Wednesday, June 18, 2008

Umeme Umerudi Zanzibar!

Habari kutoka BBC zinasema kuwa umeme umerudi Zanzibar leo. Sehemu ambazo bado hazijapata umeme ni zile ambazo nyaya za umeme ziliibiwa. Wanasema ni kama sikukuu huko leo kwa jinsi watu walivyo na furaha!

http://news.bbc.co.uk/2/hi/africa/7461995.stm

1 comment:

Anonymous said...

"Umeme Umerudi Zanzibar"

Ahsante Chemi tumeona kuwa umejali swala la Zanzibar.Kwani watu waliteseka sana hicho kipindi na kama unavyojua watu wa zanzibar wana ari hawawezi kulalamika wanavyoona wao hilo ni moja tu ya matatizo yao mengi ambayo hayashughulikiwi na Raisi wa Tanzania na mwenzake Raisi wa zanzibar.Kwa kweli ilitusikitisha sana kuono habari zote nyengine zinakuwa covered kinaga ubaga lakini tatizo la zanzibar halikuonekana ni kubwa kwa blogers wote wa Tanzania.Ni uzuri bloggers nyengine zifanye manufaa kwa jamii zetu yenyewe kwa kuwauliza leaders wetu everyday nini wanafanya kuwanufaisha wananchi wake.Tunaweza kusaidia nchi nyengine Africa lakini tazizo la zanzibar tunaliona machoni linatushinda watu wana njaa,maji hawana,umeme ndo kama hivyo.Kwa ufupi Mungu ibariki zanzibar na watu wake.Sisi tulipokuwa tukiongea na watu wetu tulikuwa tunaona uchungu.Wakati umefika kutatua matatizo ya zanzibar uchumi,siasa nk.Ahsante sana.