Thursday, February 07, 2008

Rushwa, Vistisho, Uchongoanishi....




Kamati ya Dr. Mwakyembe ilifanya kazi pamoja na kwa walitishiwa na kufanyiwa mambo mengine mabaya!


SEMA, USIOGOPE, SEMA!

Nasema mkono wa Mungu umetembea, maana kuna majina mazito yametajwa mle! DUH!

*********************************************************************

" Mheshimiwa Spika, leo tunapowasilisha taarifa hii mbele ya Bunge lako tukufu, tunajisikia kuutua mzigo mzito sana ulioanza kutuelemea kutokana na kuzongwa kila kukicha na kila aina ya uzushi, uchochezi, uchonganishi na hata vitisho. Tumezushiwa kuhongwa magari ya kifahari na fedha taslimu; tumetuhumiwa kuendesha vita dhidi ya Waislamu na mara nyingine tuhuma hiyo ikageuka kuwa vita dhidi ya Wakristo ndani ya Serikali; tumesingiziwa kuibadilisha taarifa yetu mara mbili, baadhi wakisema kwa ushawishi wa fedha, wengine wakidai kwa shinikizo la Mhe. Spika na wengine kwa shinikizo la Waziri Mkuu; tumeshuhudia pilikapilika za usiku na mchana za kujipanga na kuwashawishi baadhi ya Mawaziri na Wabunge kuikana taarifa hii na mapendekezo yake kiasi cha wengine wetu kujiuliza: kulikoni mtu asiye na hatia kuweweseka?

Mheshimiwa Spika, naomba kwa niaba ya wajumbe wenzangu wa Kamati Teule, kukuhakikishia wewe binafsi na Bunge lako tukufu kuwa tumekamilisha kazi tuliyopewa kwa uaminifu na ujasiri mkubwa, dhamira safi, moyo wa uzalendo na kwa kumtanguliza mbele Mwenyezi Mungu katika kila tulilolifanya. "

KUSOMA RIPOTI NZIMA BOFYA HAPA:

1 comment:

Anonymous said...

Nasema ni lazima walimficha Lowassa habari ya ripoti. Ajabu Mwakyembe hakupata ajali ya gari akiwa njiani kwenda Bungeni.