Monday, October 06, 2008

Coca Cola inaua shahawa!


Asante mdau 'Born Again Pagan' kwa habari hizi. Nilikuwa nimesikia fununu tu lakini sikufutalitia. Eti baada ya tendo la ndoa, ukitia hiyo soda ukeni inaua shahawa/mbegu za kiume. Basi ni contraceptive ya bei ya chini.

Kumbe soda aina ya Coca Cola ina matumizi mengi. Wengine wanasema eti inatoa kutu kwenye silver. Na wanasema ukitaka kutakasa choo umimine ndani na iache ikae kama nusu saa.

*************************************************************

Dada Chemi,

Hii habari sijui inapokelewaje?

Kuna habari kuwa Coke (Coca Cola) inaua shahawa - mbegu za kiume (spermicide)! Wataalamu wanaamini kuwa mchanganyiko wa Coke (Coca Cola) unaweza kutumika kama “contraceptive”, kulingana na utafiti bayana hapo karibu yako (Chuo Kikuu cha Harvard, Massachusetts)!Najua Coke inakula (au niseme inayeyusha chuma) chuma, kwa mfano msumari wa chuma. Sijui kama kuna uhusiano linganifu wa kunywa Coke (Coca Cola) na upungufu wa shahawa kwa wanaume!Fungueni: http://www.msnbc.msn.com/id/26996167/?GT1=43001

1 comment:

Anonymous said...

Lahaula! Sasa ukinywa inafanya nini huko tumboni!