Saturday, April 05, 2008

Tanzania - John Mndolwa (ITV/Radio One)

Marehemu John Mndolwa

MWANDISHI Mwandamizi na Mratibu waHabari na Matukio wa televisheni yaITV na Radio One, John Mndolwa (46),amefariki dunia leo alfajiri majira ya saa 10 baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Kwa mujibu wa habari zilizotolewa naMkurugenzi Mtendaji wa ITV na Radio One, Joyce Mhaville, marehemu Mndolwa alilazwa hospitali ya Kairuki kwa wiki moja. Kifo chake kimesababishwa na shinikizo la damu.

Mndolwa ambaye alizaliwa Novemba 9,1962 mkoani Tanga alianza kazi za uandishi mwaka 1980 katika Idara ya Habari ya Radio Tanzania (RTD) na aliajiriwa na ITV na Radio One Julai 1994.
Mipango ya mazishi inaendelea kufanyika. soma zaidi habari hii ya kuhuzunisha kwa kwenda lukwangule.blogspot.com

Mungu ailaze mahala pema roho ya marehemu - AMINA/AMEN

No comments: