Sunday, April 20, 2008

Ditopile Afariki!


Habari kutoka Tanzania zinasema Ditopile Ukiwaona Mzuzuri amefariki dunia leo asubuhi katika hoteli moja huko Morogoro. Habari za kuaminikia zinasema kuwa Ditopile alikuwa anatazama TV ndipo kapata Heart Attack na kufa.

Kesi ya mauji ya Ditopile, ambayo Ditopile alimwua dereva wa daladala pale njia panda ya Bagamoyo Rd. ilikuwa isikilizwe hivi karibuni.
Mola ailaze roho yake mahala pema peponi. AMIN.

***************************************


BREKING NYUUUZZZZZZ

HABARI KUTOKA MOROGORO ZINASEMA ALIYEKUWA MKUU WA MKOA WA TABORA UKIWAONA ATHUMANI DITOPILE AMEFARIKI DUNIA LEO ASUBUHI KATIKA HOTELI MOJA MJINI HUMO.

JUHUDI ZINAFANYWA KUJUA CHANZO CHA MAUTI YAKE. UONGOZI WA HOSPITALI YA MKOA IMETHIBITISHA KIFO HICHO.
**************************************
Habari kutoka Ippmedia.com
Ditopile allegedly guns down daladala driver 2006-11-06

Police in Dar es Salaam are holding Tabora Regional Commissioner, Capt (rtd) Ukiwaona Ditopile Mzuzuri for allegedly shooting to death a commuter bus driver. Dar es Salaam Special Zone Police Commander Alfred Tibaigana told a news conference yesterday that Ditopile, who once served the government as deputy minister, allegedly shot Hasani Mbonde (33) in the head, killing him instantly.
According to Tibaigana, police are holding the regional commissioner, as investigations into the killing continues. He said Ditopile, who has been in the public service for many years, having served as RC in a number of regions, allegedly shot the bus driver at around 7.pm, at the junction of Kawe and Bagamoyo roads in Kinondoni District on Saturday.
Tibaigana said Mbonde, a resident of Kawe Mzimuni, was driving a commuter bus an Isuzu Journey with registration number T788 ACC, plying between Ubungo and Tegeta. Detailing on the incident, he said the commuter bus had collided with a Prado vehicle with registration number T816 AJT which was being driven by Nasoro Mohamed (42) a resident of Kijitonyama.
Ditopile was a passenger in the Prado.
The RPC said Ditopile was heading to Bagamoyo from Dar es Salaam, with another passenger whose name could not be immediately be obtained. He said preliminary investigation shows that shortly after the collision, Ditopile’s driver alighted from his vehicle, to establish the extent of the damage.
He discovered a minor damage at the rear of the vehicle.
However, Ditopile also got out of the car to assess the damage, went straight to the commuter bus driver and ordered him out of his vehicle. The driver allegedly refused to budge and shut the door and window of the bus. ”At this juncture, Ditopile drew a pistol and used it to knocked on the window of the bus, insisting that the driver should come out,” Tibaigana explained.
He said in the course of the wrangle, Ditopile allegedly fired at the driver through the glass window and killed him on the spot. Tibaigana said the body of the deceased is being preserved at the Muhimbili National Hospital mortuary. Prior to his appointment as Tabora RC, Ditopile, popularly known as ’Dito’ served as deputy minister in the then Communication and Transport ministry and as RC for Kigoma, Lindi and Coast Region. He once served as Ilala legislator and member

10 comments:

Anonymous said...

Kalogwa huyo!

Anonymous said...

Wabongo kweli wacha mungu, marehemu aliua tena hadharani, akapewa dhamana, kawa anakula kiulaini home kwake (anyway may be ilikuwa bahati mbaya)wakati wa uhai wake maoni yalikuwa very negative juu ya tukio hilo, leo kafariki maoni yote Mungu aiweke mahala pema roho ya marehemu. Hilo ndo kati ya machache ninayojivunia kuwa mtanzania, uvumilivu, upendo na zaidi kusamehe. Mungu azidi kutubariki. Rest in peace Brother DITO.

Anonymous said...

BP lazima impate kwa mambo yote aliyokuwa nayo.Wake wawili, kesi ya kuua, nyumba ndogo ....nk

Anonymous said...

MAZISHI YA MAREHEMU UKIWAONA MZUZURI DITOPILE YANATARAJIWA KUFANYIKA SIKU YA JUMANNE, KWA MUJIBU WA HABARI ZA KIFAMILIA. MAPEMA LEO JK ALIKWENDA KUTOA MKONO WA POLE KWA FAMILIA YA MAREHEMU DITOPILE MTAA WA MINDU, UPANGA, DAR.

Anonymous said...

Rest in Peace Kada wa CCM, Ukiwaona Ramadhani Mwinshehe Athumani Ditopile Mzuzuri

Unknown said...

rest in peace bro Ditto!poeni sana kyembe,ramadhani na all family members!

Unknown said...

msimhukumu mtu jamani,uwezo wa kuhukumu anao mungu pekee,na hapa duniani tunapita tuu!

Anonymous said...

Wee anony namba 2 hapo juu, hicho unachojivua kuhusu utanzania ndo "recipe" ya umasikini, upumbavu na uzembe uliostawi.
Na hata Lowasa, Mkapa, Sumaye, Kikwete na Balali (mijizi inayotutokomeza kwenye umasikini) ikifa, pia wapumbavu (wabongo) watasema "Mungu ziweke roho zao peponi".

Mimi namwomba Mungu, Mchome Ditopile moto mpaka ajinyee

Anonymous said...

Hata kama hiyo kesi ingekuwa nchi gani ni manslaughter, watu kwa kupaplish huku hata hiyo sheria yenyewe hawaijui. Bora Mungu alivyomchukua mja wake , maana angekuwa hai angehukumiwa kwa manslaughter na kwa ushabiki wa simba na yanga watu wangesema kapendelewa! Ijue sheria na vipengele vyake hakutoka nyumbani kwake kakusudia kwenda kumuua mtu!

Poleni wafiwa popote mlipo Mungu amuondoshee marehemu madhila ya kaburini na amuweke mahala pema peponi. Amin.

Kampumzike kwa amani baba watu maana ulikuwa huishi midomoni mwa watu!

Anonymous said...

Kweli Samba Mapangala aliimba,"Duniani tunapita, hakuna kitu kitabakia." Hakika hili limejidhihirisha. Mwenzetu ametutangulia hukumu ya haki, kitakachotokea huko hakuna anayejua. Hivyo si vyema kuhukumu na kufanya mizaha isiyo kifani. Mungu ni mkubwa na ndiye pekee ajuaye lipi njema na lipi mbaya na si kwa kupitia uelewa wa binadamu. Ilale pema roho ya Marehemu.