Tuesday, June 10, 2008

Ndege ya Sudan Airways imeanguka!


Habari kutoka CNN zinasema kuwa ndege ya Sudan Airways imeanguka huko Khartoum. Ndege ilikuwa inatokea Jordan. Watu zaidi ya 100 wamekufa.

Wiki hii imekuwa mbaya kweli kwa usafiri wa anga barani Afrika.

Juzi helikopta ilianguka Arusha, Tanzania. Leo asubuhi ndege ilianguka Kenya na kuua mawaziri wawili.

Mungu alaze roho wa waliopteza maisha mahala pema mbinguni. Amen.

1 comment:

Stella Fumbuka said...

Mungu awarehemu na kuwapa mapumziko mema wote waliopoteza maisha yao. Na walioumia wapate nafuu mapema na kuungana na familia zao.