Wednesday, October 22, 2008

Mambo si ndo Hayo - Flaviana Matata


Mnamkumbuka mrembo wetu, Flaviana Matata aliyefanikiwa kufika katika Top Ten wa mashindano ya Miss Universe mwaka 2007? Watu walimpenda na kusifia kipara chake. Sasa yuko South Afrika akiendelea na shughuli zake za modelling. Hivi karibuni ametoka katika matangazo (print ad) kwenye gaztei la True Love.

Flaviana, endelea na moyo wa kutaka kujiendeleza katika fani ya modelling. Na usiache huo mtindo wako wa 'natural'. Mungu akubariki!

*************************************************************

Picha na maelezo ya chini kutoka Michuzi Blog:

Mrembo wa Miss Universe Tanzania 2007, Flaviana Matata ambaye hivi sasa yuko nchini Afrika ya Kusini ameendelea kupanda chati baada ya kunyakua tangazo katika jarida la True Love.
Flaviana ambaye anaonekana amevaa mavazi mawili tofauti ukurasa wa 73, ameweza kupata mkataba huu.

Akieleza mkataba huu wa kutangaza nguo Flaviana alieleza," Huu ni mkataba mmoja tu, na hivi punde narajia tangazo langu la televisheni pia lianze kuonekana hapa South Africa na bara la Afrika".

Flaviana hakuwa tayari kuzungumzia mkataba wake mwingine hadi itakapoonekana lakini alieleza wazi kuwa hivi sasa anaendelea kupata mialiko mingi ya kazi (casting).

Flaviana Matata aliwakilisha nchi yetu kwa mara ya kwanza katika mashindano ya Miss Universe nchini Mexico ambapo alifanikiwa kushika nafasi ya 6. Hivi sasa yuko nchini Afrika Kusini akifanya kazi ya uanamitindo.

1 comment:

Anonymous said...

Anapendeza lakini mwembamba mno na hana matiti.