Friday, August 22, 2008

Kichekesho

Vp mambo DA CHEMI,Ni matumaini yangu u-mzima wa afya.
Nimependa kukutumia kichekesho hiki uweke katika blog ili tuweze kushare na
wadau. W.K.

****************************************************************

MFUNGWA MWAFRIKA

Mfungwa mmoja Mwafrika,alitoroka jela baada ya kukaa miaka 15.Katika
kukimbiakimbia akajikuta anaingia nyumba moja na kuwakuta mke na mume wamelala
kitandani wakiwa kama walivyozaliwa.

Mfungwa akatumia mabavu akamtoa mue kitandani na kumfunga kamba kwenye kiti,
kisha yeye akaenda kumbusu kwenye shingo mke wa jamaa.Ghafla akaingia bafuni.

Wakati yupo bafuni, jamaa mwenye mke akamwambia mkewe;

"Sikiliza mke wangu, huyo bwana anaonekana ni mfungwa, angalia magwanda
yake!!
Inaonekana amekaa sana jela na hajalala na mwanamke siku nyingi sana. Hivyo mpe
chochote atakacho na usibishe, hata akitaka penzi mpe vinginevyo atatuuwa wote
wawili. Fanya ufanyavyo ili umridhishe huyu bwana aende zake,vumilia
mpenzi,nakupenda sana na nitaendelea kukupenda zaidi.

Mke Akajibu;

" Ni kweli usemavyo mume wangu. Huyu bwana hajalala na mwanamke siku
nyingi,ila aliponibusu shingoni alininong`oneza kwamba,MUME WAKO NI MZURI NA
AMENIVUTIA ZAIDI,KUNA MAFUTA YOYOTE?"Nikamjibu yapo bafuni na ndiyo
kayafuata!!Vumilia mume wangu,nakupenda sana na nitaendelea kukupenda
zaidi."

KAZI NJEMA.

3 comments:

Anonymous said...

Safi sana!

Anonymous said...

Huyo mume alikuwa hampendi mke wake. Anamwambia akubali! Alikomeshwa huyo!

Anonymous said...

I've seen this joke before and it didn't not say anything about the prisoner being African; wonder who changed the joke!!