ndulu as Ballali's successor at the central bank.

Ernst & Young, the international auditing firm contracted by the government to screen the central bank`s accounts, revealed that payments amounting to 133,015,186,220/74 were dubiously made to 22 domestic companies under the External Payments Arrears (EPA) account scheme in 2005. Some 90,359,078,804/- out of this was paid to 13 companies on the strength of fake or forged documents.

Another nine firms were said to have been paid an equivalent of 42,656,107,417/- without any documents to support their claims.

Majina Yatajwa - tuzo za Vinara wa Filamu Tanzania

Press Release Kutoka One Game:

Habari yako ndugu yangu...
Kwa kifupi kinyang'anyiro cha Tuzo za Vinara wa Filamu Tanzania kinakaribia kufika ukingoni, ambapo leo majaji wametangaza rasmi majina ya waigizaji na filamu zilizoingia katika hatua ya mwisho.
Majina yalitolewa katika ukumbi wa mgahawa wa Hadees Fast Food!
Asante sana kwa ushirikiano wako wa awali!
Tupo pamoja!


****************************************************************
TUZO ZA VINARA WA FILAMU TANZANIA (TANZANIA FILM VINARA AWARDS) 2007 – 2008

Muigizaji Chipukizi wa Kike (Up coming actress)
1. Irene James – Miss Bongo II
2. Irene Uwoya – Diversion Of Love
3. Fatuma Makame – Karibu Paradiso
4. Jennifer Mwaipaja – Silent Killer
5. Grace Michael – Malipo ya Usaliti

Muigizaji Mwandamizi wa Kike (Best Actress in a Supporting Role)
1. Irene Uwoya - Diversion Of Love
2. Mama Frank – Yolanda
3. Irene James – Miss Bongo II
4. Susan Lewis – Behind the Scene
5. Tecla Mjata – Macho Mekundu

Muigizaji Bora wa Kike (Best Actress)
1. Lucy Komba - Diversion Of Love
2. Grace Michael – Malipo ya Usaliti
3. Halima Yahya – The Stranger
4. Elizabeth Chijumba – Copy
5. Riyama Ally – Fungu la Kukosa

Muongozaji Bora wa Filamu (Best Film Director)

1. Gervas Kasiga – Fake Pastors
2. Jimmy Mponda – Misukosuko II
3. Kulwa Kikumba – Macho Mekundu
4. Haji Adam – The Stranger
5. Halfan Ahmed – Copy

Mtunza Sauti Bora (Best Soundman of The Year)
1. Adam Wazir – Fungu la Kukosa
2. Cleophance Ng’atingwa – Kolelo
3. David Sagala – Copy
4. Camillius Kanuli – Fake Pastors
5. Swalehe Juma – Fungu la Kukosa

Mpiga picha Bora wa Filamu ( Best Cameraperson of The Year)
1. Mbalikwe Kasekwa – Misukosuko II
2. Sylon Malalo – Kolelo
3. Rashid Mrutu – Copy
4. Nicholaus Mtengwa – Kilio moyoni
5. Sylon Malalo – Simu ya Kifo

Adui Bora wa Filamu (Best Film Villain)
1. Mohamed Aziz – The Body Guard
2. Irene Uwoya - Diversion Of Love
3. Sebastian Mwanangulo – Misukosuko II
4. Ahmed Ulotu – Silent Killer
5. Elizabeth Chijumba – Copy

Mhariri Bora wa Filamu (Best Film Editor)
1. Moses Mwanyilu – Misukosuko II
2. John Kalage – Miss Bongo I
3. Rashid Mrutu – Copy
4. Hassan Mbangwe – Malipo ya Usaliti
5. Sylon Malalo – Kolelo

Mwandishi Bora wa Filamu (Best Script Writer)

1. Seleman Mkangara – Malipo ya Usaliti
2. Hammie Rajab – Kolelo
3. Kulwa Kikumba - Diversion Of Love
4. Lucy Komba – Utata
5. Elizabeth Chijumba – Copy

Muigizaji Bora Mwandamizi wa Kiume (Best Actor in a Supporting Role)
1. Aliko Tshmwala – Segito
2. Single Mtambalike – The Stranger
3. Adam Kuambiana – Fake Pastors
4. Halfan Ahmed – Copy
5. Emmanuel Muyamba – Fake Pastors

Muigizaji Chipukizi Bora wa Kiume (Best New And Upcoming Actor)
1. Emmanuel Muyamba – Fake Pastors
2. Laurent Anthony – Karibu Paradiso
3. Hassan Nguleni – Body Guard
4. Yussuf Mlela - Diversion Of Love
5. Uswege – Malipo ya Usaliti

Muigizaji Bora wa Kiume (Best Actor)

1. Single Mtambalike – Agano la Urithi
2. Nurdin Mohamed – Utata
3. Jacob Steven – Copy
4. Haji Adam – Miss Bongo
5. Yussuf Mlela - Diversion Of Love


Mapambo na Maleba Bora (Best Costume And Makeup of The Year)
1. Misukosuko II
2. Macho Mekundu
3. Kolelo
4. Utata
5. Copy

Mtunzi Bora wa Filamu (Best Creater of The Year)
1. Lucy Komba – Utata
2. Nicholaus Mtitu - Diversion Of Love
3. Single Mtambalike – The Stranger
4. Halfan Ahmed – Copy
5. Hammie Rajab – Kolelo

Filamu Bora ya Mwaka (Best Movie of The Year)
1. Behind the Scene
2. The Stranger
3. Diversion Of Love
4. Macho Mekundu
5. Misukosuko II
6. Simu ya Kifo
7. Copy
8. My Sister
9. Silent Killer
10. Miss Bongo I
11. Agano la Urithi
12. Malipo ya Usaliti
13. Utata
14. Kilio Moyoni (Crying Silently)
15. Fake Pastors

Wednesday, May 21, 2008

Habari zaidi kuhusu Kifo cha Balali

Hayati Dk. Daudi Balali (picha kutoka Michuzi Blog)

Written by KLHN/Tanzania Daima

Wednesday, 21 May 2008

KLH News imeweza kuthibitisha kwa uhakika kuwa misa ya kumuombea Marehemu Balali inatarajiwa kufanyika saa nne asubuhi katika Kanisa la Mt. Stephen Washington DC. Kutoa heshima za mwisho kutafanyika katika kanisa hilo hilo na itakuwa si kwa hadhara nzima.

Mwili wake unatarajiwa kulazwa kaburini kwenye makaburi ya "Gate of Heaven" huko hukoJamaa wa karibu wa Ballali walioko Dar es Salaam na Washington walilithibitishia Tanzania Daima kuhusu kutokea kwa msiba huo.

“Ni kweli amefariki nyumbani kwake Ijumaa usiku. Na sasa hivi tuko katika maandalizi ya kwenda funeral home (taasisi ya kuandaa shughuli zote za mazishi) kwa ajili ya kuanza kufanya maandalizi kwa ajili ya msiba,” alisema ndugu wa karibu wa Ballali kutoka Washington.

Habari zaidi zinaeleza kwamba, tayari familia ya gavana huyo wa zamani wa BoT imeshaitaarifu serikali kuhusu kutokea kwa msiba huo na kwamba taarifa rasmi kuhusu kifo hicho zitatolewa leo hii.Ndugu mwingine wa karibu wa Ballali aliyezungumza na Tanzania Daima majira ya saa 4:00 usiku jana alisema mazishi ya gavana huyo wa zamani wa BoT yanatarajiwa kufanyika Ijumaa hii huko huko Marekani.

Mmoja wa wanasiasa aliye karibu na familia ya Ballali aliyezungumza na Tanzania Daima jana alithibitisha pia kupokea taarifa za kifo cha Ballali kutoka kwa mkewe, Anna Muganda. Ndugu mmoja wa Ballali alipoulizwa na Tanzania Daima sababu za kushindwa kutangazwa kwa taarifa za kifo hicho mapema alisema walilazimika kufanya hivyo ili wapate fursa ya kuwasiliana na serikali kwanza na kisha ndugu, jamaa na marafiki wa familia yao kabla ya habari hizo kusambazwa.

Badhi ya jamaa za Ballali waliozungumza na Tanzania Daima walisema kulikuwa na wasiwasi kwamba kifo cha gavana huyo wa zamani wa BoT kikawa kikawa si cha kawaida.“Kuna wasiwasi kwamba huenda alilishwa sumu wakati akiwa nchini mwaka jana na hili limekuwa likizungumzwa sana ndani ya familia,” alisema mmoja wa jamaa za karibu wa Ballali aliyezungumza na Tanzania Daima jana.

Taarifa za kuwapo kwa wasiwasi wa Ballali kulishwa sumu zilipata kusikika mwaka jana na wakati fulani ilielezwa kwamba alipelekwa Marekani kwa matibabu kutokana na sababu hizo.

Habari za kifo hicho cha Ballali ambaye uteuzi wake ulitenguliwa na Rais Jakaya Kikwete Januari mwaka huu zimekuja siku chache tu baada ya serikali kupitia Ofisi ya Rais Ikulu kutoa tamko la kutangaza kwamba ilikuwa haimtafuti gavana huyo wa zamani wa BoT.

Tamko hilo la serikali lilitolewa mbele ya waandishi wa habari na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Ikulu, Salvatory Rweyemamu.Rweyemamu alisema kuwa serikali ina mkono mrefu na iwapo itafikia hatua ya kumtafuta gavana huyo wa zamani wa BoT ili aje atoe maelezo yake kuhusu wizi wa zaidi ya shilingi bilioni 133 uliogundulika katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) haitashindwa kamwe kumfikia alipo.

Alisema kutokuwepo nchini kwa Ballai, au kutojulikana alipo, si jambo linaloisumbua serikali kwa sasa kwa sababu hivi sasa yeye ni raia wa kawaida, hivyo anao uhuru wa kuishi popote anapopenda.“Serikali haimtafuti Ballali (kwa sasa), lakini ikiamua kufanya hivyo haitashindwa.

Kwanza ni private citizen (raia huru) siyo mwajiriwa wa serikali tena,” alisema Rweyemamu na kuongeza kuwa, mkono wa serikali ni mrefu hautashindwa kumpata Ballali iwapo itamhitaji. kifafanua zaidi, alisema baada ya kutenguliwa kwa uteuzi wake, serikali iliunda timu ya kuwachunguza watuhumiwa wa EPA, kuhakikisha fedha zilizoibwa zinarudi na kuwachukulia hatua waliohusika, akiwemo Ballali.

Alisema: “Ninachofahamu ni kwamba, timu iliyopewa kazi kuhusu ubadhirifu wa EPA inaendelea na kazi yake na tunaona jinsi fedha zinavyorudishwa.”Mkurugenzi huyo pia alikiri kwamba serikali haifahamu hospitali aliyokuwa akitibiwa Ballali, licha ya Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkullo, kukaririwa akisema alimtafuta Ballali bila mafanikio alipokuwa jijini Washington, Marekani.

“Kwa kweli sifahamu hasa Ballali alikuwa akitibiwa katika hospitali gani, lakini najua alikuwa nchini Marekani katika Jimbo la Boston, ila hospitali kwa kweli siijui.“Lakini huyu ni mtu huru hivyo anaweza kuishi popote… huyu ana nyumba yake nchini Marekani… yupo huko anaishi na familia yake,” alisisitiza Rweymamu katika ufafanuzi wake.

Wiki iliyopita, ikiwa ni siku chache tu baada ya taarifa hiyo ya Ikulu, vyombo kadhaa vya habari viliandika habari zilizokuwa zikieleza kuwa makachero kutoka hapa nchini, walikuwa wamekwenda nchini Marekani katika miji ya Boston na Washington kufuatilia nyendo na maisha ya gavana huyo wa zamani.

Kwa mujibu wa habari hizo, ambazo zilikariri taarifa za ndani kutoka serikalini, makachero hao walikuwa wamekwenda huko ili kujua mahali anakoishi ili wakati wa kumhitaji utakapofika iwe rahisi kumpata. Ballali aliondoka nchini, Agosti mwaka jana kwenda Marekani kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kwa matibabu, na tangu wakati huo taarifa zake zilikuwa ni zenye utata mkubwa.

Mara ya mwisho kwa Ballali kuonekana hadharani ilikuwa ni Julai 12 mwaka jana alipozungumza na wanahabari na akasema alikuwa hatarajii kujiuzulu wadhifa wake kutokana na kukabiliwa na tuhuma za ubadhirifu.

Katika mkutano huo, Ballali alisema madai ya ubadhilifu yanayotolewa dhidi yake ni uzushi na uongo mtupu.Huku akionekana kujiamini alisema; “Niko Comfortable, moyo wangu mweupe, ari yangu ya kazi iko juu kwani tuhuma hizo ni uongo na uzushi mtupu na siwezi kujiuzulu kwa tuhuma zisizo na ushahidi.

“Tuhuma zote dhidi yangu ni za uongo mtupu. Kwanza sijui zimetoka wapi, nani mtunzi na kwanini amefanya hivyo. Hilo tunawaachia wanaofanya uchunguzi na naamini siku moja atajulikana na ukweli utajulikana, lakini mimi siwezi kujiuzulu kwa mambo ya uzushi,” alisisitiza.

Kashfa ya BoT kupitia mtandao wa Internet, uliibuliwa mara ya kwanza Bungeni na Mbunge wa Karatu, Dk. Wilbroad Slaa (CHADEMA).Akichangia maoni ya kambi ya upinzani wakati wa mjadala wa hotuba ya bajeti ya Wizara ya Fedha, Dk. Slaa alisema kambi ya upinzani imefarijika baada ya Waziri wa Fedha kukiri kufahamu taarifa aliyoitoa Bungeni kuhusu ubadhirifu mkubwa ndani ya BOT unaomgusa Ballali, pamoja na wafanya biashara wengine wakubwa akiwemo Mbunge wa Kwela, Dk. Chrisant Mzindakaya (CCM), kupitia kampuni anayoimiliki.

Dk. Slaa alisema Dk. Mzindakaya alichukua mkopo kwa shughuli za kampuni yake ya SAAFI wa sh 6.217 bilioni, uliogawanyika kama ifuatavyo. Alisema aliomba ‘Overdraft facility ya 450 millioni zitakazolipwa kwa miaka 5; mkopo wa shs 2.8 bilioni zitakazolipwa katika miaka mitano; na Dola za Marekani 2.528. Jumla yote ni Bilioni 6.217.

Kwa mujibu wa Dk. Slaa, fedha zote zilikopwa Benki ya Standard Charter na Benki Kuu ilitoa (Guarantee) mdhamana wa asilimia 100. Mwaka huu wa 2007 Benki kuu kutokana na Mdhamana huo tayari imelipa kiasi cha sh 8.1 Billion kwa niaba ya Mzindakaya na fedha hizo pamoja na riba zinakisiwa kufikia 9.7 billioni hadi sasa (Hati ref. CIBD-14662 ya tarehe 24 May, 2007, na mkopo kutolewa 2005.

Kutokana na tuhuma hizo, Meghji wakati akifanya majumuisho ya hoja yake, alisema Serikali imeagiza kuanza kufanyika kwa uchunguzi wa tuhuma za ubadhirifu wa fedha katika akaunti ya madeni ya biashara ya nje zinazoikabili Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Alikiri serikali kupata taarifa za kuwapo kwa vitendo vya rushwa na nyingine za matumizi mabaya ya fedha katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Waziri Meghji alisema, tayari alikuwa ameshamwagiza Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Fedha za Serikali, kuanza uchunguzi kuhusu tuhuma hizo.Meghji alisema, serikali ilikuwa ikitarajia kukamilisha kazi hiyo na taarifa kamili ya uchunguzi huo kutangazwa ifikapo mwishoni mwa mwaka huu.

Mbali ya BoT kutuhumiwa kutumia fedha nyingi kuliko inavyostahili katika ujenzi wa majengo yake mapya ya ‘minara miwili pacha’ (Twin Towers), kiasi cha Dola za Marekani milioni 30.8 sawa na shilingi bilioni 40 kinatuhumiwa kufujwa katika akaunti ya madeni ya biashara ya nje.

Taarifa zinaonyesha kuwa, wakopeshaji wa kimataifa kutoka nchi 12 waliingia mkataba wa kusimamia akaunti hiyo na kampuni ya Kitanzania ijulikanayo kwa jina la Kagoda Agriculture Ltd kati ya Septemba na Novermba mwaka jana.Uchunguzi wa awali wa wakaguzi wa nje wa mahesabu ya akaunti hiyo unaonyesha kuwapo kwa mazingira yenye utata mkubwa unaozingira makubaliano kati ya wakopeshaji na kampuni hiyo iliyolipwa dola milioni 30.8.

Akichangia hotuba ya Waziri Mkuu, Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe (CHADEMA) alihoji kwa nini Serikali ilikalia kimya suala la kashfa ya BoT mara baada ya habari za kashfa kutangazwa kupitia mtandao wa internet tangu Novemba 2006 na kuonya kuwa hali hiyo inaathali kubwa kiuchumi iwapo kashfa kama hizi zinaachwa bila ya ufuatiliaji wa serikali.

Taarifa za awali za uchunguzi huo zinaonyesha kuwa, BoT ilifikia hatua ya kuipa kampuni hiyo fedha zote hizo ikidai kuingia mkataba na wakopeshaji hao katika mazingira ambayo nyaraka zilizopatikana zinaonyesha kuwa na hitilafu nyingi.Miongoni mwa hitilafu zilizobainishwa katika uchunguzi wa awali ni, kukosekana kwa karatasi rasmi zenye majina ya makampuni hayo ya kimataifa.

WaTanzania Ondokeni South Africa!

WaSouth Afrika wakitafuta raia wa kigeni!

Yaani nimechukia kweli kusikia hizi habari za wahamiaji kutoka nchi za Afrika huko Afrika Kusini kunyanyaswa na kuuliwa. Hebu cheki huo ukuta huko Afrika Kusini. Kuna mshenzi kaandika kwa rangi nyekundu nchi za watu wasiotakiwa. Kweli hao watu si binadamu. Wamesahau ni nchi hizo zilizowasaidia kutoka kwenye mikono ya Apartheid! Mwalim Nyerere lazima anajigeuza huko kaburini kwake.


Kwa habariz zaidi someni:



Dr. Daudi Balali Amefariki!

Habari kutoka ippmedia.com zinasema kuwa aliyekuwa Gavana wa Beni ya Tanzania, Daudi Balali alifariki dunia siku ya Ijumaa iliyopita tarehe 5/16/08 huko Washingtom D.C.. Atazikwa Washington D.C. kesho. Sasa hii siri aliyotake kufichua ni upi? Naona kazi ya wapelelezi umeisha. Wanaweza kurudi Tanzania na kupeleleza mambo mengine.

****************************************************************
Kweli Balali kafariki!

2008-05-21

Na Mwandishi Wetu, Jijini


Aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, BOT, Dokta Daud Balali amefariki dunia. Habari za uhakika zilizolifikia gazeti hili kutoka vyanzo vyake nchini na huko Marekani, zimethibitisha kuwa Dk. Balali alifariki dunia Ijumaa iliyopita.

Vyanzo hivyo vimedai kuwa Dk. Balali alifariki baada ya mashine iliyokuwa ikimsaidia kupumua kuondolewa. Aidha, vyanzo hivyo vimedai kuwa kabla ya kifo chake, Dk. Balali aliandaa ujumbe mzito, ambao ndani yake umeanika ukweli wote kuhusiana na tuhuma mbalimbali zilizokuwa zikielekezwa kwake, ikiwa ni pamoja na zile zinazohusiana na kashfa ya upotevu wa mabilioni ya pesa za nchi kupitia akaunti ya malipo ya madeni ya nje, EPA.

Alasiri imeambiwa na vyanzo hivyo kuwa Dk. Balali alimkabidhi ujumbe huo wenye siri zote ndugu yake mmoja anayemuamini na kumpa maelekezo ya namna ya kuufikisha kunakohusika na hatimaye Watanzania kujua ukweli wa suala zima.

Hata hivyo, chanzo hicho kimedai kuwa hadi sasa haijafahamika ni ndugu yupi ameachiwa ujumbe huo. Imedaiwa zaidi na chanzo hicho kuwa Dk. Balali aliamua kuandaa ujumbe huo wenye siri zote kwa vile hakutaka achafuliwe peke yake wakati wahusika wa sakata hilo wapo na anawafahamu.

Aidha, imedaiwa alikuwa akisema kuwa hakutaka aondoke na siri nzito kuhusiana na yote aliyokuwa akielekezewa kidole. Dk. Balali alifukuzwa kazi na Rais Jakaya Kikwete baada ya uchunguzi uliofanywa na Kampuni ya Kimataifa ya Ernst &Young kubaini upotevu wa Shilingi Bilioni 133 zilikuwa zimechotwa BOT kupitia EPA wakati wa uongozi wake.

Dk. Balali alienguliwa nafasi ya ugavana na Rais wakati akiwa nje ya nchi kwa matibabu na tangu wakati huo, hakuwahi kurejea nchini mpaka umauti ulipomkuta. Habari zinadai kuwa Dk. Balali anatarajiwa kuzikwa keshokutwa huko Jijini Washington DC, Marekani.

SOURCE: Alasiri

Tuesday, May 20, 2008

Daudi Balali Asakwa na Wapelelezi Marekani!


Sijui yataishaje. Wengine wanasema Mzee Daudi Balali (pichani) amefariki, (soma Jamii Forums) wengine wanasema amejificha Boston au Washington D.C. hapa Marekani!

Kuna hii habari iliyotoka jana kwenye African Baraza kuwa Mzee Balali anasakwa na wapepelezi kuhusiana na wizi wa dola $133 milioni kutoka Benki Kuu ya Tanzania.

****************************************

Detectives Hunt for Ex-Governor

By ADAM LUSEKELO

Dar-es-Salaam, Tanzania

Posted On: 19/05/2008

A team of local investigators is currently in the United States attempting to trace the whereabouts of former Bank of Tanzania governor Daudi Ballali, as part of the ongoing investigation into the theft of over $133 million from the central bank’s external payment arrears (EPA) account.

Well-placed sources have said at least seven detectives are combing Washington DC and Boston in a bid to locate the ex-governor – a central figure in the investigation, who has surprisingly not been officially questioned by authorities.

But with less than eight weeks to go before the expiry of the six-month deadline given by President Jakaya Kikwete to the EPA investigations team lead by Attorney General Johnson Mwanyika, the focus now seems to be firmly shifting onto Balali.

“There is a team of Tanzanian investigators in the US right now, apparently trying to locate Ballali. It isn’t clear if their orders are to arrest or just question him,” said a source familiar with the investigation.

“The clock is certainly ticking for the EPA probe team to wrap up its work, and there have already been suggestions that the AG (Mwanyika) will ask the president for an extension of about two months to finish the job.” The source added.

A senior government official has confirmed that the US government has offered “full cooperation with Tanzanian authorities in tracking down Ballali.”

The US government revoked Ballali’s visa shortly after he was sacked from his job as governor by President Kikwete back in January, as a direct result of the EPA scandal discovery.

This comes amidst public speculation on Ballali’s health.There are growing suggestions that the condition of the ex-governor, who has been undergoing medical treatment in the US since last year is critical.

Some are sceptical. They claim that Ballali has been deliberately edged out of Tanzania to keep him from disclosing the names of those involved in the scandal.

“Since he went to the US nobody in government is revealing what he is suffering from. I think they are deliberately keeping him out of the country to keep him from naming names.” An informed source has said.

The Mwanyika team, which says it has so far recovered about half of the $133 million embezzled from the EPA account, has also come under strong criticism for failing to make to make any arrests so far.

Critics claim that this simply confirms that there is a cover up to shield big operatives from prosecution.

Mr Ballali is believed to have been one of the key architects in the scandal. Apart from authorising the dubious payments as central bank governor, he is also understood to have gone out of his way to get rid of the bank’s former external auditors Delloit & Touche of South Africa, after they uncovered suspicious payments from the EPA accounts in 2005/06 audit.

Michezo ya UMISSETA


Wadau, nani amewahi kushiriki michezo ya UMISSETA. Mimi niliwahi kushiriki kwenye mchezo wa Volleyball nikwa Tabora Girls. Sasa wanasema huenda michezo isifanyike mwaka huu!

****************************************************
UMISSETA sijui kama itafanyika -TMK

2008-05-20

By Abdul Mitumba, Temeke

Walimu wakuu wa Shule za Sekondari Manispaa ya Temeke, wameonyesha wasiwasi wao juu ya kukwama kwa michezo ya Shule za Sekondari nchini, UMISSETA, kutokana na tofauti ya mihula kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza na sita.

Tofauti hiyo inasababisha hata likizo za wanafunzi hao kutofautiana, hali inayotishia kutopatikana kwa wakati mmoja hasa ikizingatiwa michezo hiyo inapaswa kufanyika bila kuathiri masomo. Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya Michezo na Utamaduni kwa Shule za Sekondari ya manispaa hiyo, Meja Martine Mkisi, ameonyesha hofu hiyo na kuonya endapo serikali isipolipa uzito suala hilo, UMISSETA itakwama.

``Kila mtu anayefuatilia masomo kwa wanafunzi wa sekondari anaelewa mihula kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza hadi nne na wale wa kidato cha tano na sita inatofautiana, haitakuwa rahisi kwa wanafunzi hawa kuwaweka pamoja,`` amesema.

Amesema shule zilizomo katika manispaa hiyo zilipanga kuanza michuano ya UMISSETA wakati wa sherehe za Pasaka, lakini kutokana na ufinyu wa muda haikuwezekana. Mwenyekiti huyo ambaye pia ni mkuu wa Shule ya Sekondari Jitegemee inayomilikiwa na Jeshi la Kujenga Taifa, JKT, amesema endapo serikali imedhamiria kurejesha michuano hoyo ni lazima ifanye mabadiliko ya wakati ndipo itachezwa.

Novemba mwaka jana, Rais Kikwete alizindua rasmi michezo mashuleni kule mkoani Pwani na kuagiza utekelezaji wake uanze mwaka huu.

SOURCE: Alasiri