Friday, June 27, 2008

WAPI Zanzibar Juni 29, 2008!

JUMAPILI YA TAREHE 29 JUNI

WAPI ZANZIBAR INAWALETEA:


Lile tamasha la kila mwezi ambalo huwakusanya pamoja wasanii mbalimbali katika kunadi kazi zao. Tamasha hili na nafasi pekee kwa wasanii ambao hawafahamiki sana kuweza kujitangaza na kuthibitisha vipaji vyao.Wasanii husika ni pamoja na Waimbaji, Ma emsii, wachezaji, wachoraji, wabunifu wa mavazi, wafumaji, wachekeshaji washairi, waigizaji na wengine wengi.

KWA MARA YA KWANZA WAPI ZANZIBAR INAWALETE MASHINDANO YA WASANII WA JUKWAANI PAMOJA NA WACHORAJI NA WASHINDI WATAPATIWA NAFASI YA KUSHIRIKI KATIKA TAMASHA LA KIMATAIFA LA NCHI ZA JAHAZI.

Tamasha litafanyika katika ukumbi wa Ngome Kongwe (Old Fort) kuanzia saa 9 Alasiri hadi saa 2 usiku.

KARIBUNI MADA YA MWEZI HUU NI SANAA NI AJIRA "iendeleze ikuwezeshe"

No comments: