Saturday, June 28, 2008

Miss Zimbabwe 2008

Miss Zimbabwe 2008
Asante mdau Masoud kwa kuniletea hii picha.

6 comments:

Egidio Ndabagoye said...

Dah huyu sio Bob? kila nikimuona kwenye TV nasikia hasira

Anonymous said...

NADHANI PAMOJA NA MATATIZO YA HUYU MZEE KUNGÁNGÁNIA MADARAKA,

SIKUBALIANI HASILANI NA JITIHADA ZA KUMTUSI KWA KUMBADILISHA JINSIA YAKE KWA KUTUMIA TEKNOLOJIA YA PICHA!

PENGINE WANAOMPASWA KULAUMIWA NA (SIO KUTUKANWA) NI BAADHI YA WAZIMBABWE WENYEWE NA PIA BAADHI YA VIONGOZI WA AFRIKA NA HATA WA ULIMWENGU MZIMA.

DADA CHEMI USISHUKURU KWA PICHA HII MAANA HII NI KUPOSTI MATUSI KATIKA BLOGU YAKO!

NANYE,

NYAKARUNGU WA COAST

Anonymous said...

Mimi siwezi kushangaa kama Mugabe mwenyewe ataenda kwenye pageant na kujitangaza yeye ni Miss Zimbabwe. Zimemfyatuka huyo mzee!

Anonymous said...

mbona miguu yake safi sana

Anonymous said...

ndg.Nyakarungu wacha Mugabe atusiwe!kwani mbona yeye anatesa mamilioni ya wazimbabwe kwa njaa,vifo,ukimbizi,utawala wa mabavu,ubabe na udikteta!
mbona hasikitikii mateso wa wazimbabwe na amewageuza wazimbabwe kamangao au silaha ya kupambana na maadui zake(serikali ya uingereza na na marekani)na kambi ya upinzani?
je hii ni sawa anavyfanya mugabe?
na sasa anataka kuilazimisha mahakama inyonge katibu mkuu wa MDC-Tendai Biti.HILI KUWATISHA WATU NA UPINZANI.....!

Anonymous said...

Kwenye mkutano wa Africa wa kuzungumzia masuala ya maji na usafi (sanitation) uliokiendelea katka mji wa kitalii wa Sharm el_Sheikh, Bahari ya Shamu, Misri, msemaji wa Rais Mugabe, George Charamba, aliwajibu waandishi wa habari kuhusu swali la eti Rais Mugabe kujiuzulu wadhifa wake:

"Isn't that an odd question. He's a few days into office and you expect him to retire, do you? ... Five days have expired, not even a week after. ... Why is the issue of the retirement of the president of Zimbabwe such an obsession for the West?"

Msemaji huyo alipozidi kudadisiwa, alitamka kuhusu nchi za Magharibi:

“They can go hang. They can go and hang a thousand times."

Kauli ya ki-JONGWEISM = Pamberi na Chimurenga = Mapambano Yanaendelea = A Luta Continua = Viva le Liberación!

Maneno ya wakubwa,
Maneno ya wazee
Yote sawa
Kwa kumaliza ukoloni uliotokea
Tunawapa heko
Na tufe njaa
Sisi wote twakubali yote
Ni afadhali kuwa huru na masikini
Kuliko kuwa tajiri na mtumwa!

Madini yetu yanasombwa na matajiri wageni wakishirikian na mafisadi wenye kuunda kampuni nje ya Tanzania kuogopa kulipa kodi au kushitakiwa popote ili wanufaike na “vjisenti”!
Wakina Museveni (Uganda) na wWakina Raila Odinga (Kenya)na wakina Membe (Tanzania)nao wanajidai kumkosoa Mugabe na huku wanataka kuendelea kutawala Uganda milele kwa kushinikizwa na wakina Muamar Kaddafy (Libya); mikono yao imetapakaa damu (Kenya); na kushindwa kutatua “muafaka” (Tanzania)!

Wenye kumtakia mabaya Rais Mugabe: “They can go hang. They can go and hang a thousand times."