Saturday, April 26, 2008

Update - Mtoto Kichaa akutwa na kichwa cha mtoto


UPDATE - April 29, 2008

Mama mzazi wa mtoto salome yohana aliyechinjwa majuzi akilia kwa uchungu wakati akisaidiwa kuweka udongo kwenye kaburi la binti yake wakati wa mazishi tabata segerea jioni hii.

Picha kwa hisani ya issamichuzi.blogspot.com

**********************************************************


KUTOKA MICHUZI BLOG:

Katika kufuatilia tukio la huyu kijana pichani kukutwa na kichwa cha msichana leo asubuhi kule muhimbili, globu yenu imethibitishiwa kwamba jana usiku msichana mdogo alipotea nyumbani kwao tabata.

Inasemekana leo asubuhi ndugu wa marehemu walikuta kiwiliwili kitupu cha msichana huyo karibu na nyumbani kwao na wakaita polisi ambao wakaupeleka hospitali ya taifa ya muhimbili kwa uchunguzi. huko ndiko kichwa kinachosadikiwa kuwa cha kwake kikakutwa na huyu kijana kwenye geti la chuo kikuu cha tiba cha muhimbili ambapo mlinzi alimkamata.

Afande charles mkumbo, mkuu wa upelelezi kanda ya ilala, amethibitisha yote hayo usiku huu na kwamba kichwa hicho ni cha mtoto salome yohana mwenye umri wa miaka kati ya miaka 3 na 4 na kijana huyu ametambulwa kama ramadhani mussa na anashikiliwa na polisi yeye na mama yake kwa kutuma za kukutwa na kichwa cha mtu kwa kile kilichosemwa kuwa ni mambo ya kishirikina.

Kijana mussa mwenye umri wa miaka 12 inasemekana pia amewahi kukumbwa na mikasa mingine, ikiwa ni pamoja na kuanguka toka paa la kanisa la assemblie of God la msasaani analoongoza mh. getrude rwakatare. inasemekana baada ya mkasa huo ambapo alikuwa na mwenzie wa umri kama yeye walipelekekwa kupimwa akili muhimbili na kuachiwa baada ya kuonekana wana akili timamu.

3 comments:

Simon Kitururu said...

DUH:-(

Anonymous said...

Sasa watamfanya nini huyo mtoto? Anaweza kunyongwa kweli? Ingekuwa vyema kama wangemwua pale pale kama wanayoua wezi.

Anonymous said...

umeandika mtoto kichaa unauhakika gani kama ni kichaa?mhh